Mfungaji Bora NBC: Simba Sc imetuheshimisha

Mfungaji Bora NBC: Simba Sc imetuheshimisha

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
KINARA wa mabao wa Ligi Kuu Bara kwa msimu uliopita, George Mpole anayekipiga FC Lupopo ya DR Congo kwa sasa amesema kutinga kwa Simba katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika imeiheshimisha Tanzania na kutoa fursa kwa vijana kupata nafasi zaidi za kutoka nje ya nchi.

Simba ilipata ushindi wa mabao 7-0 juzi dhidi ya Horoya ya Guinea kwenye mechi ya Kundi C ya Ligi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa na kujihakikishia kwenda robo fainali ikiwa na mechi moja mkononi nyuma ya Raja Casablanca iliyokusanya pointi 13 na zitakutana Aprili Mosi.

Akizungumza na Mwanaspoti, Mpole alisema mafanikio ya Simba yameifanya Tanzania iendelee kutoa timu nne kwenye mashindano ya kimataifa kutokana na pointi walizozikusanya zisizoweza kufikiwa na nchi nyingine yeyote na hiyo ni heshima kubwa kwa taifa.
 
Na kwa jinsi hii nchi isivyo na shukrani, timu za NBCL (kama Prisons,Kagera,etc) Zina hamu ya kuwavunja miguu wachezaji wa Simba watakapokutana dimbani. Mtu kama Abdi Banda wala hana anachowaza zaidi ya kuwasababishia ulemavu wachezaji wa Simba. Huu ni upumbavu sana.

Sisemi kwamba wasiipe changamoto Simba, big NO! Waipe Changamoto ya kisoka na kihalisia, hii nyingine wanayofanya ni 'chuki kali dhidi ya Simba'.

Mbona Azam na hata Yanga huwa wanaocheza fresh tu na Simba,na hata kuifunga ila hatulalamiki? Unaichukiaje timu ambayo inasaidia timu nyingine 4 kushiriki michuano ya kimataifa? Muwe mnafikiri mara mbili mbili basi! Nyie vitimu vidogo visivyo na akili badilikeni.
 
Na kwa jinsi hii nchi isivyo na shukrani, timu za NBCL (kama Prisons,Kagera,etc) Zina hamu ya kuwavunja miguu wachezaji wa Simba watakapokutana dimbani. Mtu kama Abdi Banda wala hana anachowaza zaidi ya kuwasababishia ulemavu
Wamekusikia watakua hawapeleki timu uwanjani, ili wasije waumiza na kuwachosha wawakikishi wa kimataifa.
 
We mwenye kichwa chenye kona kona kama limao sijamaanisha hivyo! Timu wapeleke ila mambo ya Shaolin soccer waachane nayo. Mbona Azam hatujawahi kuwalalamikia pamoja na kuchukua mipoint yote mi4 kutoka kwetu?
Vita haichagui silaha dogo, ukikaa vibaya hata bomu la nyuklia hutumika, rejea hiroshima na nagasaki.

Usiwapangie wachezaje, ndio maana kuna marefa uwanjani kama mnaona hamtendewi haki si muwashtaki.
 
Vita haichagui silaha dogo, ukikaa vibaya hata bomu la nyuklia hutumika, rejea hiroshima na nagasaki.

Usiwapangie wachezaje, ndio maana kuna marefa uwanjani kama mnaona hamtendewi haki si muwashtaki.
Mfano wa hovyo kabisa kuwahi kutokea. Kwahiyo una akili sana kuwazidi wale walioleta dhana ya fair play?
 
KINARA wa mabao wa Ligi Kuu Bara kwa msimu uliopita, George Mpole anayekipiga FC Lupopo ya DR Congo kwa sasa amesema kutinga kwa Simba katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika imeiheshimisha Tanzania na kutoa fursa kwa vijana kupata nafasi zaidi za kutoka nje ya nchi...
Huyu ametusaidia kuweka rekodi sawa, na hansard za TFF ziseme hivyo 🤣😂🤣. Ni Simba iliyohakikisha Tanzania inapata hizo nafasi 4 msimu ujao.
 
Mfano wa hovyo kabisa kuwahi kutokea. Kwahiyo una akili sana kuwazidi wale walioleta dhana ya fair play?
Mpira una sheria zake dogo, kama hao unaowatuhumu wanafanya hayo usemayo sidhani kama hizo timu zingekuwepo mpaka leo kwa kuwacoach ujinga wachezaje wake.

Ama kah hao wachezaji wangefungiwa mazima.
 
Na kwa jinsi hii nchi isivyo na shukrani, timu za NBCL (kama Prisons,Kagera,etc) Zina hamu ya kuwavunja miguu wachezaji wa Simba watakapokutana dimbani. Mtu kama Abdi Banda wala hana anachowaza zaidi ya kuwasababishia ulemavu wachezaji wa Simba. Huu ni upumbavu sana.

Sisemi kwamba wasiipe changamoto Simba, big NO! Waipe Changamoto ya kisoka na kihalisia, hii nyingine wanayofanya ni 'chuki kali dhidi ya Simba'. Mbona Azam na hata Yanga huwa wanaocheza fresh tu na Simba,na hata kuifunga ila hatulalamiki? Unaichukiaje timu ambayo inasaidia timu nyingine 4 kushiriki michuano ya kimataifa? Muwe mnafikiri mara mbili mbili basi! Nyie vitimu vidogo visivyo na akili badilikeni.
Comment ya mwanaume wa dar mayai mayai
 
Kule fc lupopo sijui kwanini anakaa bench kila siku
 
Unaichukiaje timu ambayo inasaidia timu nyingine 4 kushiriki michuano ya kimataifa?

Kwa sentensi hii yenye mfumo wa swali, bila shaka timu zinakuwa 6.
Simba
Bingwa wa FA
Na timu nyingine 4 zinazosaidiwa na Simba kushiriki kutoka na Simba kufanya vizuri kimataifa.
 
Back
Top Bottom