Mfungo unavyoadhiri WALAFI

Mfungo unavyoadhiri WALAFI

fiksiman

JF-Expert Member
Joined
May 17, 2008
Posts
402
Reaction score
107
Jamani mwezi ndo unaelekea ukingoni, nataka kuwatonya kituko nilichokutana nacho hivi karibuni....mkanda ulikuwa hivi:

Tulikwenda kwenye kazi na wenzangu kama wanne hivi, ilikuwa maeneo ya masaki kwa mzito mmoja...(timu ya waandishi). Basi tukachapa kazi hadi majira ya jioni sana...karibia na muda wa futari. Sasa mama mwenye nyumba akauliza kama wapo waliofunga. Wote tukaonyesha vidole.

Basi adhana ilipopigwa tukasogea kwenye mkeka na vinono vikawasili. Sasa aibu ilikuja pale tulipoanza kupiga tukio. Heee, hamadi si wadau wawili wakasali rosali (wakaonyesha alama ya msalaba kwenye paji la uso kisha wakatulia kwa muda kama wanasali). Wote tushikwa na aibu maana walikuwa watu wazima.

Jamani mwezi huu!
 
Kwa mujibu wako mwenyewe swali lilikuwa "kuna waliofunga", halikuwa "kuna waislam".

Kufunga Ramadhan is nothing more than changing the hours, kutoka kula mchana kwenda kula usiku, kwa hiyo kama mtu unaweza kujilia usiku kucha na kulala mchana what is the difference?
 
Jamani mwezi ndo unaelekea ukingoni, nataka kuwatonya kituko nilichokutana nacho hivi karibuni....mkanda ulikuwa hivi:

Tulikwenda kwenye kazi na wenzangu kama wanne hivi, ilikuwa maeneo ya masaki kwa mzito mmoja...(timu ya waandishi). Basi tukachapa kazi hadi majira ya jioni sana...karibia na muda wa futari. Sasa mama mwenye nyumba akauliza kama wapo waliofunga. Wote tukaonyesha vidole.

Basi adhana ilipopigwa tukasogea kwenye mkeka na vinono vikawasili. Sasa aibu ilikuja pale tulipoanza kupiga tukio. Heee, hamadi si wadau wawili wakasali rosali (wakaonyesha alama ya msalaba kwenye paji la uso kisha wakatulia kwa muda kama wanasali). Wote tushikwa na aibu maana walikuwa watu wazima.

Jamani mwezi huu!

Ingekuwa kitaa unawachomoa tuu kundini,mnawalamba mikono kama walikuwa wameshaichonvya kunako futari kisha wanakuwa watazamaji.
 
Ingekuwa kitaa unawachomoa tuu kundini,mnawalamba mikono kama walikuwa wameshaichonvya kunako futari kisha wanakuwa watazamaji.

This is what I call a food fight, is this what Islam represent?
 
This is what I call a food fight, is this what Islam represent?

u got it wrong, hapa hatuzungumzii uislam ila tabia za watu kupenda vya dezo. Kama shida ilikuwa ni kula si wangesema hawajafunga ila wangependa kujumuika kwenye futari pengine mwenyeji angeweka mkakati mwingine kwa ajili yao.

Huo unataka kuleta kwenye thread yangu ni udini tafadhali tuache uchochezi. Afteral it is just a joke!
 
This is what I call a food fight, is this what Islam represent?

Kwa mujibu wako mwenyewe swali lilikuwa "kuna waliofunga", halikuwa "kuna waislam".

Kufunga Ramadhan is nothing more than changing the hours, kutoka kula mchana kwenda kula usiku, kwa hiyo kama mtu unaweza kujilia usiku kucha na kulala mchana what is the difference?

Mkuu inaonekana Hujaelewa maana kufunga...hebu tuambie wapi walisema kufunga ni kubadili muda wa kula? AU ndo mnavyofanya kwenye dini yenu (nahisi wewe si muislam) maana huku kwetu hatuna maana hiyo na nina hakika hata kwa wengine pia hawana maana hivyo.
 
Mkuu inaonekana Hujaelewa maana kufunga...hebu tuambie wapi walisema kufunga ni kubadili muda wa kula? AU ndo mnavyofanya kwenye dini yenu (nahisi wewe si muislam) maana huku kwetu hatuna maana hiyo na nina hakika hata kwa wengine pia hawana maana hivyo.

Mkuu kosa unalofanya ni kubishana na huyu muheshimiwa,nafikiri angeenda katika jukwaa lao la dini.Mwache aendelee kumwaga pumba zake tuu,tusije tukaonekana wote hamnazo.
 
u got it wrong, hapa hatuzungumzii uislam ila tabia za watu kupenda vya dezo. Kama shida ilikuwa ni kula si wangesema hawajafunga ila wangependa kujumuika kwenye futari pengine mwenyeji angeweka mkakati mwingine kwa ajili yao.

Huo unataka kuleta kwenye thread yangu ni udini tafadhali tuache uchochezi. Afteral it is just a joke!

Unajuaje kama hawajafunga? Katika maandishi yako hujaonyesha popote ambapo panaonyesha hawajafunga.

Kama kuna mtu anayeleta udini ni wewe unaetaka kuwabagua wakristo kwa sababu ya dini yao wakati hujui kama wamefunga ama la.

u got it wrong, hapa hatuzungumzii uislam

Kama hatuzungumzii uislam kwa nini unawatenga wakristo kwa mujibu ya dini yao? Kama issue ni kufunga unajuaje kwamba hawajafunga?

ila tabia za watu kupenda vya dezo

Kama issue ni kupenda vya dezo, hata hao waliofunga si wanapata vya dezo hapo? Sasa kama wote wamefunga na wewe si mbaguzi wa kidini, kwa nini unaona hawa wakristo tu ndio wanaopenda dezo?

Kama shida ilikuwa ni kula si wangesema hawajafunga ila wangependa kujumuika kwenye futari pengine mwenyeji angeweka mkakati mwingine kwa ajili yao.

Unajuaje kama hawajafunga, mbona hkuonyesha kwamba hawajafunga katika original post?
 
Mkuu inaonekana Hujaelewa maana kufunga...hebu tuambie wapi walisema kufunga ni kubadili muda wa kula? AU ndo mnavyofanya kwenye dini yenu (nahisi wewe si muislam) maana huku kwetu hatuna maana hiyo na nina hakika hata kwa wengine pia hawana maana hivyo.

As far as eating is concerned mnakula usiku kucha (night) na kuacha kula mchana kutwa (day), so how is that different from just switching day and night,as far as eating is concerned?
 
Umeshinda ndugu yangu maana hOja zako ni KUU...sikujua kama kuna dini nyingi nayo ipo kwenye mfungo kama waislam. Kwahiyo kaka na unahisi hao nao walikuwa wamefunga sio? Sikujua kama wakiristo hufunga sunnah au kwaresma tayari...tehetehetehete bluray acha mambo yako ya kudebate kila jambo... huchelewi kugeuza hapa kijiwe cha siasa. Hapa bwana tumekuja kucheka na kuburudika unakotupeleka SIKO MDAU LOO!
 
as far as eating is concerned mnakula usiku kucha (night) na kuacha kula mchana kutwa (day), so how is that different from just switching day and night,as far as eating is concerned?

we kiboko duuh!
 
Umeshinda ndugu yangu maana hOja zako ni KUU...sikujua kama kuna dini nyingi nayo ipo kwenye mfungo kama waislam. Kwahiyo kaka na unahisi hao nao walikuwa wamefunga sio? Sikujua kama wakiristo hufunga sunnah au kwaresma tayari...tehetehetehete bluray acha mambo yako ya kudebate kila jambo... huchelewi kugeuza hapa kijiwe cha siasa. Hapa bwana tumekuja kucheka na kuburudika unakotupeleka SIKO MDAU LOO!

Nahisi jamaa hakuelewa kilichokuwa kinazungumziwa au kama ameelewa basi ameelewa sivyo!!
 
Back
Top Bottom