Mfungo wa ramadhani mjini Berlin Ujerumani

Mfungo wa ramadhani mjini Berlin Ujerumani

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MFUNGO WA RAMADHANI MJINI BERLIN UJERUMANI

Sijapatapo kuishi mji mgumu duniani kama Berlin na naamini hii ni sawa katika miji yote ya Ujerumani.

Kwanza ni Wajerumani wenyewe na sura zao za chuma.

Hawana tabasamu wakati wote sura zao ni za jiwe yaani, ''stone face.''

Pili Wajerumani hawaelewi kwa nini wewe hujui Kijerumani na kuhakikisha kuwa unatia juhudi ya kukijua Kijerumani hakuna tafsiri ya tangazo lolote mahali popote.

Huna njia ya mkato ila kujifunza Kijerumani.

Mwezi Mtukufu wa Ramadhani umenikuta Berlin.

Siku chache kabla ya mfungo nikawa nauliza msikiti wa jirani na ratiba ya sala khasa sala ya Maghrib kwa ajili ya kufungua ''muadhin.''

Sehemu niliyokuwa naishi kulikuwa na Waturuki wengi na maduka niliyokuwa nanunua mahitaji yangu yalikuwa ya Waturuki hata migahawa niliyokuwa napita kununua, ''take away,'' zangu ilikuwa migahawa ya halal.

Lugha ikawa kikwazo changu kikubwa sana kuelewana na Mturuki mwenye duka kubwa jirani yangu lakini alinielekwa kuwa nilikuwa namuuliza msikiti.

Akanielekeza mtaa wa pili tu hapo jirani kuwa upo msikiti.

Nimepita mchana wa Ramadhani kuangalia kama nitakuta sala ya jamaa.

Hakika ulikuwa msikiti na mchana wa Ramadhani lakini sikuona dalili ya watu kuingia kusali.

Nilinyongonyea kupita kiasi.

Nimeishi Ulaya na najua hali ya Mwezi wa Ramadhani mathalan London msikiti wa White Chapel, East London au Msikiti wa Finsbury Park achilia mbali msikiti wa Regents Park.

Hii misikiti yenyewe itakupa hali ya kuwa Mwezi Mtukufu umefika.

Berlin ilikuwa tofauti sana.

Nilitamani niruke nijikute nimefika Dar es Salaam Msikiti wa Mtoro nimeswali na nasubiri kusikiliza darsa za Ramadhani.

Nilirudi nyumbani nimelowa sana.
Nilijiuliza kitu gani kimenileta huku porini.

Rafiki yangu katika Take Away yangu aliponiona akajua nimefata futari akawa ananionesha, ''barbecue,'' za kunitia hamu lakini vyote vilivyokuwapo pale vilinitumbukia nyongo achilia mbali ile kunitolea chupa ya juisi kwenye jokofu lile lile ambalo ndani yake alikuwa amaweka bia za Kijerumani.

Kanitolea kila aiana ya salad nikawa nachagua kama mtu niliyepigwa na radi nachukua tu lakini moyo wangu haukuwapo katika ile futari.

Nimeadhini mwenyewe chumbani kwangu nimefungua muadhini kisha nimeswali.

Sijapatapo katika maisha yangu kushuhudia Ramadhani ya unyonge kama hii.

Hii kwa unyonge ilishinda Ramadhani yangu ya kwanza Uingereza, Cardiff miaka mingi iliyopita nikiwa bado kijana sana.

Hiyo picha hapo chini ni kituo changu cha treni nashuka hapo asubuhi kisha natembea kama robo saa hadi ofisini kwangu Zentrum Moderner Orient (ZMO) taasisi ya utafiti mfano wa University of London School of Oriental and African Studies (SOAS).

ZMO wakati wa WW II jumba hili ilipokuwa ofisi yangu lilikuwa makao ya GESTAPO.

Kusafiri ni elimu tosha.

1093687
 
Mkuu kwahiyo waislam huko hawapo au watu hawafungi tu?.
 
Watu hawana habari na mambo ya dini kabisa..
 
Mimi si Mwislamu lakini ninavyojua Berlin kuna msikiti tele. Ukifika kama mgeni nchi usipojua lugha heri ujiandae; kama unataka kitu uandae maswali yako. SIku hizi Inteneti unaweza kupata habari nyingi , kwa mfano orodha hii ya msikiti Berlin

Gebetszeiten Heute Fadschr Sonnenaufgang Dhuhur Assr Maghreb Ishaa
05.05.2019 03:33 05:24 13:05 17:11 20:42 22:22

Abdulkadir Geylani Camii Stuttgarter Straße 50 Neukölln
Africa Moschee CHIEF IMAM Scheich Hussein Kurfürstenstraße 88 Mitte
Al Imam Badstraße 21 Wedding
Arresalah Moschee Brunnenstraße 70 Wedding
Ayasofya Camii Stromstraße 35 Tiergarten
Aziziye Camii Möwenweg 36 Buckow
Dagestan Mosque Schönwalder Straße 11 Wedding
Darul Arqam Großbeerenstraße 91 Kreuzberg
Dzemat IKRE Berlin e.V. Meteorstraße 30 Reinickendorf
Ertuğrul Gazi Camii Oranienstraße 189
Fatih Camii Falckensteinstraße 12 Kreuzberg
Haus der Weisheit (Darul Hikma) Rathenower Straße 16 Tiergarten
Hicret Camii Perleberger Straße 14 Moabit
Hoca Ahmet Yesevi Camii Neuendorfer Straße 101 Spandau
Ibrahim Alkhalil Moschee Colditzstraße 27 -29 Tempelhof-Schöneberg
Ikra Bashkimi Reinickendorfer Straße 50A Wedding
Kocasinan Camii Pankower Allee 45 Berlin
Markaz Imam Nafi Ollenhauerstraße 15 -16
Merkez Furkan Glasower Straße 41 Neukölln
Mescid ve Kuran Kursu Stettiner Straße 28 Wedding
Pakistanische Moschee Residenzstraße 9 Bezirk Reinickendorf
Tekke-i Kadiriyye Mescidi Hermannstraße 120 Bezirk Neukölln
Tekke Mehmed Zahid Kotku Turiner Straße 6 Wedding
Türkische Moschee Müllerstraße 119 Wedding
مسجد الزيتونة Seituna Moschee Sophie-Charlotten-Straße 31 Charlottenburg
Afrikanishe Mosche Leykestraße 4
Aksemsettin Camii Bellermannstr. 90 Wedding
Anadolu Camii Katzlerstraße 15 Schöneberg
Ashabi Kehf Camii Jasmunder Str. 3 Berlin-Wedding railway station
Baitul Mukarram Masjid e.V. Fontanestraße 17 Neukölln
Beyazid Camii Lindower Str. 18 Wedding
Bilal Moschee Drontheimer Str. 16 Wedding
Bosnisches Islamisches Kulturzentrum Adalbertstr. 94 Kreuzberg
Büyük Camii Seeburger Str. 90 Spandau
Dar Assalam Moschee Flughafenstraße 43 Berlin
Ensar Moschee Spandauer Damm 44 Charlottenburg
Eyüp Sultan Camii Lindower Straße 24 Wedding
Gazi Osman Pasa Camii Schöneweider Straße 11 Neukölln
Haci Bayram Moschee Koloniestraße 127 Wedding
Hamidiye Camii Sonnenallee 18 Neukölln
Interkulturelles Zentrum für Dialog und Bildung e.V. Drontheimer Str. 32a Berlin-Wedding
Islamische Gemeinde Emir Sultan Kulturhaus e.V. Hauptstraße 150 Schöneberg
Islamische Gemeinschaft deutschsprachiger Muslime Geßlerstr. 11 Schöneberg
Islamisches Kultur- und Erziehungszentrum Finowstr. 27 Neukölln
Kocatepe Camii Grammestraße 17 Siemensstadt
Lübars Camii Quickborner Straße 96 Lübars
Mabet Camii Alt-Moabit 112 Tiergarten
Mariendorfer Moschee Mariendorfer Damm 46 Mariendorf
Masjid Al-Falah Feldzeugmeisterstraße 1 Tiergarten
Masjid Al- Ummah Buttmannstraße 17
Merkez Camii Wiener Str. 12 Kreuzberg
Mescidi Aksa Soldiner Straße 72-74 Wedding
Mescidi Nur Camii Eisenbahnstr. 16 Kreuzberg
Mevlana Camii Skalitzer Straße 131-132 Kreuzberg
Mimar Sinan Cami Hermannstraße 120 Neukölln
Minhaj-ul-Quran International Berlin Müllerstraße 47A Wedding
Moschee As-Salaam Goslarer Platz 5 Charlottenburg
Muradiye Camii Kottbusser Damm 75 Kreuzberg
Neukölln Camii Hermannstraße 177 Neukölln
Orhan Gazi Camii Obentrautstraße 35 Kreuzberg
Osman Gazi Camii Nehringstraße 27 Charlottenburg
Sehitlik Camii Columbiadamm 128
Semerkant Moschee Kurfürstenstraße 37
Spandau Yeni Camii Lynarstraße 17 Spandau
Sultan Abdulhamid Han Moschee Amsterdamer Str. 17a Wedding
Sultan Ahmed Camii Lehrter Straße 39 Tiergarten
Tegel Selimiye Camii Trettachzeile 7 Wittenau
Vakif Moschee Boppstr. 4 Kreuzberg
Valide-i-Sultan Camii Hedwigstraße 15 Friedenau
Xhamia Isa Beuy Karl-Marx-Straße 58
Yeni Camii Richardstraße 112 Neukölln
Yunus Emre Camii Reinickendorfer Str. 38-39 Wedding
 
Pole, mkuu karibu ila ndo hivyo lazima ujifunze kidogo hata , bitte, könnten Sie mir helfen, kaeuro kana tabu, hawa jamaa n lugha zao , sijui utafanyaje mkuu na lugha yenye ya der, die, das na makonjugation yake kadiri ya verbs na preposition. Kazi kweli mkuu aber yote kwa yote wir dürfen Sie ganz herzlich willkommen heißen. Misikiti iko ya kutosha google then chukua tax siku ya kwanza nenda.
MFUNGO WA RAMADHANI MJINI BERLIN UJERUMANI

Sijapatapo kuishi mji mgumu duniani kama Berlin na naamini hii ni sawa katika miji yote ya Ujerumani.

Kwanza ni Wajerumani wenyewe na sura zao za chuma.

Hawana tabasamu wakati wote sura zao ni za jiwe yaani, ''stone face.''

Pili Wajerumani hawaelewi kwa nini wewe hujui Kijerumani na kuhakikisha kuwa unatia juhudi ya kukijua Kijerumani hakuna tafsiri ya tangazo lolote mahali popote.

Huna njia ya mkato ila kujifunza Kijerumani.

Mwezi Mtukufu wa Ramadhani umenikuta Berlin.

Siku chache kabla ya mfungo nikawa nauliza msikiti wa jirani na ratiba ya sala khasa sala ya Maghrib kwa ajili ya kufungua ''muadhin.''

Sehemu niliyokuwa naishi kulikuwa na Waturuki wengi na maduka niliyokuwa nanunua mahitaji yangu yalikuwa ya Waturuki hata migahawa niliyokuwa napita kununua, ''take away,'' zangu ilikuwa migahawa ya halal.

Lugha ikawa kikwazo changu kikubwa sana kuelewana na Mturuki mwenye duka kubwa jirani yangu lakini alinielekwa kuwa nilikuwa namuuliza msikiti.

Akanielekeza mtaa wa pili tu hapo jirani kuwa upo msikiti.

Nimepita mchana wa Ramadhani kuangalia kama nitakuta sala ya jamaa.

Hakika ulikuwa msikiti na mchana wa Ramadhani lakini sikuona dalili ya watu kuingia kusali.

Nilinyongonyea kupita kiasi.

Nimeishi Ulaya na najua hali ya Mwezi wa Ramadhani mathalan London msikiti wa White Chapel, East London au Msikiti wa Finsbury Park achilia mbali msikiti wa Regents Park.

Hii misikiti yenyewe itakupa hali ya kuwa Mwezi Mtukufu umefika.

Berlin ilikuwa tofauti sana.

Nilitamani niruke nijikute nimefika Dar es Salaam Msikiti wa Mtoro nimeswali na nasubiri kusikiliza darsa za Ramadhani.

Nilirudi nyumbani nimelowa sana.
Nilijiuliza kitu gani kimenileta huku porini.

Rafiki yangu katika Take Away yangu aliponiona akajua nimefata futari akawa ananionesha, ''barbecue,'' za kunitia hamu lakini vyote vilivyokuwapo pale vilinitumbukia nyongo achilia mbali ile kunitolea chupa ya juisi kwenye jokofu lile lile ambalo ndani yake alikuwa amaweka bia za Kijerumani.

Kanitolea kila aiana ya salad nikawa nachagua kama mtu niliyepigwa na radi nachukua tu lakini moyo wangu haukuwapo katika ile futari.

Nimeadhini mwenyewe chumbani kwangu nimefungua muadhini kisha nimeswali.

Sijapatapo katika maisha yangu kushuhudia Ramadhani ya unyonge kama hii.

Hii kwa unyonge ilishinda Ramadhani yangu ya kwanza Uingereza, Cardiff miaka mingi iliyopita nikiwa bado kijana sana.

Hiyo picha hapo chini ni kituo changu cha treni nashuka hapo asubuhi kisha natembea kama robo saa hadi ofisini kwangu Zentrum Moderner Orient (ZMO) taasisi ya utafiti mfano wa University of London School of Oriental and African Studies (SOAS).

ZMO wakati wa WW II jumba hili ilipokuwa ofisi yangu lilikuwa makao ya GESTAPO.

Kusafiri ni elimu tosha.

View attachment 1093687
 
Mkuu pole sana na Allah akufanyie wepesi
Waislam wengi tu hapo na misikiti ipo usife moyo tafuta tu
 
Pole, mkuu karibu ila ndo hivyo lazima ujifunze kidogo hata , bitte, könnten Sie mir helfen, kaeuro kana tabu, hawa jamaa n lugha zao , sijui utafanyaje mkuu na lugha yenye ya der, die, das na makonjugation yake kadiri ya verbs na preposition. Kazi kweli mkuu aber yote kwa yote wir dürfen Sie ganz herzlich willkommen heißen. Misikiti iko ya kutosha google then chukua tax siku ya kwanza nenda.
Unprejudiced,
Haya si ya leo ni miaka mingi iliyopita.
 
MFUNGO WA RAMADHANI MJINI BERLIN UJERUMANI ....
...
Rafiki yangu katika Take Away yangu aliponiona akajua nimefata futari akawa ananionesha, ''barbecue,'' za kunitia hamu lakini vyote vilivyokuwapo pale vilinitumbukia nyongo achilia mbali ile kunitolea chupa ya juisi kwenye jokofu lile lile ambalo ndani yake alikuwa amaweka bia za Kijerumani....
Mzee samahani lkn swali moja:
inaonekana umeshtushwa ulipoona huyu Bwana Mturuki alichukua juisi yako "kwenye jokofu lile lile ambalo ndani yake alikuwa amaweka bia za Kijerumani.."

Naelewa labda ulishangaa maana huyu Mturuki uliyemchukua ni Mwaislamu anatunza pia bia katika duka lake. Ninavyojua Waturuki wengi hunywa bia , wanaitengeneza pia (aina ya Efes ni mashuhuri...)

Ila tu napenda kujua: je kuna kanuni ya Kiislamu kinachofanya chakula kuwa najisi kikikaa karibu na chakula haramu? Hata bila kugusana kwa vyakula vyenyewe?

Maana juisi iko ndani ya chupa cha kioo, bia iko ndano ya chupa cha kioo ,hakuna mwingiliano baina ya juisi na bia.

Najua Wayahudi wanaona matatizo hapa katika kanuni zao za kosher / kashrut. Maana wanapotakiwa kutochanganya nyama na maziwa wana seti mbili za sufuria na sahani kwa kila aina ya chakula, pia huwa na jokofu mbili, moja kwa nyama na soseji, nyingine kwa maziwa na jibini ya yoghurt ili kutunza kashrut.
Je, Waislamu wanaona yale kama Wayahudi kama vitu viwili vya kinyunme viko karibu vimeingiliana tayari?
 
Back
Top Bottom