Mgao wa umeme waisha

Mgao wa umeme waisha

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
Date::9/29/2008
Tanesco watangaza mgawo wa umeme kwaheri
Jackson Odoyo na Aika Mushi
Mwananchi

MGAWO wa umeme uliokuwa ukiendelea nchi nzima sasa umekwisha baada ya mafundi kutoka Marekani kuwasili na kutengeneza mtambo mmoja wenye uwezo wa kuzalisha megawati 40.

Awali Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ilitangaza kuwepo kwa mgao wa umeme nchini nzima baada ya mitambo mitatu ya Kampuni ya Songas inayozalisha umeme wa gesi asilia ya megawati 182 kuharibika.

Akizungumza na Waandishi wa habari jana ofisini kwake Meneja Uhusiano wa Tanesco, Badra Masudi alisema mgao huo umesitishwa rasmi kuanzia sasa baada ya mafundi hao kufanikiwa kutengeneza mtambo mmoja.

"Kuanzia leo hakutakuwa na mgao wa umeme kwa sababu wataalamu kutoka Marekani waliwasili juzi na kuanza kazi ya kutengeneza mitambo iliyokuwa imeharibika,"alisema Masudi.

Alisema megawati hizo 40 zilizoomgezeka pamoja zile 72 zilizokuwa zinazalishwa awali na kampuni hiyo zitaweza kusaidia na kwamba mbali na megawatt hizo pia wanategemea mitambo yao mingine inayotumia nguvu ya maji na mafuta.

Badra aliongeza kusema kwamba kutokana na hatua hizo Tanesco ina uhakika suala la mgao wa umeme halitakuwepo tena na kwamba kama kutakuwa na tatizo lolote watatoa taarifa mapema iwezekanavyo.

Kuhusu suala la Kampuni ya Songas kuharibikiwa mitambo yao wakati wameingia mkataba na Tanesco alisema kwa mujibu wa mkataba wao katika kipindi hiki ambacho Kampuni hiyo ilishindwa kuzalisha umeme katika kiwango kinachotakiwa hawatawalipa.

Alisema mkataba huo unawaelekeza wawalipe mara baada ya wao kuzalisha umeme tena kwa kiwango walicho kubaliana tu na kwamba kwa mantiki hiyo katika kipindi chote walichoshindwa kuzalisha kutokana na mitambo yao kuwa mibovu hawatalipwa.
 
Date::9/29/2008
Tanesco watangaza mgawo wa umeme kwaheri
Jackson Odoyo na Aika Mushi
Mwananchi

MGAWO wa umeme uliokuwa ukiendelea nchi nzima sasa umekwisha baada ya mafundi kutoka Marekani kuwasili na kutengeneza mtambo mmoja wenye uwezo wa kuzalisha megawati 40.

Awali Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ilitangaza kuwepo kwa mgao wa umeme nchini nzima baada ya mitambo mitatu ya Kampuni ya Songas inayozalisha umeme wa gesi asilia ya megawati 182 kuharibika.

Akizungumza na Waandishi wa habari jana ofisini kwake Meneja Uhusiano wa Tanesco, Badra Masudi alisema mgao huo umesitishwa rasmi kuanzia sasa baada ya mafundi hao kufanikiwa kutengeneza mtambo mmoja.

“Kuanzia leo hakutakuwa na mgao wa umeme kwa sababu wataalamu kutoka Marekani waliwasili juzi na kuanza kazi ya kutengeneza mitambo iliyokuwa imeharibika,”alisema Masudi.

Alisema megawati hizo 40 zilizoomgezeka pamoja zile 72 zilizokuwa zinazalishwa awali na kampuni hiyo zitaweza kusaidia na kwamba mbali na megawatt hizo pia wanategemea mitambo yao mingine inayotumia nguvu ya maji na mafuta.

Badra aliongeza kusema kwamba kutokana na hatua hizo Tanesco ina uhakika suala la mgao wa umeme halitakuwepo tena na kwamba kama kutakuwa na tatizo lolote watatoa taarifa mapema iwezekanavyo.

Kuhusu suala la Kampuni ya Songas kuharibikiwa mitambo yao wakati wameingia mkataba na Tanesco alisema kwa mujibu wa mkataba wao katika kipindi hiki ambacho Kampuni hiyo ilishindwa kuzalisha umeme katika kiwango kinachotakiwa hawatawalipa.
Alisema mkataba huo unawaelekeza wawalipe mara baada ya wao kuzalisha umeme tena kwa kiwango walicho kubaliana tu na kwamba kwa mantiki hiyo katika kipindi chote walichoshindwa kuzalisha kutokana na mitambo yao kuwa mibovu hawatalipwa.

Huu unaonyesha ni moja ya mikataba iliyosainiwa kwa hila na yenye harufu ya rushwa. Ikiwa Tanesco hawatawalipa Songas kwa kutopatiwa umeme its common sense kuwa Tanesco wamepata hasara na Songas wanatakiwa wawalipe Tanesco kwa damages walizopata. Hiyo condition ingewawezesha hao Songas wawe makini na kuwa na back up nzuri ili inapotokea matatizo Tanzania isiwe gizani. Kwani ukweli wa mambo sio Tanesco tu ndio watakosa kuuza umeme na wauza bidhaa (perishable goods) wanaingia hasara ya mamilioni. Sijui hili mnalionaje au labda mimi I am from mars! maana watu wanachukulia poa tu kwa kila kitu
 
Huu unaonyesha ni moja ya mikataba iliyosainiwa kwa hila na yenye harufu ya rushwa. Ikiwa Tanesco hawatawalipa Songas kwa kutopatiwa umeme its common sense kuwa Tanesco wamepata hasara na Songas wanatakiwa wawalipe Tanesco kwa damages walizopata. Hiyo condition ingewawezesha hao Songas wawe makini na kuwa na back up nzuri ili inapotokea matatizo Tanzania isiwe gizani. Kwani ukweli wa mambo sio Tanesco tu ndio watakosa kuuza umeme na wauza bidhaa (perishable goods) wanaingia hasara ya mamilioni. Sijui hili mnalionaje au labda mimi I am from mars! maana watu wanachukulia poa tu kwa kila kitu

Umeongea point, juzi juzi nilisoma habari kwenye gazeti (thisday ---soma hapa) moja baada ya mgawo kuanza kuwa Tanesco wanaandaa master plan kwa ajili ya umeme wa nchi nzima na wanapendekeza kuwe na buffer ya 15% kwa sababu nchi nyingine ndio wanafanya hivyo. Nikawa najiuliza ina maana miaka yote ili lilikuwa halijulikani? Halafu bado tunashangaa kwanini investors wanakwenda Kenya na sio Tanzania....we are not serious on everything we do.
 
Back
Top Bottom