Matojo Cosatta
JF-Expert Member
- Jul 28, 2017
- 234
- 390
MGAWANYO WA WABUNGE WANAWAKE WA VITI MAALUM KATIKA JICHO LA SHERIA.
Kabla ya Chama cha Siasa kupewa mgao wake wa wabunge wanawake wa Viti Maalum lazima kitimize masharti yafuatayo;
(1) Lazima chama cha siasa kiwe kimeshiriki katika uchaguzi mkuu.
(2) Lazima chama cha siasa kiwe kimepata walau asilimia 5 % ya jumla ya kura halali zote katika uchaguzi wa wabunge wa majimbo.
(3) Chama cha Siasa lazima kipendekeze kwa Tume ya Uchaguzi majina ya wanawake ambao wanagombea ubunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya chama hicho kwa mpangilio wa upendeleo (order of preference).
(3) Wanawake wanaopendekezwa na Chama cha Siasa husika lazima wajaze Fomu za Uteuzi (Fomu Na. 8) na kuziwasilisha katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi pamoja na viambatanusho vyake.
(4) Chama cha siasa lazima kiwasilishe mapendekezo ya majina ya wanawake ambao wanagombea ubunge wa Viti Maalum kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika muda wa siku 30 kabla ya Uchaguzi.
(5) Chama cha siasa kitapa idadi ya wabunge wa Viti Maalum kwa kuzingatia uwiano wa jumla ya kura ambazo kimepata katika uchaguzi wa wabunge. Kwa mfano, kama Idadi ya wabunge ni 100 na NCCR-Mageuzi ikapata asilimia 7% ya kura za uchaguzi wa wabunge basi NCCR-Mageuzi itapata mgao wa wabunge 7 ambao ni sawa na asilimia 7% ya kura za uchaguzi wa wabunge.
N.B: Idadi ya wabunge wanawake wa Viti Maalum ni asilimia 40% ya wabunge wote ambao sio Viti Maalum.
🔹 N.B: Mbunge aliyepita bila kupingwa
Kwa mujibu wa Ibara ya 78 (2) (a) na (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, iwapo mbunge amepita bila kupingwa basi kura zifuatazo zitahesabiwa ni kura halali za mbunge ambaye amepita bila kupingwa;
(a) Kura za mgombea Urais lakini iwapo chama cha siasa cha mgombea ubunge ambaye amepita bila kupingwa katika Jimbo la Uchaguzi kimesimamisha mgombea Urais katika Uchaguzi wa Rais.
(b) Asilimia 51% ya watu wote ambao walijiandikisha kama wapiga kura katika jimbo la uchaguzi husika lakini iwapo tu chama cha siasa cha mgombea ubunge ambaye amepita bila kupingwa katika Jimbo la Uchaguzi hakikusimamisha mgombea Urais katika Uchaguzi wa Rais.
⛔ Msingi wa Kikatiba na Kisheria wa maelezo haya ni masharti ya sheria yafuatayo;
(1) Ibara ya 78 na 81 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977
(2) Kifungu cha 86 A cha Sheria ya Uchaguzi wa Taifa, Sura ya 343.
(3) Kanuni ya 70 ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge, 2020 (G.N. No. 402 of 2020)
(4) Aya ya 10 ya Maelekezo ya Uchaguzi kwa Vyama vya Siasa na Wagombea, 2020
Imeandikwa na Matojo M. Cosatta, Senior JF Member.
Kabla ya Chama cha Siasa kupewa mgao wake wa wabunge wanawake wa Viti Maalum lazima kitimize masharti yafuatayo;
(1) Lazima chama cha siasa kiwe kimeshiriki katika uchaguzi mkuu.
(2) Lazima chama cha siasa kiwe kimepata walau asilimia 5 % ya jumla ya kura halali zote katika uchaguzi wa wabunge wa majimbo.
(3) Chama cha Siasa lazima kipendekeze kwa Tume ya Uchaguzi majina ya wanawake ambao wanagombea ubunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya chama hicho kwa mpangilio wa upendeleo (order of preference).
(3) Wanawake wanaopendekezwa na Chama cha Siasa husika lazima wajaze Fomu za Uteuzi (Fomu Na. 8) na kuziwasilisha katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi pamoja na viambatanusho vyake.
(4) Chama cha siasa lazima kiwasilishe mapendekezo ya majina ya wanawake ambao wanagombea ubunge wa Viti Maalum kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika muda wa siku 30 kabla ya Uchaguzi.
(5) Chama cha siasa kitapa idadi ya wabunge wa Viti Maalum kwa kuzingatia uwiano wa jumla ya kura ambazo kimepata katika uchaguzi wa wabunge. Kwa mfano, kama Idadi ya wabunge ni 100 na NCCR-Mageuzi ikapata asilimia 7% ya kura za uchaguzi wa wabunge basi NCCR-Mageuzi itapata mgao wa wabunge 7 ambao ni sawa na asilimia 7% ya kura za uchaguzi wa wabunge.
N.B: Idadi ya wabunge wanawake wa Viti Maalum ni asilimia 40% ya wabunge wote ambao sio Viti Maalum.
🔹 N.B: Mbunge aliyepita bila kupingwa
Kwa mujibu wa Ibara ya 78 (2) (a) na (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, iwapo mbunge amepita bila kupingwa basi kura zifuatazo zitahesabiwa ni kura halali za mbunge ambaye amepita bila kupingwa;
(a) Kura za mgombea Urais lakini iwapo chama cha siasa cha mgombea ubunge ambaye amepita bila kupingwa katika Jimbo la Uchaguzi kimesimamisha mgombea Urais katika Uchaguzi wa Rais.
(b) Asilimia 51% ya watu wote ambao walijiandikisha kama wapiga kura katika jimbo la uchaguzi husika lakini iwapo tu chama cha siasa cha mgombea ubunge ambaye amepita bila kupingwa katika Jimbo la Uchaguzi hakikusimamisha mgombea Urais katika Uchaguzi wa Rais.
⛔ Msingi wa Kikatiba na Kisheria wa maelezo haya ni masharti ya sheria yafuatayo;
(1) Ibara ya 78 na 81 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977
(2) Kifungu cha 86 A cha Sheria ya Uchaguzi wa Taifa, Sura ya 343.
(3) Kanuni ya 70 ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge, 2020 (G.N. No. 402 of 2020)
(4) Aya ya 10 ya Maelekezo ya Uchaguzi kwa Vyama vya Siasa na Wagombea, 2020
Imeandikwa na Matojo M. Cosatta, Senior JF Member.