SULEIMAN ABEID
JF-Expert Member
- Feb 26, 2013
- 390
- 385
SIKU moja mara baada ya aliyekua Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai kutangaza rasmi kujiuzulu wadhifa wake wa Uspika, baadhi ya wakazi wa Shinyanga wametoa maoni yao kuhusiana na maamuzi yake hayo.
Mmoja wa wakazi hao, ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Mzalendo Foundation ya Mjini Kahama Mkoani Shinyanga, Khamis Mgeja ameishauri Serikali kuangalia uwezekano wa kuondoa jina la Ndugai katika maeneo yote ya majengo ya Umma.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Shinyanga, Mgeja amesema kitendo kilichotendwa na Ndugai cha kuikosoa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Samia Suluhu Hassan ni sawa na kuinajisi nchi hivyo kuendelea kuonekana kwa jina lake katika majengo ya umma ni kuwatia kichefuchefu watanzania.
Mgeja amewapongeza watanzania kwa jinsi walivyoonesha mshikamano wa "nguvu ya Umma" mara baada ya Ndugai kutoa kauli yake ya kuikosoa Serikali kuhusiana na suala zima la mikopo kwa ajili ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa hapa nchini ambapo alidai nchi inaweza kupigwa mnada kwa kuzidiwa na mikopo.
Amesema kitendo cha wananchi kuonesha mshikamano katika kupinga kwa nguvu zote kauli hiyo ya Ndugai kimeweza kumng'oa katika nafasi yake na kwamba siku zote nguvu ya umma ina nguvu kuliko kitu chochote katika nchi yoyote duniani na inaweza kumng'oa ye yote bila kujali "Ubabe" alionao.
Pamoja na kuishauri Serikali iangalie uwezekano wa kuondoa jina la Ndugai kwenye majengo yote ya Umma pia Mgeja ambaye ni Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga amewashauri wale wote waliokuwa nyuma ya Ndugai wajitathimini na ikibidi wachukue maamuzi kama aliyochukua "Boss" wao.
“Binafsi nimefurahishwa na kitendo cha Mheshimiwa Ndugai kutangaza kujiuzulu wadhifa wake wa Uspika wa Bunge letu tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kweli kitendo chake cha kudai nchi yetu inaweza kupigwa mnada kutokana na ukubwa wa madeni kiliwashitua watanzania wengi,”
“Ni wazi kauli hiyo ililenga kudhoofisha utendaji kazi wa Rais Samia lakini pia kuwaonesha wale wasiopenda mafanikio yake kwamba nchi imemshinda kutokana na kutegemea kuiendesha kwa mikopo, kitu ambacho hakikuwa na ukweli wowote, bali ni kusukumwa na uroho wa madaraka," ameeleza Mgeja.
Amesema Job Ndugai hakuidharau tu Ikulu, hakumdharau tu na kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan bali aliwadharau Watanzania wote kwa vile unapomgusa Rais unakuwa umewagusa watanzania wote na wao sasa hawatapenda hata kuona hilo bango la Job Ndugai lililopo katika Soko Kuu la Dodoma na kushauri ni vyema likaondolewa.
“Kwa makosa hayo aliyoyafanya Ndugai kwa kweli hata kama kutakuwa na kumbukumbu zake zilizoandikwa katika majengo ya umma ziondolewe mara moja, nchi nyingine hata mabango, sanamu za viongozi wanaofanya mambo ya hovyo huwa yanaharibiwa na mengi huvunjwa kwa hasira na wananchi,” ameongeza Mgeja.
Amesema kwa vile watanzania tuna asili ya ustaarabu basi itumike busara tu kwa kuondoa majina yake popote pale yalipo mfano kule mkoani Dodoma ambako kuna jina lake kwenye Soko la Kisasa lililopewa jina la Ndugai.
Kwa upande mwingine Mgeja ambaye pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa mkoa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga ametoa ushauri wake kwa wote waliokuwa nyuma ya Ndugai wajitathimini haraka na ikiwezekana wachukue maamuzi kama yaliyochukuliwa na nahodha wao Ndugai kwa kujiuzulu ili wapishe kazi ziendelee.
“Katika Mtafaruku huu bado mabaki ya Ndugai yapo, watu wake na genge lao lipo. Genge hili tulilisema huko nyuma tulipozungumza kumuonya Polepole na Genge lake sasa wasisubiri tena wananchi waanze kuwanyoshea vidole, walinde heshima zao, wachukue maamuzi magumu kwa kujiuzulu kwenye nyadhifa walizonazo,”
“Huko nyuma sisi wazee wa Shinyanga tulikemea sana tabia ya Humphrey Polepole na kundi lake na tulieleza wazi hawa nyuma ya pazia wana jambo lao, na hakuwa Polepole peke yake nyuma alikuwa na kundi kubwa, sasa hili genge tayari kiongozi wao (Ndugai) amejipambanua tunashauri wafuasi wasisubiri tuwasonte vidole,” ameeleza Mgeja.
Mmoja wa wakazi hao, ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Mzalendo Foundation ya Mjini Kahama Mkoani Shinyanga, Khamis Mgeja ameishauri Serikali kuangalia uwezekano wa kuondoa jina la Ndugai katika maeneo yote ya majengo ya Umma.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Shinyanga, Mgeja amesema kitendo kilichotendwa na Ndugai cha kuikosoa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Samia Suluhu Hassan ni sawa na kuinajisi nchi hivyo kuendelea kuonekana kwa jina lake katika majengo ya umma ni kuwatia kichefuchefu watanzania.
Mgeja amewapongeza watanzania kwa jinsi walivyoonesha mshikamano wa "nguvu ya Umma" mara baada ya Ndugai kutoa kauli yake ya kuikosoa Serikali kuhusiana na suala zima la mikopo kwa ajili ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa hapa nchini ambapo alidai nchi inaweza kupigwa mnada kwa kuzidiwa na mikopo.
Amesema kitendo cha wananchi kuonesha mshikamano katika kupinga kwa nguvu zote kauli hiyo ya Ndugai kimeweza kumng'oa katika nafasi yake na kwamba siku zote nguvu ya umma ina nguvu kuliko kitu chochote katika nchi yoyote duniani na inaweza kumng'oa ye yote bila kujali "Ubabe" alionao.
Pamoja na kuishauri Serikali iangalie uwezekano wa kuondoa jina la Ndugai kwenye majengo yote ya Umma pia Mgeja ambaye ni Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga amewashauri wale wote waliokuwa nyuma ya Ndugai wajitathimini na ikibidi wachukue maamuzi kama aliyochukua "Boss" wao.
“Binafsi nimefurahishwa na kitendo cha Mheshimiwa Ndugai kutangaza kujiuzulu wadhifa wake wa Uspika wa Bunge letu tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kweli kitendo chake cha kudai nchi yetu inaweza kupigwa mnada kutokana na ukubwa wa madeni kiliwashitua watanzania wengi,”
“Ni wazi kauli hiyo ililenga kudhoofisha utendaji kazi wa Rais Samia lakini pia kuwaonesha wale wasiopenda mafanikio yake kwamba nchi imemshinda kutokana na kutegemea kuiendesha kwa mikopo, kitu ambacho hakikuwa na ukweli wowote, bali ni kusukumwa na uroho wa madaraka," ameeleza Mgeja.
Amesema Job Ndugai hakuidharau tu Ikulu, hakumdharau tu na kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan bali aliwadharau Watanzania wote kwa vile unapomgusa Rais unakuwa umewagusa watanzania wote na wao sasa hawatapenda hata kuona hilo bango la Job Ndugai lililopo katika Soko Kuu la Dodoma na kushauri ni vyema likaondolewa.
“Kwa makosa hayo aliyoyafanya Ndugai kwa kweli hata kama kutakuwa na kumbukumbu zake zilizoandikwa katika majengo ya umma ziondolewe mara moja, nchi nyingine hata mabango, sanamu za viongozi wanaofanya mambo ya hovyo huwa yanaharibiwa na mengi huvunjwa kwa hasira na wananchi,” ameongeza Mgeja.
Amesema kwa vile watanzania tuna asili ya ustaarabu basi itumike busara tu kwa kuondoa majina yake popote pale yalipo mfano kule mkoani Dodoma ambako kuna jina lake kwenye Soko la Kisasa lililopewa jina la Ndugai.
Kwa upande mwingine Mgeja ambaye pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa mkoa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga ametoa ushauri wake kwa wote waliokuwa nyuma ya Ndugai wajitathimini haraka na ikiwezekana wachukue maamuzi kama yaliyochukuliwa na nahodha wao Ndugai kwa kujiuzulu ili wapishe kazi ziendelee.
“Katika Mtafaruku huu bado mabaki ya Ndugai yapo, watu wake na genge lao lipo. Genge hili tulilisema huko nyuma tulipozungumza kumuonya Polepole na Genge lake sasa wasisubiri tena wananchi waanze kuwanyoshea vidole, walinde heshima zao, wachukue maamuzi magumu kwa kujiuzulu kwenye nyadhifa walizonazo,”
“Huko nyuma sisi wazee wa Shinyanga tulikemea sana tabia ya Humphrey Polepole na kundi lake na tulieleza wazi hawa nyuma ya pazia wana jambo lao, na hakuwa Polepole peke yake nyuma alikuwa na kundi kubwa, sasa hili genge tayari kiongozi wao (Ndugai) amejipambanua tunashauri wafuasi wasisubiri tuwasonte vidole,” ameeleza Mgeja.