Mgeni aingia Dar, wenyeji wamfurahia

Mchumi90

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2015
Posts
1,099
Reaction score
1,315
Hatimae jiji la Dar es Salaam limepata ugeni mzito kutoka kanda ya ziwa. Ugeni huu umewafurahisha wakazi wengi wa jiji la DSM na viunga vyake na wengi wao wakimtaka abaki nao kwa muda mrefu zaidi kwani anawapa faraja sana kipindi hiki wanavyojaribu kupambana na HAPA KAZI TU. Mgeni huyo amajitahidi kutembelea maeneo yote ya jiji bila kubagua tabaka lolote, Masaki, Mikocheni amefika pia huku kwetu Majimatitu pia amefika. Tunasema karibu nasi kwani umekuwa mkombozi wetu kwa kipindi hiki kigumu.



Wakuu karibuni BALIMI.
 
siku mbili hizi zimekuwa adimu hazipatikani tena
 
Ha ha ha ha huyu mgeni watu wanampapakatia sana aisee!...watu wanamnywa kama hawana akili nzuri, nasikia hata bei yake ya 1,500/ kwa usawa huu amekuwa mkombozi kwa wale ambao hawawezi lala bila kupiga Yale Maji ya dhahabu!
 
Bia tam, bia nzito, imetengenezwa kitaalam sana, hatimae serengeti apata mbabe wake
 
Unafanya kazi nzuri Mr marketing manager...ila wamekuangusha watu wa branding...haivutiii....
Ila hongereni, nitaijaribu leo
 
Yaani hii beer niliijaribu for two days na ikaninyorosha, ilinichosha na nikawa nasinzia kama teja. Siigusi tena aisee. Sasa hivi natiririka na Kill ndogo tu na konyagi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…