Mgodi wa dhahabu unatafuta muwekezaji au mnunuzi mkoa wa Mtwara

Mgodi wa dhahabu unatafuta muwekezaji au mnunuzi mkoa wa Mtwara

wanchijiko

Member
Joined
Jul 14, 2019
Posts
20
Reaction score
14
RIPOTI FUPI YA UHITAJI WA UWEKEZAJI AU MNUNUZI WA MGODI WA DHAHABU

Historia:
mgodi una leseni PMLs na ziko tatu zilizo ungana pamoja
Mgodi ulianza rasmi shughuli za uchimbaji mwaka 2019. Ni mgodi mpya ambao bado haujafikia uchimbaji wa kina, kwani uchimbaji upo kwenye miamba laini karibu na uso wa ardhi kwa ufupi ndio kwanza uko juu . Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa dhahabu inapatikana hata juu kabisa ya uso wa ardhi. Kiasi cha dhahabu kinachopatikana kutoka kwenye viroba vidogo vinne vya udongo kinakadiriwa kuwa kati ya 0.5 gram na 1.5 gram, na kiwango hiki huongezeka kadri uchimbaji unavyoendelea kwenda chini.
Ripoti zilizowahi kufanyika zinathibitisha kiwango cha dhahabu kilichopo kwenye mgodi, ambapo kiwango cha PPM (parts per million) kinaanzia 1.5 ppm hadi 5 ppm, kulingana na tabaka lililotolewa sampuli. Hii inaashiria uwepo wa dhahabu wa kiwango cha kutosha kufanya mgodi huu kuwa na faida kubwa iwapo utaendelezwa ipasavyo.

2. a. Fursa ya Uwekezaji
Mgodi huu unaonyesha uwepo wa dhahabu wa kiwango cha kuridhisha, na bado haujachunguzwa kikamilifu.
Kuna nafasi kubwa ya kuendeleza uchimbaji kwa kutumia vifaa vya kisasa ili kufikia dhahabu zaidi.
Hii ni fursa ya kipekee ya kushiriki kwenye sekta ya madini yenye faida kubwa, hasa wakati ambapo bei ya dhahabu kimataifa iko juu.
b.Fursa ya kununua
Endapo mtu au kampuni ikijitokeza ikiwa na hitaji la kununua pasipo kutaka kuingia ubia ,ilo linawezekana tutazungumza tukifikia makubaliano biashara inafanyika


3. Changamoto za Sasa
Excavator: Mgodi unahitaji excavator kutokana na aina ya matabka kuwa laini hivyo ukatika mara kwa mara , ivyo tulishauliwa na tume madini ili kuondoa udongo na miamba kwa ufanisi lazima uchimbwe kwa excavator adi pale utapofika katika matabaka magumu
Shimo la wazi (Open Pit): Kwa usalama na ushauri wa Tume ya Madini, uchimbaji unapaswa kufanyika kwa njia ya shimo la wazi (open pit) ili kupunguza hatari.
Kemikali za Kuchuja: Mgodi unahitaji kemikali za leaching ili kuchuja dhahabu kutoka kwenye mchanga. Hii inahitaji gharama kubwa kwa ajili ya ununuzi na usalama wa utumiaji.
Gharama za Uendeshaji: Gharama za uendeshaji kwa ujumla, pamoja na kulipia vifaa, kulipia mishahara ya wafanyakazi, na matumizi ya kemikali, ni changamoto kubwa kwa sasa.
Miundombinu:
Umeme wa uhakika: Mgodi umeletwa umeme wa uhakika, ambao unahitajika kwa shughuli zote za uchimbaji na usindikaji wa dhahabu.
Maji ya bomba: Kuna upatikanaji wa maji ya bomba kwa ajili ya matumizi ya kila siku, ikiwa ni pamoja na mchakato wa uchimbaji na usindikaji.
Vat Leaching Plant: Mgodi umejenga tank mbili za vat leaching plant ndogo kwa ajili ya kuchuja dhahabu kutoka kwenye mchanga.
Mwalo wa Kuoshea: Kuna mwalo wa kuoshea vifaa na uchimbaji ili kudumisha usafi wa mazingira na vifaa.
Crusher: Mgodi unatumia crusher moja ili kupunguza ukubwa wa mawe ya madini kabla ya kuendelea na michakato mingine.
4. Mahitaji ya Mgodi
Uwekezaji wa Gharama za Uendeshaji: Mgodi unahitaji muwekezaji ambaye atajiunga na mgodi kwa njia ya ubia au kununua mgodi kwa jumla.
Muwekezaji huyo atahitajika kuingiza gharama za uendeshaji na vifaa vya kazi kama excavator, vinu vya kusagia, na vifaa vingine vya uchimbaji ili kuzalisha dhahabu kwa ukubwa na kupata faida kubwa.
Hii itahakikisha uzalishaji mkubwa wa dhahabu kwa gharama nafuu, na mgodi unaweza kufikia viwango vya juu vya uzalishaji.
Kuna pia uwezekano wa kuuza mgodi kwa mteja anayehitaji kumiliki mgodi na kuendeleza uchimbaji kwa manufaa yake mwenyewe.
5. Fursa za Kibiashara
Thamani ya Dhahabu: Tanzania ni moja ya wazalishaji wakubwa wa dhahabu Afrika, na mgodi huu uko kwenye eneo lenye historia ya madini.
Soko la Ndani na Nje: Dhahabu inahitajika sana ndani na nje ya nchi, na kuna soko thabiti kwa uzalishaji mpya.
Faida ya Kijiografia: Mgodi uko kwenye eneo linalofikika kirahisi 2km kutokea kijijini, na hii inapunguza changamoto za usafirishaji wa madini.

6. Mahitaji ya Uwekezaji
Mgodi unahitaji uwekezaji katika maeneo yafuatayo:
Kuandaa ripoti ya kijiolojia (hii ni chaguo ikiwa mwekezaji ataamua kufanya hivyo).
Kununua au kukodisha excavator na vifaa vya uchimbaji.
Gharama za ununuzi wa kemikali za kuchuja madini (leaching chemicals).
Gharama za uendeshaji na kulipia madeni.
Kuajiri wataalamu wa madini na kuongeza nguvu kazi.

7. Mapato Yanayotarajiwa
Mgodi unatarajiwa kuzalisha kiasi kikubwa cha dhahabu kwa kutumia vifaa vya kisasa. Uzalishaji mkubwa unatarajiwa kutoa mapato yanayoweza kuwa ya juu, na faida inaweza kuwa kubwa kutokana na uzalishaji wa dhahabu.
8. Faida kwa Mwekezaji
Fursa ya kushiriki kwenye sekta ya madini yenye faida kubwa.
Mrejesho wa uwekezaji katika muda mfupi kupitia uzalishaji wa dhahabu.
Ushirikiano wa muda mrefu na nafasi ya kupanua shughuli za madini.

9. Hitimisho
Mgodi ni fursa bora ya uwekezaji kwa mtu au kampuni inayotaka kuwekeza kwenye madini ya dhahabu. Uwezo wa mgodi huu umeonekana kupitia uzalishaji wa awali, ripoti za kiwango cha PPM, na miundombinu ya msingi. Tunaamini kupitia uwekezaji wa mtaji na teknolojia, tunaweza kuufanya mgodi huu kuwa chanzo cha mapato makubwa kwa pande zote mbili.
KWA MWENYE KUGUSWA NA FURSA HII AU MDAU YEYOTE MWENYEWE CONNECTION UNAKARIBISHWA NA DILI LIKIKITIKI KUNAKIFUTA JASHO

mawasiliano zaidi ni PM
 
Katika kupata mnunuzi au muwekezaji wengi hutaka kujua exploration report SASA nyie hapo mmefanya exploration? Maana mnunuzi ni ngumu kuwekeza mpunga mrefu pasipo kujua Mali IPO kwa UKubwa gani. Kama hiyo report ipo sema nimlete machina chap
 
Katika kupata mnunuzi au muwekezaji wengi hutaka kujua exploration report SASA nyie hapo mmefanya exploration? Maana mnunuzi ni ngumu kuwekeza mpunga mrefu pasipo kujua Mali IPO kwa UKubwa gani. Kama hiyo report ipo sema nimlete machina chap
Uko sahihi,lakin kama uko katika hii industry nadhani unajua gharama za kuipata iyo geology report so kitu rahisi kwa mitaji yetu ya kuunga unga ni sawa au zaidi ya pesa unayoitafuta katika haraka zetu izi.
Alafu mbona wachina ni watu ambao hawana sana mambo ya report wanahitaji wafike site nawajiridhishe wenyewe physically na wakisha ona dhahabu hatua zngine zina fuata,
 
Uko sahihi,lakin kama uko katika hii industry nadhani unajua gharama za kuipata iyo geology report so kitu rahisi kwa mitaji yetu ya kuunga unga ni sawa au zaidi ya pesa unayoitafuta katika haraka zetu izi.
Alafu mbona wachina ni watu ambao hawana sana mambo ya report wanahitaji wafike site nawajiridhishe wenyewe physically na wakisha ona dhahabu hatua zngine zina fuata,
Ninajua na ndio ukweli lakini ni ngumu kupata investor bila kuwa na report Mzee, huo ndio ukweli okay let's say wewe ndio investor utaweka vipi uwekezaji eneo ambalo hakuna uhakika wa uzalishaji? Maana yawezekana hiyo ppm1.5 ni Ka mchirizi Tu lakini pia ppm ya 1.5 ni ndogo Sana kupata muwekezaji maana hairudishi gharama labda kama huko chini zaidi itapanda. kama report ipo, asubuhi Tu investor namleta. Na mpaka SASA nimeshampeleka huko mwabomba kanunua mgodi 20 mil USD. Kikubwa ni report ya exploration hapo mtakaa mezani kujadili kulingana na ppm na Hali zingine kama water base, na changamoto nyingine zitakazoonekana kwenye report mkuu.
Kuna maelezo mengi yalishapimwa ishu vizuri na watu WA wizarani kupata reports kama fedha ni changamoto
 
Katika kupata mnunuzi au muwekezaji wengi hutaka kujua exploration report SASA nyie hapo mmefanya exploration? Maana mnunuzi ni ngumu kuwekeza mpunga mrefu pasipo kujua Mali IPO kwa UKubwa gani. Kama hiyo report ipo sema nimlete machina chap
Wengi wanakwambia mwekezaji ndio afanye.. yaani nilete hela zangu nikiwa sina uhakika hapo ndipo wanafeli
 
Ninajua na ndio ukweli lakini ni ngumu kupata investor bila kuwa na report Mzee, huo ndio ukweli okay let's say wewe ndio investor utaweka vipi uwekezaji eneo ambalo hakuna uhakika wa uzalishaji? Maana yawezekana hiyo ppm1.5 ni Ka mchirizi Tu lakini pia ppm ya 1.5 ni ndogo Sana kupata muwekezaji maana hairudishi gharama labda kama huko chini zaidi itapanda. kama report ipo, asubuhi Tu investor namleta. Na mpaka SASA nimeshampeleka huko mwabomba kanunua mgodi 20 mil USD. Kikubwa ni report ya exploration hapo mtakaa mezani kujadili kulingana na ppm na Hali zingine kama water base, na changamoto nyingine zitakazoonekana kwenye report mkuu.
Ninajua na ndio ukweli lakini ni ngumu kupata investor bila kuwa na report Mzee, huo ndio ukweli okay let's say wewe ndio investor utaweka vipi uwekezaji eneo ambalo hakuna uhakika wa uzalishaji? Maana yawezekana hiyo ppm1.5 ni Ka mchirizi Tu lakini pia ppm ya 1.5 ni ndogo Sana kupata muwekezaji maana hairudishi gharama labda kama huko chini zaidi itapanda. kama report ipo, asubuhi Tu investor namleta. Na mpaka SASA nimeshampeleka huko mwabomba kanunua mgodi 20 mil USD. Kikubwa ni report ya exploration hapo mtakaa mezani kujadili kulingana na ppm na Hali zingine kama water base, na changamoto nyingine zitakazoonekana kwenye report mkuu.

Ninajua na ndio ukweli lakini ni ngumu kupata investor bila kuwa na report Mzee, huo ndio ukweli okay let's say wewe ndio investor utaweka vipi uwekezaji eneo ambalo hakuna uhakika wa uzalishaji? Maana yawezekana hiyo ppm1.5 ni Ka mchirizi Tu lakini pia ppm ya 1.5 ni ndogo Sana kupata muwekezaji maana hairudishi gharama labda kama huko chini zaidi itapanda. kama report ipo, asubuhi Tu investor namleta. Na mpaka SASA nimeshampeleka huko mwabomba kanunua mgodi 20 mil USD. Kikubwa ni report ya exploration hapo mtakaa mezani kujadili kulingana na ppm na Hali zingine kama water base, na changamoto nyingine zitakazoonekana kwenye report mkuu.
Kuna maelezo mengi yalishapimwa ishu vizuri na watu WA wizarani kupata reports kama fedha ni changamoto
Iyo ppm kadri unavoenda chini inaongeza na hata ukubwa wa mchirizi inaongezeka coz apo ndipo ilipopulia yani ata ukikusanya udogo ukipiga chabo unaziona dhahabu,
"Kuna maelezo mengi yalishapimwa ishu vizuri na watu WA wizarani kupata reports kama fedha ni changamoto"
Apo nifafanulie vizuri sijakuelewa kiongozi
 
Kuna maeneo
"Kuna maelezo mengi yalishapimwa ishu vizuri na watu WA wizarani kupata reports kama fedha ni changamoto"
Apo nifafanulie vizuri sijakuelewa kiongozia

Kuna maeneo yalishfanyiwa tafiti kitambo ripoti zake zipo,kuzitoa wizarani ndio lazima kuhonga. Muwekezaji kuanza kumuelezea mambo ya chabo ni ngumu maana wewe ni mchimbaji unajua ilivyo risk. Gharama za mchimbaji ni kubwa SASA utamshawishi VP bila vielelezo? Ndio maana nakwambia kupata muwekezaji WA uhakika geological report ni muhimu zaidi
 
Bila the JORC au NI 43-101 report hamna mtu ataweka hela zake. Hiyo ndo standard ya mining industry. Hakuna mtu anawekeza kwa Imani tu.

Ukiwa na report investors wapo wengi sana hata 10M USD and above utapata. Investors wengi wanataka wewe ndo ufanye exploration sio wao. Wakiamua kufanya wao basi hawakuhitaji wewe hizo PML hata kwa laki2 unapata.
 
Ninajua na ndio ukweli lakini ni ngumu kupata investor bila kuwa na report Mzee, huo ndio ukweli okay let's say wewe ndio investor utaweka vipi uwekezaji eneo ambalo hakuna uhakika wa uzalishaji? Maana yawezekana hiyo ppm1.5 ni Ka mchirizi Tu lakini pia ppm ya 1.5 ni ndogo Sana kupata muwekezaji maana hairudishi gharama labda kama huko chini zaidi itapanda. kama report ipo, asubuhi Tu investor namleta. Na mpaka SASA nimeshampeleka huko mwabomba kanunua mgodi 20 mil USD. Kikubwa ni report ya exploration hapo mtakaa mezani kujadili kulingana na ppm na Hali zingine kama water base, na changamoto nyingine zitakazoonekana kwenye report mkuu.
Kuna maelezo mengi yalishapimwa ishu vizuri na watu WA wizarani kupata reports kama fedha ni changamoto
Kiongozi zoezi la report ndio liko mbioni kukamilika hivyo ikiwa tayar nitakutafuta tuone namna ya kufanya
 
Kiongozi zoezi la report ndio liko mbioni kukamilika hivyo ikiwa tayar nitakutafuta tuone namna ya kufanya

Hakuna exploration survey inafanyika in one month. Kampuni gani inafanya survey yako?

Naona wabongo wengi hamjui hizi ripoti zinakuwaje for international investors to consider them ngoja nikuwekee hapa ripoti ya mgodi wa Magamba Handeni ujionee mfano ulinganishe na hiyo yako kama inafikia hata robo ya hii in details. Hizi survey can easily cost north of 500k USD.
 

Attachments

Hakuna exploration survey inafanyika in one month. Kampuni gani inafanya survey yako?

Naona wabongo wengi hamjui hizi ripoti zinakuwaje for international investors to consider them ngoja nikuwekee hapa ripoti ya mgodi wa Magamba Handeni ujionee mfano ulinganishe na hiyo yako kama inafikia hata robo ya hii in details. Hizi survey can easily cost north of 500k USD.
Ni sehemu ilishawai fanywa tafiti na kampuni xxxx siwezi itaja ndio tunainyonya kutoka kwa iyo kampuni wana report whole village ikiwemo na site yetu ilipo. Coz n leseni ambayo imezungukwa na PL za graphit za iyo kampuni, hivyo katika kufatilia utaratibu ndipo tukaambiwa eneo liko na report tayar na hata watu wa GST wathitisha ilo .so ukihitaji details ni PM
 
Back
Top Bottom