Tembea uone , jamani dar kweli ni kubwa na mgogoro huu nimeupata sehemu fulani hebu pata mkasa ulivyo
Mzee athumani mwinyi mvua ( sio jina halisi) aliuza shamba lake la heka mia moja kwa bwana michael ( sio jina halisi) mnamo mwaka 1989. Bwana michael akafuata taratibu zote na kulimiliki kihalali eneo hilo mwaka 1990 kwa kupata hati miliki kutoka wizara ya ardhi. Tangu anunue na kuanza kulimiliki kihalali shamba hilo bwana michael alitembelea si zaidi ya mara mbili shamba hilo akiwa na watoto wake wawili moja ana umri wa mika minne na mwingine ana umri wa miaka miwili. Mwaka 1992 alihamia marekani na kwa bahati mbaya alifariki kwa ajali ya gari na kuwaacha watoto wake pamoja na mke wake huko marekani na huo ndio ukawa mwisho wa bwana michael. Hivyo mzee Mwinyimvua ambaye alikuwa ameuza shamba akaendelea kuliangalia shamba hilo na kumweleza siri hiyo mwanae shomari. kuwa alinde shamba la watu na ikitokea watoto wa bwana michael wamerudi wapewe eneo lao. matajiri wengi walilitamani shmaba hilo na walimwendea shomari kwa ahadi lukuki ili awauzie lakini shomari alikataa. Mnamo mwaka 1999 mwenyekiti wa serikali ya mtaa na mjumbe wa eneo hilo bwana chakupewa akauza kwa siri hekari hamsini kwa bwana siyangu na kumwandikia karatasi zote mbili zenye sahihi yake na mihuri kama mjumbe na mwenyekiti wa serikali ya mtaa. mwaka 2000 mzee chakupewa akafariki. hivyo akateuliwa mjumbe na kuchaguliwa mwenyekiti mwingine. Mwaka 2001 bwana siyangu akaja na watu wa ardhi ili afanye tasmini na apate hati miliki. kwa bahati nzuri mtoto wa mzee mwinyimvua , shomari ndio aliteuliwa kushika wadhifa wa ujumbe hivyo alipomwendea shomari na kumweleza kuhusu tasmini shomari alishangaa na kumwambia kuwa ametapeliwa na yeye kama mjumbe mwenye eneo hilo anayemiki kihalali ambaye ni mareheru michel, na huyo mtu aliyemuuzia siyangu sio mmiliki halai wa eneo lile alitumia vyeo vyake kuandaa karatasi na mashahidi wa uwongo. Bwana siyangu alitaharuki baada ya kupewa ukweli na akaamua kuongea na watu wa ardhi wamtengenezee hati miliki kwa kutumia barua za yule aliyemtapeli. na kwa sababu pesa zinaongea bwana siyangu alifanikiwa kupata hati miliki. Bwana siyangu akaliacha eneo lake pasipo kuliendeleza kuanzia mwaka 2001. Mnamo june 2009 wananchi wa eneo hilo baada ya kuona eneo hilo limekuwa ni kichaka na maficho kwa wezi kwani watu walikuwa wanakabwa na wakina mama kubakwa. wakaamua kuvamia shamba hilo la hekari mia zikiwemo zile hamsini za bwana siyangu. wakakata miti na kusafisha eneo lote kuwa jeupe na kila mtu akajigawia kwa jinsi anavyoweza na kuanza kujenga nyumba na wengine misingi. bwana siyangu akajitokeza september 2009 na kuanza kudai heka hamsini zake na kubomoa misingi na nyumba ambazo zilikuwa ndani ya eneo lake na kufungua kesi polisi kwamba watu wavamia shamba lake na kukata mazao yao yenye thamani ya milioni nane. hivyo anawatishia watu polisi na sio kuwapeleka mahakamani akawashitaki.
Walio bomolewa nyumba wanamuogopa bwana siyangu. Kwani hawana barua yoyote ya kuwatambua kama ni wamiliki halali wa eneo hilo . kwani mjumbe ambae ni bwana shomari anawaona kuwa bwana siyangu na watu wote ni wavamizi wa eneo la marehemu michael. vivyo wanaogopa kumpeleka bwana siyangu mahakamani. na bwana siyangu hataki kuwashitaki mahakamani. kuna watu wengine ambao ni wabishi wameendelea kujenga kwa kujificha wakiogopa polisi ambao bwana siyangu huwa anawaleta kwa kuwatisha na sio kwenda mahakamani kuomba sop warant ili watu wasiendelee kujenga.
jamani naomba buasra zenu wanasheria
Mzee athumani mwinyi mvua ( sio jina halisi) aliuza shamba lake la heka mia moja kwa bwana michael ( sio jina halisi) mnamo mwaka 1989. Bwana michael akafuata taratibu zote na kulimiliki kihalali eneo hilo mwaka 1990 kwa kupata hati miliki kutoka wizara ya ardhi. Tangu anunue na kuanza kulimiliki kihalali shamba hilo bwana michael alitembelea si zaidi ya mara mbili shamba hilo akiwa na watoto wake wawili moja ana umri wa mika minne na mwingine ana umri wa miaka miwili. Mwaka 1992 alihamia marekani na kwa bahati mbaya alifariki kwa ajali ya gari na kuwaacha watoto wake pamoja na mke wake huko marekani na huo ndio ukawa mwisho wa bwana michael. Hivyo mzee Mwinyimvua ambaye alikuwa ameuza shamba akaendelea kuliangalia shamba hilo na kumweleza siri hiyo mwanae shomari. kuwa alinde shamba la watu na ikitokea watoto wa bwana michael wamerudi wapewe eneo lao. matajiri wengi walilitamani shmaba hilo na walimwendea shomari kwa ahadi lukuki ili awauzie lakini shomari alikataa. Mnamo mwaka 1999 mwenyekiti wa serikali ya mtaa na mjumbe wa eneo hilo bwana chakupewa akauza kwa siri hekari hamsini kwa bwana siyangu na kumwandikia karatasi zote mbili zenye sahihi yake na mihuri kama mjumbe na mwenyekiti wa serikali ya mtaa. mwaka 2000 mzee chakupewa akafariki. hivyo akateuliwa mjumbe na kuchaguliwa mwenyekiti mwingine. Mwaka 2001 bwana siyangu akaja na watu wa ardhi ili afanye tasmini na apate hati miliki. kwa bahati nzuri mtoto wa mzee mwinyimvua , shomari ndio aliteuliwa kushika wadhifa wa ujumbe hivyo alipomwendea shomari na kumweleza kuhusu tasmini shomari alishangaa na kumwambia kuwa ametapeliwa na yeye kama mjumbe mwenye eneo hilo anayemiki kihalali ambaye ni mareheru michel, na huyo mtu aliyemuuzia siyangu sio mmiliki halai wa eneo lile alitumia vyeo vyake kuandaa karatasi na mashahidi wa uwongo. Bwana siyangu alitaharuki baada ya kupewa ukweli na akaamua kuongea na watu wa ardhi wamtengenezee hati miliki kwa kutumia barua za yule aliyemtapeli. na kwa sababu pesa zinaongea bwana siyangu alifanikiwa kupata hati miliki. Bwana siyangu akaliacha eneo lake pasipo kuliendeleza kuanzia mwaka 2001. Mnamo june 2009 wananchi wa eneo hilo baada ya kuona eneo hilo limekuwa ni kichaka na maficho kwa wezi kwani watu walikuwa wanakabwa na wakina mama kubakwa. wakaamua kuvamia shamba hilo la hekari mia zikiwemo zile hamsini za bwana siyangu. wakakata miti na kusafisha eneo lote kuwa jeupe na kila mtu akajigawia kwa jinsi anavyoweza na kuanza kujenga nyumba na wengine misingi. bwana siyangu akajitokeza september 2009 na kuanza kudai heka hamsini zake na kubomoa misingi na nyumba ambazo zilikuwa ndani ya eneo lake na kufungua kesi polisi kwamba watu wavamia shamba lake na kukata mazao yao yenye thamani ya milioni nane. hivyo anawatishia watu polisi na sio kuwapeleka mahakamani akawashitaki.
Walio bomolewa nyumba wanamuogopa bwana siyangu. Kwani hawana barua yoyote ya kuwatambua kama ni wamiliki halali wa eneo hilo . kwani mjumbe ambae ni bwana shomari anawaona kuwa bwana siyangu na watu wote ni wavamizi wa eneo la marehemu michael. vivyo wanaogopa kumpeleka bwana siyangu mahakamani. na bwana siyangu hataki kuwashitaki mahakamani. kuna watu wengine ambao ni wabishi wameendelea kujenga kwa kujificha wakiogopa polisi ambao bwana siyangu huwa anawaleta kwa kuwatisha na sio kwenda mahakamani kuomba sop warant ili watu wasiendelee kujenga.
jamani naomba buasra zenu wanasheria