Uchaguzi 2020 Mgombea ubunge wa Kigamboni kupitia ACT Wazalendo anapitia mazingira magumu mno kisiasa. Membe kawaangusha sana watu wake

Uchaguzi 2020 Mgombea ubunge wa Kigamboni kupitia ACT Wazalendo anapitia mazingira magumu mno kisiasa. Membe kawaangusha sana watu wake

dikteta2020

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2018
Posts
595
Reaction score
3,991
Hawa wagombea wachanga kama huyu wa Kigamboni waliingia kwenye kinyang'anyiro cha ubunge huku wakiamini fika kuwa ujio wa Membe ndani ya ACT Wazalendo ungekuwa mkombozi kwao na walitarajia angewainua vilivyo.

Membe hata alipokuwa Pemba na Unguja pamoja na Maalim alishindwa kabisa kutumia jukwaa lake vilivyo, mbaya zaidi Membe alishindwa kabisa kutumia ujasusi wake kuweka mgombea ubunge ndani ya jimbo analotoka.

Ilitegemewa kutokana na uzoefu wa Membe basi mgombea huyo angepita kama anateleza tu. Matokeo yake mgombea wa Chadema ndiye alionekana tishio dhidi ya Nape Nnauye wa CCM. Membe alishindwa kabisa kuhakikisha kuwa jimboni kwake anaweka mizizi.

Kiukweli Membe kawaangusha sana ACT Wazalendo, pongezi kwa CHADEMA kwa kumgundua mapema. Ona sasa imebidi Zitto Kabwe ndiye awe mhimili wa chama kwa upande wa bara. Membe haonekani popote kumnadi mgombea yeyote wa ACT au hata kwenye vyombo vya habari. Huu ni zaidi ya usaliti.

 
Siku hizi kuhama ccm kwenda upinzani sio dili tena. Lowassa ndio alifanya hilo dili liwe haramu kwahiyo sasahivi watu hawana imani na makada wa muda huko CCM wanaokuja upinzani
 
Siku izi kuhama ccm kwenda upinzani sio dili tena. Lowassa ndio alifanya hilo dili iwe haramu kwaio saivi watu hawana iman na makada wa muda huko ccm wanaokuja upinzani

..upinzani kuna karaha zake.

..hivi kwa mfano Membe anaweza kukubali kupigwa mabomu, au kulala mahabusu?

..Na akipigwa mabomu unadhani mkewe na watoto wake watamwambia nini?

..Sumaye anasema alipokuwa upinzani familia yake ilikuwa inamsumbua.
 
Daaaa! Hadi huruma, yaani mdada mpaka anatamani kulia
 
Wewe MATAGA unataka Membe awapigie kampeni ili watu wajue bado anagombea kisha kura zigawanyike.

Huyo Binti anajijenga kisiasa bado mdogo sana, huko mbeleni atakuwa mwiba huyo.
 
Upinzani inabidi uingie ukiwa bado kijana.

Ukiwa CCM na kuonja utamu wa kubebwa na tume ya uchaguzi huwezi kuhamia upinzani na kudumu.
Lowasa kaingia upinzani akiwa mzee, lakini katikisa. Membe si mwanasiasa, alibebwa na chama. Ni vizuri katambua kuwa nje ya CCM yeye si lolote.
 
Kuna kitu hujui.Wanachama wa CCM ni weupe sana,yaani hawawezi kuhimili mikikimikiki.Membe huko CCM alikuwa amezoea miteremko ya bao la mkono,sasa unategemea huku upinzani ataweza kuhimili bao la ukweli?
 
"Kazi na bata" kwisha habari yake.
Zito afanye jitihada baada ya kuungana na Chadema ammalize Lissu kisiasa kama alivyommaliza Membe ili uchaguzi ujao kwenye anga la siasa pisiwepo na mtu wakuitwa Lissu.
 
"Kazi na bata" kwisha habari yake.
Zito afanye jitihada baada ya kuungana na Chadema ammalize Lissu kisiasa kama alivyommaliza Membe ili uchaguzi ujao kwenye anga la siasa pisiwepo na mtu wakuitwa Lissu.
Hii ni ndoto ya saa 12 jioni wakati shetani anarejea mwilini mwako, utasubiria sana kumuona Lisu akishuka chini mpaka uzeeke na kufariki pasipo ndoto yako ya kishetani kutimia
 
Lowasa kaingia upinzani akiwa mzee, lakini katikisa. Membe si mwanasiasa, alibebwa na chama. Ni vizuri katambua kuwa nje ya CCM yeye si lolote.

..Lowassa angetikisa zaidi kama angekuwa ana afya nzuri.

..pia nadhani alikuwa anapoteza kura na imani kadiri muda wa kampeni ulivyokuwa ukisonga mbele.
 
Membe atarudi CCM mapema zaidi ya mnavyofikiri. Hawezi mikikimikiki ya “kusumbuliwa” na kuulizwa asset hii na ile pale uliipataje.

Huyu Jasusi amefail vibaya sana na inaonekana hata ACT wenyewe walishagundua huyu ni liability tu
 
..Lowassa angetikisa zaidi kama angekuwa ana afya nzuri.

..pia nadhani alikuwa anapoteza kura na imani kadiri muda wa kampeni ulivyokuwa ukisonga mbele.

Lowasa ana 18% ya wapiga kura yeye kama yeye
 
Back
Top Bottom