Uchaguzi 2020 Mgombea Urais SAU: Magufuli amefanya kazi nzuri, nitamteua kuwa Waziri Mkuu endapo atakubali

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais SAU: Magufuli amefanya kazi nzuri, nitamteua kuwa Waziri Mkuu endapo atakubali

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Dodoma. Mgombea urais wa Chama cha Sauti ya Umma (Sau), Muttamwega Mgaywa amewataka Mawaziri watatu wa serikali ya Rais John Magufuli kwamba hatawaacha pindi akiingia Ikulu.

Mbali na mawaziri hao lakini amemtaja Rais Magufuli kuwa akikubali atampa nafasi ya Waziri Mkuu kwa kuwa ameridhishwa na utendaji wake na kuwa aliyoyafanya siyo ya kubeza.

Muttamwega ametoa kauli hiyo leo Oktoba 25,2020 jioni Jijini Dodoma akiwa safarini kuelekea Mara ambako amesema ndiko anakokenda kumalizia kampeni zake akisubiri kupelekwa Ikulu.

Mgombea huyo amewataja mawaziri ambao wanauguza moyo wake katika utendaji ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Ummi Mwalimu (Afya) na Selemani Jafo (Tamisemi) ambao amesema atawateua katika serikali yake.

“Kama mwenzako amefanya kazi nzuri basi mpongeze, huyu Rais Magufuli amefanya kazi kubwa na nzuri ni muhimu kushukuru, lakini mimi nitaanzia hapo alipoishia na nitaleta ndege 30 katika Uongozi wangu,” amesema Mgaywa.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dodoma. Mgombea urais wa Chama cha Sauti ya Umma (Sau), Muttamwega Mgaywa amewataka Mawaziri watatu wa serikali ya Rais John Magufuli kwamba hatawaacha pindi akiingia Ikulu.

Mbali na mawaziri hao lakini amemtaja Rais Magufuli kuwa akikubali atampa nafasi ya Waziri Mkuu kwa kuwa ameridhishwa na utendaji wake na kuwa aliyoyafanya siyo ya kubeza.

Muttamwega ametoa kauli hiyo leo Oktoba 25,2020 jioni Jijini Dodoma akiwa safarini kuelekea Mara ambako amesema ndiko anakokenda kumalizia kampeni zake akisubiri kupelekwa Ikulu.

Mgombea huyo amewataja mawaziri ambao wanauguza moyo wake katika utendaji ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Ummi Mwalimu (Afya) na Selemani Jafo (Tamisemi) ambao amesema atawateua katika serikali yake.

“Kama mwenzako amefanya kazi nzuri basi mpongeze, huyu Rais Magufuli amefanya kazi kubwa na nzuri ni muhimu kushukuru, lakini mimi nitaanzia hapo alipoishia na nitaleta ndege 30 katika Uongozi wangu,” amesema Mgaywa.
Mgombea urais hajui hata sifa zimpasazo Waziri mkuu?

SAU bure kabisa!
 
Back
Top Bottom