Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Dodoma. Mgombea urais wa Chama cha Sauti ya Umma (Sau), Muttamwega Mgaywa amewataka Mawaziri watatu wa serikali ya Rais John Magufuli kwamba hatawaacha pindi akiingia Ikulu.
Mbali na mawaziri hao lakini amemtaja Rais Magufuli kuwa akikubali atampa nafasi ya Waziri Mkuu kwa kuwa ameridhishwa na utendaji wake na kuwa aliyoyafanya siyo ya kubeza.
Muttamwega ametoa kauli hiyo leo Oktoba 25,2020 jioni Jijini Dodoma akiwa safarini kuelekea Mara ambako amesema ndiko anakokenda kumalizia kampeni zake akisubiri kupelekwa Ikulu.
Mgombea huyo amewataja mawaziri ambao wanauguza moyo wake katika utendaji ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Ummi Mwalimu (Afya) na Selemani Jafo (Tamisemi) ambao amesema atawateua katika serikali yake.
“Kama mwenzako amefanya kazi nzuri basi mpongeze, huyu Rais Magufuli amefanya kazi kubwa na nzuri ni muhimu kushukuru, lakini mimi nitaanzia hapo alipoishia na nitaleta ndege 30 katika Uongozi wangu,” amesema Mgaywa.
Mbali na mawaziri hao lakini amemtaja Rais Magufuli kuwa akikubali atampa nafasi ya Waziri Mkuu kwa kuwa ameridhishwa na utendaji wake na kuwa aliyoyafanya siyo ya kubeza.
Muttamwega ametoa kauli hiyo leo Oktoba 25,2020 jioni Jijini Dodoma akiwa safarini kuelekea Mara ambako amesema ndiko anakokenda kumalizia kampeni zake akisubiri kupelekwa Ikulu.
Mgombea huyo amewataja mawaziri ambao wanauguza moyo wake katika utendaji ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Ummi Mwalimu (Afya) na Selemani Jafo (Tamisemi) ambao amesema atawateua katika serikali yake.
“Kama mwenzako amefanya kazi nzuri basi mpongeze, huyu Rais Magufuli amefanya kazi kubwa na nzuri ni muhimu kushukuru, lakini mimi nitaanzia hapo alipoishia na nitaleta ndege 30 katika Uongozi wangu,” amesema Mgaywa.