Uchaguzi 2020 Mgombea Urais wa ADC, Queen Cuthbert Sendiga aendelea na kampeni zake Mkoa wa Pwani (Sept 3, 2020)

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais wa ADC, Queen Cuthbert Sendiga aendelea na kampeni zake Mkoa wa Pwani (Sept 3, 2020)

ADC Party

Member
Joined
Sep 14, 2020
Posts
28
Reaction score
29
Mgombea wa kiti cha Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ADC, Bi Queen Cuthbert Sendiga ameendelea na kampeni zake leo katika Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Bagamoyo.

Leo hii mapema akiwa katika viwanja vya oko la Samaki aliweza kuelezea vipaumbele vyake 3 ambavyo vipo ndani ya Ilani hasa akigusia katika sekta ya Uvuvi alisema haya:

"Wavuvi ni kundi kubwa sana ambalo ukiwatengenezea maisha mazuri, mipango na taratibu tunatengeneza ajira nyingi sana za kutosha na zenye uhakika badala ya kwamba mvuvi akiumwa siku tatu ama siku nne hawezi kwenda kuvua tena sababu hakuna uwezo wa kuweka akiba.

“Chama cha ADC chini ya uongozi wangu kwa miaka mitano tunaenda kuhakikisha mvuvi wa kitanzania anaenda kua mvuvi bora, mwenye kupatiwa elimu juu ya shughuli zake za uvuvi, mwenye kupatiwa vitendea kazi bora na kuondolewa tozo zisizoendana na uwezo wake wa kuvua, na cha mwisho anaenda kuongezewa thamani ya bidhaa zake zinazotoka baharini ili iweze kumkwamua kutoka alipo kimaisha "

PICHA: Mgombea wa Urais kupitia ADC akiongea na wananchi, wavuvi na wafanyabiashara wa Soko la Samaki huko Bagamoyo mapema leo Jumamosi, Septemba 3, 2020 👇🏾

781EC9A6-A5C0-47A4-B470-28C6570C2632.jpeg

8246C491-3E2C-4A42-964F-438D45F2845F.jpeg

EB6570AC-916D-44D5-8BCF-4C7BCE3C1F4E.jpeg

CE786512-74C3-4F42-8A1D-9CF699863FD1.jpeg

1ACFE4C8-3090-449C-9505-E62FD631584E.jpeg
 
Huyu dada ananadi sera zake atafanya nini endapo akipewa nafasi ya kuongoza serikali na sio malalamiko kama wakina flani.
 
kusema ukwel dada anajua nini anfnya kameni z kistaraabu na anajua nini anaongea,nadhani wengi mkimskia na jinsi anavyohangaika kufanya kampeni hasa sehemu ngum kutokana na uwezo wake hakika akisikilizwa huenda upepo ukageuka
 
She is an outsider only to re- right history.
 
Huyu dada hata asiposhinda ila atayeshinda amfikirie kidogo kwenye uteuzi ni mstarabu kupitiliza
Awali yayote toka moyoni napenda kumpongeza sana huyu mama. Ameonyesha ukomavu na ustahimilivu wa hali ya juu tangu zoezi la uchaguzi lianze mpaka leo. Amepambana kuliko kina Shibuda na mzee wa matreka na miwa (Mgaya). Huu ni mfano wa kutosha kwani amepiga kampeni za kutosha zaidi hata ya Membe na yule mgombea wa Mbatia. Hongera sana Queen.
 
Back
Top Bottom