Mgonjwa kutoa sadaka; Mchungaji yupo sahihi?

Mgonjwa kutoa sadaka; Mchungaji yupo sahihi?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Mimi sijazama sana kwenye biblia na neno la Mungu.
Nina jirani yangu hapa mdogo wake anaumwa masuala ya uzazi na vidonda vya tumbo. Ana hali ngumu sana kiafya na safari za Bugando haziishi. Pamoja na madaktari Dada jirani amekuwa na option ya kwenda mchungaji kuombewa na kukabidhi swala lake kwa Mungu amponye.

Watu hawa nawaonea huruma sana kwa sababu hawana bima na matibabu ni ghali.

Sasa mchungaji amewashauri wamtolee sadaka Mungu ili awaponye. Amesema ni sadaka ya nathiri wamtolee sana Bwana na wamuombe awaponye. Mchungaji amewasihi wasisite kumtolea Bwana kama wafanyavyo hospitali.

Hii imekaaje wakuu. Maana hawa ndugu wanapambana kupata fedha ya matibabu halafu tena sadaka?!

Tujadili bila kashfa wala matusi. Ni kwa hoja tu
 
Mimi sijazama sana kwenye biblia na neno la Mungu.
Nina jirani yangu hapa mdogo wake anaumwa masuala ya uzazi na vidonda vya tumbo. Ana hali ngumu sana kiafya na safari za Bugando haziishi. Pamoja na madaktari Dada jirani amekuwa na option ya kwenda mchungaji kuombewa na kukabidhi swala lake kwa Mungu amponye.

Watu hawa nawaonea huruma sana kwa sababu hawana bima na matibabu ni ghali.

Sasa mchungaji amewashauri wamtolee sadaka Mungu ili awaponye. Amesema ni sadaka ya nathiri wamtolee sana Bwana na wamuombe awaponye. Mchungaji amewasihi wasisite kumtolea Bwana kama wafanyavyo hospitali.

Hii imekaaje wakuu. Maana hawa ndugu wanapambana kupata fedha ya matibabu halafu tena sadaka?!

Tujadili bila kashfa wala matusi. Ni kwa hoja tu
Sadaka ya nadhiri ina nguvu sana ikitolewa kwa imani na upendo kwa Mungu. Ilimpa Hanna mtoto.
 
Mkuu swala la imani lazima liambatane na sadaka. Bila sadaka na mambo mengine utachelewa sana.
Nakupatia mfano mdogo tu. Kwa shetani yan mganga ukiwa unaumwa waweza ambiwa mpeleke kuku mqwkundu au mweupe wa dawa. Kwa gharama ya haraka haraka ni tshs 10 000 kuku mmoja. Na kweli ukipeleka shida yako inaisha ila ukisema huna basi shida yako inabaki pale pale.
Swala la sadaka liko hivi, hakuna kitu kikubwa kama funga na sadaka kiimani. Tatizo la watu wengi tunamtolea Mungu kidogo sana ilihali sehemu nyingine tunapeleka kikubwa. Kwa mganga umepeleka kuku kwa Mungu si ndo ungepaswa upeleke mbuzi kabisaaa? Lakini kwa Mungu tunapeleka buku. Kwa mfumo huu tunajikwamisha sana katika maisha yetu. Sadaka inanguvu ya ajabu kama umesimama kiimani na ukatimiza yale yakupasayo.

Funga+maombi+sadaka+shukrani=miujiza mikuu juu ya mwombaji.
Tusimtolee Mungu chenchi na tutoe kwa mioyo yetu na si kwa kushurutishwa na mtu.
 
Kwa kweli,mamkubwa wangu aliumwa vichomi alikwenda kwa mganga...mganga akamwambia kunywa mkojo wako utapona...akakojoa kwenye kopo akanywa...nadhani imani ndo ilimponya
Waga ni dawa, nje na imani ukigugo 'urine therapy' utashangaa
 
Kun mmoja alitoa uz humu akasema mchungaji kila waikutana anakumbushua sadaka 😂😂
Mtu anaelalamika kuhusu sadaka bado hana ufahamu na sadaka. Kwa shetani kqwnyewe wanatoa sadaka tena qao sadaka zao si za kitoto. Wanatoa mtu. Mara unaona mtu anamiliki ndegee
 
Kutoa sadaka ni jambo jema sana lakini jambo la kujiuliza.
Mchungaji amesomea udaktari? Jee Anafanya upimaji na kujua tatizo la muumini wake kwa kutumia njia gani hata akaona sadaka itamponya?.
 
Back
Top Bottom