Mh. Hamad Rashid: Maeneo yanayopotoshwa ambayo yaeelezwa vyema ndani ya Katiba Inayopendekezwa .

Mh. Hamad Rashid: Maeneo yanayopotoshwa ambayo yaeelezwa vyema ndani ya Katiba Inayopendekezwa .

nyimbag

Member
Joined
Feb 28, 2015
Posts
41
Reaction score
17
Mh. Hamad Rashid: Maeneo yanayopotoshwa ambayo yaeelezwa vyema ndani ya Katiba Inayopendekezwa .
a. Zanzibar Kukopa

Zanzibar kwa muda mrefu imekuwa ikitafuta misaada na mikopo kupitia Tanzania Bara ila kwa Katiba Inayopendekezwa inatoa fursa kwa Zanzibar kukopa, kutafuta misaada na kujiunga na Jumuiya yoyote duniani ili mradi inafuata taratibu na sheria zitazowekwa na Baraza la wawakilishi na traratibu zitakapokamilika kama serikali ya mapinduzi ya Zanzibar imeshindwa dhamana basi serikali ya jamhuri ya muungano lazima itoe dhamana, hivyo wanaopotosha na kusema tumechelewa kufanya hivyo wamekosa hoja na wana lenga kuleta mgongano na uvunjifu wa amani kwa kupandikiza chuki miongoni mwa watanzania.

b. wananchi kumwajibisha mbunge
Akizungumzia kuhusu suala la wananchi kupokwa haki ya kuwajibisha mbunge Mh. Hamad alisema kuwa hakuna sehemu yoyote duniani wanaotekeleza suala hilo hata Marekani ni majimbo Kumi na Tatu (13) tu kati ya 50 ndiyo yanatekeleza suala hilo, hivyo haina mashiko kutumia hoja hiyo kuipinga Katiba Inayopendekezwa.

c. Mafuta na Gesi
Mh. Hamad alisema kuwa suala la mafuta na gesi kwenye Katiba Inayopendekezwa inasema kuwa Mafuta au gesi inayopatikana Zanzibar ni mali ya Zanzibar vivyo hivyo kwa upande wa Bara suala ambalo halikuwa limewekwa kwenye Katiba ya mwaka 1977, lakini Katiba ya sasa hivyo hii inatoa fursa kwa Zanzibar kujiendeleza kupitia rasilimali hii iwapo itagundulika kwa upande wa Zanzibar.
Pia Katiba hii ibara ya 23 inasema kuwa ardhi ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa madhumuni na matumizi ya watanzania lakini bunge na Baraza la wawakilishi watapitisha sheria kwa matumizi wa Ardhi hiyo hivyo kuwapa fursa wazanzibar kumiliki ardhi kwa upande wa Bara mana ni watanzania hivyo wanaopotosha hawawatakii mema wazanzibar.
:nod:
 
Halafu haya mabandiko ya katiba ya vijisenti yamekuwa mengi hapa jukwaani kuliko hata nakala zilizochapwa na kusambazwa kwa wananchi ili wajisomee.
 
nyimbag,

..Hamad Rashid kafukia-fukia mambo mengi sana.

..amezungumza mambo mengi kuhusu Znz, bila kuelekeza mambo ya Tanganyika yatashughulikiwa vipi.

..kitu cha msingi ni kwamba Watanganyika nao watambuliwe, waenziwe, na walindwe ktk muungano, kama inavyofanyika kwa ndugu zao wa Zanzibar.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom