Mh. Shibuda, Nataka serikali mbili

Mh. Shibuda, Nataka serikali mbili

tpmazembe

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
2,469
Reaction score
586
MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, John Shibuda amesema msimamo wake ni kuwapo kwa Serikali mbili, huku akisisitiza kuwa ilipaswa wajumbe wa bunge hilo wapewe elimu ya ufahamu ya kazi yao.

Akizungumza katika viwanja vya Bunge jana, Shibuda ambaye ni Mbunge wa Maswa Magharibi kwa tiketi ya Chadema, alisema hata kama itamlazimu kufukuzwa katika chama, msimamo wake ni muundo wa Serikali mbili.

Msimamo wa Chadema katika muundo wa Serikali ni kuwapo kwa Serikali tatu, muundo ambao pia umependekezwa katika Rasimu ya mwisho ya Katiba, iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ambayo itawasilishwa katika Bunge hilo.

Wakati Chadema ikijinadi kwa mfumo huo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinataka kuwapo kwa mfumo wa Serikali mbili, na wajumbe wake ndani ya Bunge wataeleza kwa nini kinataka mfumo huo.

"Ndio nataka mfumo wa Serikali mbili. Wale Wasukuma wangu, wafugaji na wavuvi wangu nitawaeleza nini.Mimi nimetumwa na watu, na nitasimamia mfumo huo," alisema Shibuda.

Alisema kumekuwapo na uhusiano wa karibu kati ya watu wa Tanzania Bara na Zanzibar kwa miaka 50, wakiwamo Wasukuma, ambao alisema wapo Visiwani na Bara, na wamekuwa pamoja kwa miaka yote hiyo.

"Kuna makabila zaidi ya 130 hapa. Yana uhusiano wa moja kwa moja, wakiwamo Wasukuma ambao ni asilimia 30 ya Wazanzibari. Sasa hawa niseme siwataki," aliongeza Shibuda.

Aliwafananisha wanaokataa Serikali mbili sawa na mtoto anayemkataa babu yake, kwani ni sawa na kuikana historia yake.

"Kuna watu hawajui hata historia ya Tanzania. Hawajui historia ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar. Hawajui Tanganyika ilipataje uhuru. Hawajui Zanzibar ilivyopata Uhuru wake. Kuna sintofahamu kubwa," alisema Shibuda na kupendekeza kwanza wajumbe wangepitishwa kufahamu historia ya nchi.

Alisema uanaharakati na uprofesa ni vitu tofauti linapokuja suala la historia ya nchi, hivyo kwa sababu ya kuwa na wajumbe wa aina mbalimbali katika Bunge hilo, kulipaswa kuwa na uelimishwaji kabla.

"Hata kama Rasimu ya Kanuni itakuwa nzuri, haisaidii kitu. Kuna sintofahamu ya uelewa kwa wajumbe, hivyo hili lilipaswa kwanza tuelimishane," aliongeza mwanasiasa huyo machachari.

Bunge Maalumu la Katiba halijaanza mijadala yake likisubiri kukamilika kwa Kanuni ambazo kuanzia leo kwa siku mbili, wajumbe watajadili Rasimu ya Kanuni. Baada ya kuridhiwa kwa Kanuni hizo, ndipo utafuata uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti na baadaye viapo kwa wajumbe, kabla ya ufunguzi rasmi wa Bunge hilo lenye wajumbe 629.

Ufunguzi utafuatiwa na kuwasilishwa kwa Rasimu ya Katiba, na ndipo mjadala sasa utaanza wa kuichambua Rasimu hiyo, huku eneo la mfumo wa Serikali likitarajiwa kuwa na mjadala mkali. Katika hatua nyingine, wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ambao ni wabunge wa CCM, walikuwa na kikao jana kuanzia saa moja usiku.

Inaelezwa kuwa kikao hicho kilikuwa mahsusi kwa ajili ya kuweka msimamo katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge, ambao makada wao wawili, Samuel Sitta na Andrew Chenge wanaaminika kukitaka kiti hicho.

Source: Habari Leo
 
shibuda anasema 30% ya wazanzibar ni wasukuma. mimi nampinga nasema wazanzibar wengi wenye asili ya bara ni wanyamwezi na wamakonde
 
Du! Mawazo ya Ki-CCM hayo. Huyu ni lazima atakuwa balozi wa CCM ndani ya Chadema.
 
Shibuda anasema sababu kubwa ya kutaka serikali 2 ni kwa vile kabila la wasukuma limeenea zanzibar na tanganyika. s

Sasa kama hiyo ndio sababu basi tuungane na kenya maana wamasai , wachaga, na wajaluo wako wengi sana kenya tufanye nao muungano wa serikali 2. Pia tuungane na msumbuji maana wamakonde ndio kabila kuu msumbuji na tufanye serikali 2. Pia tuungane na uganda maana wahaya wako wengi uganda.pia tuungane na rwanda na kongo maana nao wako wengi tu watusi haa nchini. iweje iwe kwa zanzibar pekee
 
Ni maoni yake inabidi yaeshimiwe na haya niyakwangu Huyu tushamzoea ni walewale tu kama vile vidonge vya langi mbili.
 
Lazima afuate msimamo wa chama chake - hakuna cha ajabu hapo!!
 
MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, John Shibuda amesema msimamo wake ni kuwapo kwa Serikali mbili, huku akisisitiza kuwa ilipaswa wajumbe wa bunge hilo wapewe elimu ya ufahamu ya kazi yao.

Akizungumza katika viwanja vya Bunge jana, Shibuda ambaye ni Mbunge wa Maswa Magharibi kwa tiketi ya Chadema, alisema hata kama itamlazimu kufukuzwa katika chama, msimamo wake ni muundo wa Serikali mbili.

Msimamo wa Chadema katika muundo wa Serikali ni kuwapo kwa Serikali tatu, muundo ambao pia umependekezwa katika Rasimu ya mwisho ya Katiba, iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ambayo itawasilishwa katika Bunge hilo.

Wakati Chadema ikijinadi kwa mfumo huo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinataka kuwapo kwa mfumo wa Serikali mbili, na wajumbe wake ndani ya Bunge wataeleza kwa nini kinataka mfumo huo.

“Ndio nataka mfumo wa Serikali mbili. Wale Wasukuma wangu, wafugaji na wavuvi wangu nitawaeleza nini.Mimi nimetumwa na watu, na nitasimamia mfumo huo,” alisema Shibuda.

Alisema kumekuwapo na uhusiano wa karibu kati ya watu wa Tanzania Bara na Zanzibar kwa miaka 50, wakiwamo Wasukuma, ambao alisema wapo Visiwani na Bara, na wamekuwa pamoja kwa miaka yote hiyo.

“Kuna makabila zaidi ya 130 hapa. Yana uhusiano wa moja kwa moja, wakiwamo Wasukuma ambao ni asilimia 30 ya Wazanzibari. Sasa hawa niseme siwataki,” aliongeza Shibuda.

Aliwafananisha wanaokataa Serikali mbili sawa na mtoto anayemkataa babu yake, kwani ni sawa na kuikana historia yake.

“Kuna watu hawajui hata historia ya Tanzania. Hawajui historia ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar. Hawajui Tanganyika ilipataje uhuru. Hawajui Zanzibar ilivyopata Uhuru wake. Kuna sintofahamu kubwa,” alisema Shibuda na kupendekeza kwanza wajumbe wangepitishwa kufahamu historia ya nchi.

Alisema uanaharakati na uprofesa ni vitu tofauti linapokuja suala la historia ya nchi, hivyo kwa sababu ya kuwa na wajumbe wa aina mbalimbali katika Bunge hilo, kulipaswa kuwa na uelimishwaji kabla.

“Hata kama Rasimu ya Kanuni itakuwa nzuri, haisaidii kitu. Kuna sintofahamu ya uelewa kwa wajumbe, hivyo hili lilipaswa kwanza tuelimishane,” aliongeza mwanasiasa huyo machachari.

Bunge Maalumu la Katiba halijaanza mijadala yake likisubiri kukamilika kwa Kanuni ambazo kuanzia leo kwa siku mbili, wajumbe watajadili Rasimu ya Kanuni. Baada ya kuridhiwa kwa Kanuni hizo, ndipo utafuata uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti na baadaye viapo kwa wajumbe, kabla ya ufunguzi rasmi wa Bunge hilo lenye wajumbe 629.

Ufunguzi utafuatiwa na kuwasilishwa kwa Rasimu ya Katiba, na ndipo mjadala sasa utaanza wa kuichambua Rasimu hiyo, huku eneo la mfumo wa Serikali likitarajiwa kuwa na mjadala mkali. Katika hatua nyingine, wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ambao ni wabunge wa CCM, walikuwa na kikao jana kuanzia saa moja usiku.

Inaelezwa kuwa kikao hicho kilikuwa mahsusi kwa ajili ya kuweka msimamo katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge, ambao makada wao wawili, Samuel Sitta na Andrew Chenge wanaaminika kukitaka kiti hicho.

Source: Habari Leo
hizo serikali mbili anazozitaka shibuda moja ni ya nchi gani na nyingine ya nchi gani, na kama jibu ni moja ya zanzibar ya nyingine ya ya zanzibar na tanganyika,anaweza kutueleza kwa nini nchi moja ya zanzibar iwe na serikali mbili?
 
Shibuda ni mbunge wa ccm kupitia chadema! Kama chadema watafanya kosa kumpitisha kugombea ubunge mwaka 2015 kupitia chadema watafanya kosa kubwa!
 
Popo ni kiumbe cha ajabu sana...........

Giant_Bat_1_(FFXI).png
 
sio balozi wa ccm usiwe na mawazo finyu amesema hali halisi
Hali halisi ya kwamba wapuuzie kero mama ya muungano ambayo ni serikali mbili? Serikali mbili haitadumisha huu muungano labda moja au tatu. Wakiacha serikali mbili wajiandae kuendelea kukabiliana na kero zaidi za muungano. Nakwambia ukweli kama huamini Mark my words.
 
Badala ya kumtimua huyu mamluki.....mnatimua watu wenye damu na CDM
 
Chadema mmekuwa na Misimamo ya kuilaumu CCM kwa kutoa Msimamo wa Chama, iweje nyie mpinge wa Shibuda halafu mseme kama Chama hamna msimamo? je angesema anataka serikal 3 mngempinga?
 
Back
Top Bottom