Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa(SEKOMU) alishwa madawa ya kulevya, aibiwa kila kitu

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,587
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU), Mchungaji Dk Msafiri Mbilu amelazwa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Tanga ya Bombo akiwa mahututi baada ya kula keki inayohofiwa kuwa ilikuwa na dawa za kulevya.

Dk Mbilu amepatwa na mkasa huo wakati akiwa kwenye basi akitokea Jijini Dar es salaam kuelekea Tanga.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba ni kuwa mchungaji huyo amebainika kupoteza fahamu baada ya basi hilo kuwasili jijini Tanga na kushindwa kushuka.

Nitawaletea updates
 
Hata kama watz ni wakarimu sili kitu cha mtu kwenye basi wala simkaribishi mtu kitu changu, kila mtu ale vyake
 
Reactions: rr4
ameshaonjeshwa poda
manana kuna ka-maith fulani hivi kuwa ukitest huwezi acha
 
Hiko chuo kina umri gani? Ndio kwanza nakisikia (msinilaumu kwa umbumbu wangu)

Pole mhadhiri
 
Hiko chuo kina umri gani? Ndio kwanza nakisikia (msinilaumu kwa umbumbu wangu)

Pole mhadhiri
Ninaamini kuna vyuo vingi huvifahamu Tanzania ikiwemo vya serikali. Hiki nadhani hakikosi miaka 8
 
Labda wanipulizie dawa ila kwenye basi huwa sili kitu kutoka kwa mtu yeyote yule.
 
nilitamani kukoment lakini nisije kusaidia polis bure ngoja niwaachie wenyewe
 
Unakulaje chakula cha mtu usiyemfahamu!?

Any way, kwa wahadhiri inawezekana mana mtu atakudanganya kuwa ni mwanafunzi wake.

Waambie waachie ajira na hela zije mitaani maana vijana watatenda vitu visivyo.

Japo, hali ngumu ya maisha inakuwa siyo kigezo cha mtu kumfanyia mtu unyama wa kiasi hicho cha kumlisha dawa za aina hiyo.
 
Hiko chuo kina umri gani? Ndio kwanza nakisikia (msinilaumu kwa umbumbu wangu)

Pole mhadhiri
Hicho chuo kimetokana na dhambi ya kiongozi mmoja kutumiwa vibaya na dhehebu lake fulani akaamua kuwarudishia shule zao zilizokuwa zimetaifishwa na Nyerere kuwa za umma. Kwaaibu ilimbidi arudishe hata zile za madhehebu mengine, hivyo ikazaliwa SEKOMU kutoka Magamba Secondary School hukoooo Ushoto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…