Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU), Mchungaji Dk Msafiri Mbilu amelazwa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Tanga ya Bombo akiwa mahututi baada ya kula keki inayohofiwa kuwa ilikuwa na dawa za kulevya.
Dk Mbilu amepatwa na mkasa huo wakati akiwa kwenye basi akitokea Jijini Dar es salaam kuelekea Tanga.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba ni kuwa mchungaji huyo amebainika kupoteza fahamu baada ya basi hilo kuwasili jijini Tanga na kushindwa kushuka.
Nitawaletea updates