Pre GE2025 Mhandisi James Jumbe Wiswa, amechangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga

Pre GE2025 Mhandisi James Jumbe Wiswa, amechangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mjini, Mhandisi James Jumbe Wiswa, amechangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga.

Mhandisi Jumbe amekabidhi mifuko hiyo ya saruji wakati wa ziara ya Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambapo wamekagua maendeleo katika Kituo cha Afya Kambarage na ujenzi wa barabara ya Kenyatta-Karena kwenye kata hiyo.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya mifuko ya saruji, Mhandisi Jumbe amesema, “Nimeamua kutimiza ahadi yangu kutoa mifuko hii ya saruji ili kuimarisha ulinzi katika Kituo cha Afya Kambarage. Kamati ya Kituo hiki iliniletea ombi la kuchangia ujenzi wa uzio na mimi nimelijibu kwa vitendo. Kituo hiki kipo kwa ajili ya wagonjwa mbalimbali na wengi ni akina mama na watoto, na tunahitaji kuwalinda kwa kila hali.”
 
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mjini, Mhandisi James Jumbe Wiswa, amechangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga.

Mhandisi Jumbe amekabidhi mifuko hiyo ya saruji wakati wa ziara ya Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambapo wamekagua maendeleo katika Kituo cha Afya Kambarage na ujenzi wa barabara ya Kenyatta-Karena kwenye kata hiyo.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya mifuko ya saruji, Mhandisi Jumbe amesema, “Nimeamua kutimiza ahadi yangu kutoa mifuko hii ya saruji ili kuimarisha ulinzi katika Kituo cha Afya Kambarage. Kamati ya Kituo hiki iliniletea ombi la kuchangia ujenzi wa uzio na mimi nimelijibu kwa vitendo. Kituo hiki kipo kwa ajili ya wagonjwa mbalimbali na wengi ni akina mama na watoto, na tunahitaji kuwalinda kwa kila hali.”
Ni hela kidogo sana, haifiki hata 2m mifuko yote hiyo.
 
Anataka ubunge
Ndio wenda anataka , kituo cha kambarage nakifaham vizuri badala achangie hospital ya mkoa ambayo ipo namapungufu kibao huko Mwawaza anachangia kituo cha afya Kambarage ? Aakili hana uyu.

Hospital ya mkoa mpya kule Mwawaza pamoja na upya wake bado ipo na mapungufu sana ,watumishi wamebanana kama kunguni , idara hazijakamilika, japo Mganga mfawidhi ( dr Mzila) na timu yake wanajitahidi ila bado ,wapo Ct scan n.k mpaka implant ya O2 lakini bado katika odi za wagonjwa , vyumba bora vya upasuji n.k , wapo na vifaa bora sana tu .

Sasa huyu mjinga anawekeza kituo cha afya Kambarage yupo na akili kweli
 
Back
Top Bottom