Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,984
Watu wanafika hospitali, wanapiga picha wapendwa wao na watu wengine wanowazunguka bila ridhaa ya wale waliopigwa picha, hii si sawa.
Madaktari wapo kazini, baadhi ya wahudumu wa afya wasio na maadili wanarekodi video na kupiga picha kwa maelekezo ya ndugu wa mgonjwa au utashi wao tu..hii si sawa.
Waandishi wa habari wanakwenda maeneo ya kutolea huduma wanakuta wagonjwa wamelala au wapo foleni then wanarusha bila hata kuwaomba ruhusa wagonjwa husika ..hii si sawa.
Tupige marufuku huu utaratibu, tuweke sheria ya kushtaki mtu atakarekodi video na kuisambaza bila ridhaa ya wahusika, Jamhuri imejilinda kisheria, wagonjwa nao Wapewe nguvu ya kujilinda kisheria.
Watu waliopo hospitalini walindwe, tusiwadhalilishe. Mwisho sipendezwi na haya matangazo yanayoendelea kuhusu kipimo kipya cha COVID, yanaondoa utu na ni kinyume kabisa na maadili....picha za uchi za watu wakiwa wamelela kifudifudi wakisubiri kupimwa COVID zipigwe marufuku.
Madaktari wapo kazini, baadhi ya wahudumu wa afya wasio na maadili wanarekodi video na kupiga picha kwa maelekezo ya ndugu wa mgonjwa au utashi wao tu..hii si sawa.
Waandishi wa habari wanakwenda maeneo ya kutolea huduma wanakuta wagonjwa wamelala au wapo foleni then wanarusha bila hata kuwaomba ruhusa wagonjwa husika ..hii si sawa.
Tupige marufuku huu utaratibu, tuweke sheria ya kushtaki mtu atakarekodi video na kuisambaza bila ridhaa ya wahusika, Jamhuri imejilinda kisheria, wagonjwa nao Wapewe nguvu ya kujilinda kisheria.
Watu waliopo hospitalini walindwe, tusiwadhalilishe. Mwisho sipendezwi na haya matangazo yanayoendelea kuhusu kipimo kipya cha COVID, yanaondoa utu na ni kinyume kabisa na maadili....picha za uchi za watu wakiwa wamelela kifudifudi wakisubiri kupimwa COVID zipigwe marufuku.