Mheshimiwa Rais na Waheshimiwa Wabunge Wetu Tunaomba........

Sabi Sanda

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
409
Reaction score
31
Mheshimiwa Rais na Wabunge Wetu,

Tunaomba kuanzia mwaka ujao wa fedha 2014/2015 Serikali iongeze kiwango cha Ruzuku kwa kila mwanafunzi wa shule za Msingi na za Sekondari za umma kwa ajili ya uendeshaji wa shule zetu za msingi na sekondari.

Kwa upande wa shule za msingi kiwango kipya cha Ruzuku kinachopendekezwa kwa kila mwanafunzi kwa mwaka ni shilingi elfu 25. Na kwa upande wa Sekondari kiwango kipya cha Ruzuku kinachopendekezwa ni shilingi elfu 75 kwa mwaka kwa kila mwanafunzi.

Pia Mheshimiwa Rais tunaomba fedha hizi za Ruzuku ziwe zinatumwa moja kwa moja kwenye akaunti za shule bila kupitia TAMISEMI NA HALMASHAURI ZETU.

Ni mimi,

Josephat S. Sanda

Kerege
Bagamoyo
0654 467758
 
Na nyie hesabu mnapeleka wapi kwa ukaguzi????!!!!
 
Mh na utaratibu wachakula kwa shule za bweni uangaliwe pia.

Wakati niko Advance Tuliambiwa makadirio ya chakula kwa kila mwanafunzi wa bweni wa serikali ni sh 1500/= kwa siku. Hapo nikatambua kwa nini tunalishwa bora chakula.

Halafu na ule mchezo wa wazabuni ufutwe!! Inawezekana siuelewi zaidi ila unaleta usumbufu na kuinyonya serikali kwa bei zao.!
 
Na nyie hesabu mnapeleka wapi kwa ukaguzi????!!!!

Katika hili kazi ya TAMISEMI na Halmashauri inatakiwa iwe ni kuhakikisha matumizi mazuri ya fedha za ruzuku baada ya kupokea taarifa toka Hazina. Wakuu wa Shule hulepeleka taarifa zao Halmashauri kila robo mwaka.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…