Mhitimu wa Chuo Kikuu afungua kesi dhidi ya Bodi ya mikopo akidai tozo zinachelewesha maendeleo ya Wahitimu

Mhitimu wa Chuo Kikuu afungua kesi dhidi ya Bodi ya mikopo akidai tozo zinachelewesha maendeleo ya Wahitimu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira Arusha, Alexanda Bakunguza, amefungua kesi Mahakama Kuu dhidi ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali akipinga elimu ya juu kugharamiwa na serikali kwa njia ya mikopo.

Katika kesi hiyo namba 16 ya mwaka 2021, mhitimu huyo anatetewa na mawakili watatu kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ambao ni Mpale Mpoki, Steven Mwakibolwa na Amani Jowachim.

Kesi hiyo iko chini ya majaji watatu wa Mahakama Kuu ambao ni Jaji Victoria Makani, Jaji Benihaj Masoud na Jaji Opiyo.

Mhitimu huyo anadai hoja yake ya msingi ni kwamba tozo na riba katika mikopo wanayopewa wanafunzi wa elimu ya juu inamchelewesha mwanafunzi kupata maendeleo japokuwa ameshaelimika.

Kufuatia hali hiyo, anadai elimu ya juu igharamiwe na serikali kuanzia mwanzo wa masomo hadi mwisho bila mwanafunzi kulipishwa gharama yoyote.

Msingi wa madai hayo unatokea kwenye Ibara ya 11 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inaeleza kuwa serikali itafanya jitihada kuhakikisha watu wote wanapata fursa sawa na za kutosha kuwawezesha kupata elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo vinginevyo vya mafunzo.

Hata hivyo, kesi hiyo imewekewa mapingamizi matatu na serikali ikisema haina mashiko hivyo ifutwe.

Kesi hiyo ilifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Julai 29, mwaka huu na jana ilitarajiwa kutolewa uamuzi juu ya mapingamizi yaliyowekwa na serikali.

Ippmedia
 
Basic salary ya mtu unakuta ni 400k. Heslb wachukue 15%, Paye wakate 8%, NSSF akatwe 10%. Hapo hapo atoe kodi ya pango na chakula. Hiyo hiyo atume kwa wazazi kijijini na ada za serikali alipe. Gesi imepanda. Mafuta ya kupika yamepanda. Hii nchi tunaongozwa na viongozi “wajinga”
 
kashaonesha udhaif sana bora 2025 iwai kufika tuingie kwenye uchaguzi
Jiandae kisaikolojia tu, bado yupo sana, mpaka 2030, mambo ya kutawaliwa kinyapara na kifalme yameenda na mwendazake! Hutaki kuishi kwenye mfumo huu mpya basi nenda Burundi (According to Mwigulu)
 
Hawajamuita wampime mkojo tu hadi sasa, au kuulizwa juu ya uraia wake maana ndio akili zao zilikoishia hawana tena akili, ikishindikana wamuite Gaidi tu, masikini Tanzania
 
Yupo sahihi. Nchi ya Tanzania imekuwa na wabunge wa ovyo ambao wanaunda miswada ya kukandamiza masikini. Yaani mtu anakatwa kodi mpaka anadidimia katika umasikini.

Kutwa wanasiasa wanaimba uzalendo na kisha kuleta makato, kodi, ushuru na tozo chungu nzima kwa watanzania masikini.
 
Yupo sahihi. Nchi ya Tanzania imekuwa na wabunge wa ovyo ambao wanaunda miswada ya kukandamiza masikini. Yaani mtu anakatwa kodi mpaka anadidimia katika umasikini.

Kutwa wanasiasa wanaimba uzalendo na kisha kuleta makato, kodi, ushuru na tozo chungu nzima kwa watanzania masikini.
Bado kuna karatasi inapita ya mchango wa mwenge
Am sorry my boss kwa hili utanisamehe tu siwezi kutoa hata Mia kwaajili ya mwenge
 
L
Jiandae kisaikolojia tu, bado yupo sana, mpaka 2030, mambo ya kutawaliwa kinyapara na kifalme yameenda na mwendazake! Hutaki kuishi kwenye mfumo huu mpya basi nenda Burundi (According to Mwigulu)
Lakini pi hatutaki kutawaliwa na utawala wenye kurembua macho tu!
 
Kama ndio hoja yake hiyo Mwamba ataangukia pua mapema sana. Maendeleo ya mtu hayana uhusiano sana na elimu ya darasani japo tunategemea msomi apate maendeleo kwa kasi baada ya kuelimika namnabya kutumia fursa zilizopo na sio kwa kutokurudisha fedha za bodi ambazo uliomba na kuingia makubaliano na bodi.

Anyway jaribio zuri ila mkakati wake ndio una mashaka.
 
Bwana alezanda Bakunguza safi Sana tuma account namba yako ya benki nami nikugharamie gharama za usafiri, chakula na maradhi unapokuwa mahakamani make huyu mtunga sera syo haiwezekani Kila mwaka riba ya 6% Mfano ulitumia million 12 asilimia 6 Kila mwaka Mfano ukae bila ajira au biashara yoyote ambayo haijaorodheshwa Kama tax payer itafika zaidi ya million 19,200,000 sasa jiulize Hilo Deni litakuwa mzigo mkubwa siku ukianza kulipa ,, hii ndyo maana wanufaika wanaumia Sana na huu mzigo.
 
Back
Top Bottom