Miaka 10 iliyopita iPhone 6 ilitoka na ya bei ya juu kabisa ilikua $499, mwaka huu iPhone 16 imetoka bei ya juu kabisa ni $1,599

Miaka 10 iliyopita iPhone 6 ilitoka na ya bei ya juu kabisa ilikua $499, mwaka huu iPhone 16 imetoka bei ya juu kabisa ni $1,599

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Wazee wa JF.

Nakumbuka 2014 September, Tim Cook alipanda stejini na kutangaza simu mpya mbili, iPhone 6 na iPhone 6 Plus.

IMG_0291.jpeg


iPhone 6 ilianzia $199 kwa 16 GB na 6 Plus ilianzia $299 kwa 16 GB.

Bei ya juu kabisa ya 6 Plus ilikua ni $499 yenye 128 GB.

Mwaka huu, September yule yule CEO wa Apple katutangazia iPhone nne, iPhone 16, 16 Plus, 16 Pro, na 16 Pro Max.

IMG_0292.jpeg


iPhone 16 ya GB 128 ndio ya bei ya chini kabisa $799 na iPhone ya bei ghali ni iPhone 16 Pro Max ya 1 TB kwa $1,599 tu!

Sijui hizi bei zinaendaje, mfano miaka 10 ijayo.

Ngoja nitafute hela.
 
Ndo maana kwenye mabenki, Unaambiwa riba Yao Ni 25%

Ila ukikopeshwa bil 10, baada ya miaka 10 utatakiwa kuwarejeshea benki almost bil. 30.

Yaani Riba Ni Almost 3 times ya ulichokopeshwa
 
iPhone 6 Plus iliuzwa kwa bei ya $499 ikiwa tu mnunuzi ataingia mkataba wa miaka 2 na mtandao wa simu husika. Bei yake bila contract ilikuwa ni:
  • iPhone 6 (16GB): $649
  • iPhone 6 (64GB): $749
  • iPhone 6 (128GB): $849
  • iPhone 6 Plus (16GB): $749
  • iPhone 6 Plus (64GB): $849
  • iPhone 6 Plus (128GB): $949
Ninakumbuka kabisa mwaka huo ninatafuta simu ya kununua, ingekuwa $199 wote tungekuwa na iPhone; kwa kuwa kipindi hiko USD 1 ilikuwa kama 1600 Tshs hivyo hiyo iPhone ingekuwa inauzwa kwa 320,000.
 
Back
Top Bottom