Miaka 10 iliyopita iPhone 6 ilitoka na ya bei ya juu kabisa ilikua $499, mwaka huu iPhone 16 imetoka bei ya juu kabisa ni $1,599

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Wazee wa JF.

Nakumbuka 2014 September, Tim Cook alipanda stejini na kutangaza simu mpya mbili, iPhone 6 na iPhone 6 Plus.



iPhone 6 ilianzia $199 kwa 16 GB na 6 Plus ilianzia $299 kwa 16 GB.

Bei ya juu kabisa ya 6 Plus ilikua ni $499 yenye 128 GB.

Mwaka huu, September yule yule CEO wa Apple katutangazia iPhone nne, iPhone 16, 16 Plus, 16 Pro, na 16 Pro Max.



iPhone 16 ya GB 128 ndio ya bei ya chini kabisa $799 na iPhone ya bei ghali ni iPhone 16 Pro Max ya 1 TB kwa $1,599 tu!

Sijui hizi bei zinaendaje, mfano miaka 10 ijayo.

Ngoja nitafute hela.
 
Ndo maana kwenye mabenki, Unaambiwa riba Yao Ni 25%

Ila ukikopeshwa bil 10, baada ya miaka 10 utatakiwa kuwarejeshea benki almost bil. 30.

Yaani Riba Ni Almost 3 times ya ulichokopeshwa
 
iPhone 6 Plus iliuzwa kwa bei ya $499 ikiwa tu mnunuzi ataingia mkataba wa miaka 2 na mtandao wa simu husika. Bei yake bila contract ilikuwa ni:
  • iPhone 6 (16GB): $649
  • iPhone 6 (64GB): $749
  • iPhone 6 (128GB): $849
  • iPhone 6 Plus (16GB): $749
  • iPhone 6 Plus (64GB): $849
  • iPhone 6 Plus (128GB): $949
Ninakumbuka kabisa mwaka huo ninatafuta simu ya kununua, ingekuwa $199 wote tungekuwa na iPhone; kwa kuwa kipindi hiko USD 1 ilikuwa kama 1600 Tshs hivyo hiyo iPhone ingekuwa inauzwa kwa 320,000.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…