Miaka 150 mpaka 200 ijayo, lugha zetu za asili nyingi zitakuwa zimetoweka

Miaka 150 mpaka 200 ijayo, lugha zetu za asili nyingi zitakuwa zimetoweka

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Ukichunguza kwa makini utagundua moja ya athari ya watu kuhamia mijini kutoka vijijini ni vijana wengi kuzaliwa na kukulia mijini kias kwamba wengi hawapati fursa ya kujifunza lugha zao za asili kama ilivyo kwa wale wanaozaliwa vijijini waliko wazee.

Wazazi wengi huku mijini wanaacha ule utamaduni wa kuwaongelesha kilugha watoto wao tangu utotoni na badala yake wanakuwa wakijifunza kiswahili na wengine kingereza kwa wale wanaosoma shule hizi za kisasa.

Baadhi ya watoto hawa wengine hata kiswahili hawakijui bali wanajua zaidi kingereza kutokana na muda wote kuongea kingereza shuleni, na hata wakirudi nyumbani ni ndani ya mageti huku wakiongea kingereza na wazazi wao.

Sasa hawa watoto lugha zetu za asili (makabila) ndio kabisa hawataka wayajue kwani hata salamu tu ni mtihani.

Siku hizi hata ule utamaduni wa kuwapeleka watoto vijijini kwa babu na bibi zao haupo acha ule wa kuacha watoto kulelewa na babu/bibi, utamaduni uliosaidia watoto kujifunza lugha za makabila yao kwa kuongea kilugha na babu,bibi, wajomba, mashangazi na ndugu na jamaa wengine waliko vijijini.

Ukichunguza utagundua hali hii ilianza kujitokeza kidogo kidogo kwa wale waliozaliwa miaka ya 70 na kuendelea watu walipoanza kuishi katika nyumba (kota) za serikali, watu kuhamia na kujenga mijini kutoka vijijini.

Kwahiyo, katika kipindi hiki cha miaka 50, utagundua hali hii inazidi kuongezeka na hivyo ndani ya miaka 150 mpaka 200 ijayo, idadi ya watu wasiojua lugha zao za asili inaweza kuongezeka mara tatu mpaka mara nne ya hali ilivyo sasa na kuziweka lugha zetu za asili katika hatari ya kuanza kutoweka kabisa na tukabaki na kiswahili na kingereza.

Mwisho, kama ambayo leo hii tunalaumu wazungu kwa kudhoofisha mila na desturi zetu, ndivyo hivyo hivyo tutakuja kulaumu wazungu kwa kuua lugha za makabila yetu wakati chanzo ni sisi wenyewe.

Kuna uwezekano identify ya mtu mweusi itabaki kuwa ni rangi yake ya asili na pengine akili yake ikilinganishwa na akili za wenzetu.

Tatizo hili linakwenda na linaoongezeka mithili ya tatizo la climate change linaoongezeka huku jamii ikilipuuza kwasababu tu linaongezeka kidogo kidogo lakini madhara yake teyari yapo na sasa yanaanza kuwa dhahiri .

Mimi kuongelea jambo hili sasa, kutapokelewa mithili ya watu walivyopokea tatizo la climate change katika karne ya 20 wakiona ni kitu ambacho hakipo.

Muda utaongea.
 
Zaidi kwa wanaoishi mijini na wanaona makabila tofauti ndio tabu lkn haimaanishi huko vijijini wataisha.
 
Binafsi sioni faida ya hizo lugha

Japo mwenyewe nilitumia nguvu kubwa sana kujifunza kilugha maana wazee wangu hawakuwa wakiongea na sisi japo wote wanatoka kabila moja
Unaweza kukuta nyumbani kwenu mmeachiwa dawa ya saratani, babu kataja mti kwa jina la lugha yenu ya asili, halafu hakuna mtu anayejua mti huo ni mti gani.

Hapo ndipo utajua faida ya kujua hizi lugha.

Zikifa zinakufa na historia ya kabila nzima watu watashindwa kujua hata walitokea wapi, walipitia wapi, walifikaje hapo walipo.

Wakati sisi tunasema hatuoni umuhimu wa hizi lugha, kuna watafiti wa ughaibuni wanakuja kwetu kufanya tafiti kwenye hizi jamii na lugha zao.

Sikiliza hapa watafiti wanajadili kama chakula cha Wahadzabe kina siri ya kufanya mwili upate afya nzuri zaidi.

Sasa hapo ukipoteza lugha ya hawa Wahadzabe, hata majina ya vyakula muhimu utapoteza.

 
Hiki ulichoandika hapa kinawezekana kama utachukulia mfano wa mijini kama ulivyofanya, lakini nikikumbuka kuna watoto wadogo huko vijijini wasiojua kiswahili napata shaka na hiki ulichoandika kama kinaweza kutokea, hizi lugha za asili ukiangalia vizuri ni kama urithi, kupotea itachukua muda sana, au labda tuseme watu wote wahamie mijini vijiji vibaki tupu.
 
Inaweza kutokea lakini itachukua tena miaka elf mbili lugha za asili kupotea katika jamii zetu, kwa sababu vijiji bado vina watu wanakua na wanazaliana huko huko bila kufika mijini,Lugha inayoendelea huko ni Lugha mama,kwa muktadha huu sioni uwezekano wa lugha za asili zikipotea.
 
Hiki ulichoandika hapa kinawezekana kama utachukulia mfano wa mijini kama ulivyofanya, lakini nikikumbuka kuna watoto wadogo huko vijijini wasiojua kiswahili napata shaka na hiki ulichoandika kama kinaweza kutokea, hizi lugha za asili ukiangalia vizuri ni kama urithi, kupotea itachukua muda sana, au labda tuseme watu wote wahamie mijini vijiji vibaki tupu.
Tunakokwenda idadi ya watu kubaki vijijini itazidi kupungua na badala yake wengi watahamia mijini kutafuta fursa za kimaisha.

Kilimo ndio kingeweza kuwabakiza vijjini ila kilimo chenyewe ndio kinazidi kudorora huku kilimo cha mazao ya biashaara ndio kikiwa hatarini kutoweka kabisa katika nchi yetu kadri miaka inavyoenda.

Miji inapanuka huku vijiji vinamweza na muingiliano wa watu unaongezeka, hivyo ni swala la muda tu haya nisemayo kutokea hata kama itachukua muda mrefu.
 
Mkuu unachosema ni kweli lakini moja ya sababu japo inaweza kuchekesha ni kwamba, unapeleka mwanao kijijini kwa bibi na babu kwenda kusalimia wazee halafu anarudi nyumbani anafikia kuumwa na hata kuvuta waya kabisa.
Swali linabaki je kapigwa kipapai ama mazingira yamemkataa?
Jibu linalotoka hapo linasababisha 'kuban' kabisa ishu za kwenda vijijini kutokana na hizi imani potofu.
 
Tunakokwenda idadi ya watu kubaki vijijini itazidi kupungua na badala yake wengi watahamia mijini kutafuta fursa za kimaisha.

Kilimo ndio kingeweza kuwabakiza vijjini ila kilimo chenyewe ndio kinazidi kudorora huku kilimo cha mazao ya biashaara ndio kikiwa hatarini kutoweka kabisa katika nchi yetu kadri miaka inavyoenda.

Miji inapanuka huku vijiji vinamweza na muingiliano wa watu unaongezeka, hivyo ni swala la muda tu haya nisemayo kutokea hata kama itachukua muda mrefu.
Nionavyo as long as watu wataendelea kizaliana vijijini basi lugha za asili haziwezi kwisha, hao wanaozaliwa watakuta wazazi wao wanazungumza nao watoto watazifahamia kupitia kwa wazazi wao.
 
Mkuu unachosema ni kweli lakini moja ya sababu japo inaweza kuchekesha ni kwamba, unapeleka mwanao kijijini kwa bibi na babu kwenda kusalimia wazee halafu anarudi nyumbani anafikia kuumwa na hata kuvuta waya kabisa.
Swali linabaki je kapigwa kipapai ama mazingira yamemkataa?
Jibu linalotoka hapo linasababisha 'kuban' kabisa ishu za kwenda vijijini kutokana na hizi imani potofu.
 
Ukubwa wa kabila sio hoja, hoja ni nini kinafanyika kuhakikisha idadi ya kizazi cha leo kinaenzi lugha zao.

Ni swala la muda tu.
Sio ukubwa tu, jamaa wanapenda lugha zao labda wakiwa huku mjini na watoto wao wa English medium.
 
Inaweza kutokea lakini itachukua tena miaka elf mbili lugha za asili kupotea katika jamii zetu, kwa sababu vijiji bado vina watu wanakua na wanazaliana huko huko bila kufika mijini,Lugha inayoendelea huko ni Lugha mama,kwa muktadha huu sioni uwezekano wa lugha za asili zikipotea.
Miaka 60 au 70 iliyopita, kuna watu walikuwa hawajui lugha zao za aaili kama ilivyo leo hii?

Inawezekana walikuwepo, lakini idadi yao inaweza kulingana na ya leo?

Sasa hesabu miaka mingine 100 kuanzia leo uone trend itakwendaje na zaidi jiulize tunachukua hatua gani ku-address hali hii.
 
ni ushamba tu wa watanzania nenda makabila ya kinigeria kama igbo,yoruba,hausa njoo kenya kama kikuyu,luo,kalenjin n.k nenda south africa kama zulu,khoxa n.k daima mtoto lazima aijue asili yake kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kuiongea lugha yake ya asili fluently bila kigugumizi chochote na amesoma kweli kweli

hapa tanzania tu hasa kwa makabila ambayo hayajielewi ndio yatapoteza identity pakubwa sana pia baadhi nchi zisizojielewa kweli zitapoteza identity na ndio itakuwa mwanzo wa utumwa wa kiakili na identity nyingine kama kizungu kuziona ndio bora
 
Back
Top Bottom