Miaka 40 shule haijawa na mwl wa kike

NJALI

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2014
Posts
1,534
Reaction score
1,090
Ni jambo la kushangaza sana ndg zangu. Kuna shule moja inaiwa Juma kisiwani, ni shule ya msingi iliyopo kata ya Katunguru Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza. Shule hii licha ya kuwa na uhaba wa walimu pia haija wahi kuwa na mwalimu hata mmoja wa kike tangu ianzishwe 1974. Sijui wadau wa elimu wanalijua hilo au la! Kwa kuwa ajira mpya za walimu hazijatoka ni bora wadau wa elimu mko, wilaya na kata wakaliangalia hili kwa jicho pevu ili wapatikane walimu wa kike wa kupelekwa shule hii.
 
NJALI hii nchi haina kiongozi bora, nenda hata nyakahako kama utapata walimu wa kutosha achilia mbali jinsia
 
Last edited by a moderator:
Naifahamu vizuri sana hiyo shule, kuna shule moja sijui inaitwaje iko pale sengerema mjini karibu na bank ya NMB ina walimu wengi kama utitili more than 50. Serikali haiko makini kwenye mgawanyo wa walimu kati za shule za mjini na zile za pembezoni
 
Kwa pale sengerema mjini si mwenyeji sana, niko huku magulukenda ila hua nafika nyakahako kupitia huku nyamazugo road
 
Ipo shule pale mjini inaitwa Pambaru s/m ina walimu kila aina na kila jinsia. Kwa kweli serikali haizitendei haki baadhi ya shule. Shule yenye walimu saba haiwezi kulingana na yenye 50 hata ki ufanisi wa ufundishaji.
 
Kazi tunayo na mwakani tujiandae kupokea tsheti, kofia, kanga na chumvi kisha tutaabike tena miaka kadhaa ijayo
 
Naifahamu vizuri sana hiyo shule, kuna shule moja sijui inaitwaje iko pale sengerema mjini karibu na bank ya NMB ina walimu wengi kama utitili more than 50. Serikali haiko makini kwenye mgawanyo wa walimu kati za shule za mjini na zile za pembezoni

Kuna shule moja, bahati mbaya sikumbuki jina, iko maeneo ya mpakani mwa Dodoma na Kiteto, ilikuwa na waalimu 2 tu, kwa madarasa ya kwanza mpaka la saba.....Hakuna mwanafunzi aliyewahi kufaulu kwenda sekondari, toka ianzishwe mwaka 1972 (though haishangazi sana kutegemea na idadi ya hao walimu)....kama ametoka mwanafunzi basi ni ndani ya miaka 5 iliyopita....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…