DOKEZO Miaka 45 tangu Majeshi ya Tanzania yashinde vita Uganda dhidi ya Iddi Amini: Wazee wetu wanakumbukwaje?

DOKEZO Miaka 45 tangu Majeshi ya Tanzania yashinde vita Uganda dhidi ya Iddi Amini: Wazee wetu wanakumbukwaje?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

w0rM

Member
Joined
May 3, 2011
Posts
81
Reaction score
192
IMG_0372.jpeg

Juni 9, mwaka 1979 Kamanda aliyeongoza Vita vya Uganda dhidi ya Iddi Amin alitamka kuikamata Ngome ya mwisho ya adui. Haikupita muda Amiti Jeshi Mkuu, Julius Kambarage Nyerere akatangazia Taifa na Dunia kuwa ngome ya mwisho ya adui imeanguka.

Ikiwa ni miaka 45 sasa tangu ushindi wa Vita hii. Je, tunawakumbuka na kuwaenzi vipi Mashujaa wetu wa Vita hii? Wapo walio hai hadi sasa!

Wenzetu Mataifa yaliyoendelea yanawaheshimu sana Mashujaa na Veterans wao. Mwezi huu Uingereza, Marekani, Canada na Ufaransa wanasherekea miaka 80 ya Wanajeshi wao waliopigana Kijasiri pale ufukwe wa Normandy (Ufaransa) wakitokea English Channel. Jumla ya Askari 150,000 walivuka na kuwakomesha Wajerumani na Waitaliano.

Mwaka 1978 - 1979 Tanzania kupitia kwa Jeshi la Wananchi (JWTZ) iliingia katika vita yake ya kwanza kutetea mipaka yake dhidi ya majeshi ya Idd Amin. Ushiriki wa JWTZ katika mapambano hayo ulikuwa wa Kiukombozi zaidi.

Tarehe 25/7 kila mwaka ni siku ya Mashujaa ambapo hufanyika kumbukizi kwa gwaride na vitu vingine. Imekuwa hivyo tangu tupate uhuru. Mstari wa mbele wanapitishwa waliopigana vita Kuu ya pili. Je, kwanini Mashujaa (Wanajeshi) waliopigana katika Vita vya Uganda na kuleta ushindi hawajawahi kutajwa katika sherehe hizo?

Hawa Wanajeshi waliopo hai na waliofariki tunawathamini na kuwaenzi kwa namna gani?

Soma:
 
"Yes, we need war, but not the fracas war."

Barrack Obama.

Haya utuambie, Nini hasa sababu ya kuzuka kwa vita hiyo? Kulikuwa na ulazima wowote ule kwa Tanzania Kupigana Vita hiyo? Je, Kati ya Tanzania (Mwl. Nyerere) na Uganda (Idd Amin) nani hasa alikuwa chanzo Cha kuanzisha chokochoko zilizosababisha Vita hiyo?
Faida gani tulipata kutokana na Vita hiyo??
 
"Yes, we need war but not the fracas war."

Barrack Obama.

Haya utuambie, Nini hasa sababu ya kuzuka kwa vita hiyo? Kulikuwa na ulazima wowote ule kwa Tanzania Kupigana Vita hiyo? Je, Kati ya Tanzania (Mwl. Nyerere) na Uganda (Idd Amin) nani hasa alikuwa chanzo Cha kuanzisha chokochoko zilizosababisha Vita hiyo?
Faida gani tulipata kutokana na Vita hiyo??
Ukisoma humu Mkuu utapata kwa uzuri majibu ya maswali yako

 
Wewe unaulizia waliopiga vita na Uganda kwanza Tungewakumbuka walio Pigania Uhuru wa Tanganyika hata kutajwa husikii Ukimuliza mwanafuzi wa Form 6 Bibi Titi ni nani na Alisaidia nini hamjuwi
 
Ahsante kwa uzi mzuri ila nasikitika kizazi cha sasa hakizingatii mambo muhimu kama haya!!

Pia kuweka rekodi sawa, sherehe ya mashujaa ni 25/07 ya kila mwaka tofauti na hpo ulipoandika!

Naomba kuwasilisha…
 
Ahsante kwa uzi mzuri ila nasikitika kizazi cha sasa hakizingatii mambo muhimu kama haya!!

Pia kuweka rekodi sawa, sherehe ya mashujaa ni 25/07 ya kila mwaka tofauti na hpo ulipoandika!

Naomba kuwasilisha…
Ni kwa sababu hawaoni UMUHIMU, faida au haina impact yoyote ile kwao katika maisha yao ya kila siku. Kwa nini wajishughulishe na jambo ambalo halina faida yoyote ile kwao??
 
Tanzania ndio nchi pekee wanaokusimulia wamepigana vita ya kagera wanauza kahawa na wapo mashambani wamechoka
 
Kama wewe ulivyo tabularasa
Eleza faida zake kama zipo ili Watu wapime wenyewe kuona kwamba Lina UMUHIMU wa kulizingatia au la.
Msipende kukumbukwa kwa UMUHIMU kutokana na mambo ya hovyo mliyofanya.

Barrack Obama aliwahi kusema kwamba "Yes, we need war, but not the fracas war.'

Kagera War is a fracas war.
 
Ilikuwa ni vita binafsi ya nyerere iliyotutia umasikini sana, ndio maana watu hawataki hatakuisimulia kwa jinsi masiha ya watanzania yalivyokuwa magumu na yalifikia mpaka kama nchi iliomba msaada wa chakula na kupewa mahindi ya njano na US.
 
Back
Top Bottom