Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
MIAKA 60 YA UHURU WA TANGANYIKA: JOHN RUPIA SIKU ZOTE ALIKUWA PEMBENI YA JULIUS NYERERE
Shughuli ilikuwa fupi.
Waandaaji wa hafla siku hizi wamekuwa makini sana kwa muda.
Hupenda kuzipeleka ratiba mbio ili watu wakafanye mambo yao mengine.
Tulikuwa tumefikia karibu ya kufunga ghafla Joyce ananiomba nimzungumze Mzee John Rupia.
Nikamwambia kuwa sikujitayarisha kuzungumza.
"Sikutaka ujitayarishe nilitaka umzungumze John Rupia kama umjuavyo.''
Nilizungumza maneno machache kwa kuwagutusha wanahistoria kumtazama vizuri Mzee John Rupia kwa sura yake nyingine ya mtu wa fikra.
Wasimtazame John Rupia kama anavyoelezwa kuwa alikuwa mfadhili wa TANU tu.
Wamtazame John Rupia kutokea mwaka wa 1950 alipokuwa mjumbe ndani ya TAA Political Subcommittee akiwaunga mkono vijana wanamapinduzi walioigeuza TAA kuwa chama cha siasa bila ya katiba ya siasa.
Nilipomaliza kuzungumza wajukuu wa John Rupia na watu wengine wakawa wananifata wakati wa chai kutaka niwaeleze zaidi kuhusu mzalendo huyu.
Nilikuwa nikiwachekesha wajukuu wa Mzee Rupia kwa kuwaambia kuwa wasidhani babu yao alikuwa "Sanduku la Fedha."
Niliwaambia kuwa John Rupia alikuwa na mchango mkubwa wa fikra mbali ya uwezo wa mali.
Niliwaambia kuwa kama vile alivyoendesha makampuni yake kwa ufanisi ni hivyo hivyo ndivyo alivyoisaidia TANU kufanikiwa na kuwa chama imara.
Niliwaeleza kuwa sahihi yake ipo katika nyaraka muhimu sana ya Mapendekezo ya Katiba yaliyopeleka kwa Gavana Edward Twining mwaka wa 1950.
Mapendekezo haya yalijadiliwa kwenye mkutano wa TAA wa 1954 uliounda TANU na ni sehemu ya hotuba aliyotoa Julius Nyerere UNO mwaka wa 1955.
Shughuli ilikuwa fupi.
Waandaaji wa hafla siku hizi wamekuwa makini sana kwa muda.
Hupenda kuzipeleka ratiba mbio ili watu wakafanye mambo yao mengine.
Tulikuwa tumefikia karibu ya kufunga ghafla Joyce ananiomba nimzungumze Mzee John Rupia.
Nikamwambia kuwa sikujitayarisha kuzungumza.
"Sikutaka ujitayarishe nilitaka umzungumze John Rupia kama umjuavyo.''
Nilizungumza maneno machache kwa kuwagutusha wanahistoria kumtazama vizuri Mzee John Rupia kwa sura yake nyingine ya mtu wa fikra.
Wasimtazame John Rupia kama anavyoelezwa kuwa alikuwa mfadhili wa TANU tu.
Wamtazame John Rupia kutokea mwaka wa 1950 alipokuwa mjumbe ndani ya TAA Political Subcommittee akiwaunga mkono vijana wanamapinduzi walioigeuza TAA kuwa chama cha siasa bila ya katiba ya siasa.
Nilipomaliza kuzungumza wajukuu wa John Rupia na watu wengine wakawa wananifata wakati wa chai kutaka niwaeleze zaidi kuhusu mzalendo huyu.
Nilikuwa nikiwachekesha wajukuu wa Mzee Rupia kwa kuwaambia kuwa wasidhani babu yao alikuwa "Sanduku la Fedha."
Niliwaambia kuwa John Rupia alikuwa na mchango mkubwa wa fikra mbali ya uwezo wa mali.
Niliwaambia kuwa kama vile alivyoendesha makampuni yake kwa ufanisi ni hivyo hivyo ndivyo alivyoisaidia TANU kufanikiwa na kuwa chama imara.
Niliwaeleza kuwa sahihi yake ipo katika nyaraka muhimu sana ya Mapendekezo ya Katiba yaliyopeleka kwa Gavana Edward Twining mwaka wa 1950.
Mapendekezo haya yalijadiliwa kwenye mkutano wa TAA wa 1954 uliounda TANU na ni sehemu ya hotuba aliyotoa Julius Nyerere UNO mwaka wa 1955.