Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Nimeandika mengi hapa kuhusu Abbas Sykes.
Mengi sana.
Atakae kumjua Abbas Sykes atafute tu hapa na kwengineko ataisoma historia yote ya kupigania uhuru wa Tanganyika kwa undani wake.
''Hesabu yangu ya wanachama watatu waliobakia wa siku za mwanzo za TANU na harakati za kudai uhuru mwaka wa 1954 imepungua baada ya kufariki Abbas Sykes.
Yawezekana sana kuwa bado wapo waasisi wengi wa TANU walio hai lakini hawajulikani.
Daftari langu limebakia na Mama Maria Nyerere na Mzee Athmani Matenga wa Magomeni Mwinyimkuu.''
''Abbas Sykes alinambia, ‘’Nilimwambia Dossa lazima ahudhurie mkutano wa Kizota na nilihakikisha hilo.
Nilimwambia tutaondoka pamoja kwenda Dodoma kwa hiyo nilimnunulia nguo na viatu.’’
Balozi alinieleza maneno haya kwa shida sana na kwa hakika niliona kuwa historia ya Dossa ilikuwa imemuumiza sana.''
''Hapo King's College Budo ndipo Abbas Sykes ailipokuja kusoma na Freddie Mutesa ambae baadae akajakuwa Kabaka wa Buganda na Rais wa Uganda mwaka 1962 Uganda ilipopata uhuru.
Balozi Sykes anakumbuka kumuona mama yake Freddie Mutesa akiwa kavaa yale magauni ya Kiganda akija shule kumtembelea mwanae na jinsi shule nzima ilivyokuwa ikitetemeka kwa ujio wa bi. mkubwa yule kwani Freddie ndiye aliyekuwa akitegemewa kuwa Kabaka wa Uganda.''
''Ananihadithia safari yake ya London akiwa Mwenyekiti wa ATC alipokwenda kuchukua mwili wa ndugu yake, kama alivyomwita mwenyewe, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Abbas Sykes kamjua Nyerere mwaka wa 1952 na Nyerere alipoacha kazi ya ualimu akaja kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes wakati wanamtafutia makazi yake.
Kifo cha Mwalimu na Abbas Sykes yumo ndani ya ndege ya ATC analiangalia jeneza la Nyerere.
Hili lilimrudisha nyuma sana wakati wako katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Fikra zake zilikarudi nyuma sana wako Mnazi Mmoja katika mkutano wa TANU yeye kijana wa kiasi cha miaka 24 hivi ikamjia picha Nyerere kaishiwa maneno anamwambia Bi. Titi, ''Titi hebu zungumza wewe.''
''Abbas Sykes alinihadithia anasema Nyerere alikuwa akija Dar es Salaam kutoka Pugu kuja kuonana na kaka yake alikuwa anapanda basi moja la Muhindi likiitwa ''Majigo.''
Kituo cha basi hili kilikuwa Mtaa wa Msimbazi na Aggrey.
Ukiingia na mzigo ndani ya basi basi yule Muhindi utamsikia akipiga kelele, ''Majigo juu, majigo juu.''
Maana ya maneno haya ilikuwa, ''Mzigo juu.''
Yaani mizigo ipandishwe juu ya basi kwenye ''carrier.''
Hivi ndivyo basi lile lilivyopata umaarufu wake na kuishia kuitwa ''Majigo.''
Hiki kilikuwa kipindi kabla ya Nyerere hajajiuzulu ualimu.
Nyerere alikuwa akishashuka pale kwa Majigo atashika njia kuelekea Kariakoo Market ofisini kwa Market Master Abdul Sykes.''
Mengi sana.
Atakae kumjua Abbas Sykes atafute tu hapa na kwengineko ataisoma historia yote ya kupigania uhuru wa Tanganyika kwa undani wake.
''Hesabu yangu ya wanachama watatu waliobakia wa siku za mwanzo za TANU na harakati za kudai uhuru mwaka wa 1954 imepungua baada ya kufariki Abbas Sykes.
Yawezekana sana kuwa bado wapo waasisi wengi wa TANU walio hai lakini hawajulikani.
Daftari langu limebakia na Mama Maria Nyerere na Mzee Athmani Matenga wa Magomeni Mwinyimkuu.''
''Abbas Sykes alinambia, ‘’Nilimwambia Dossa lazima ahudhurie mkutano wa Kizota na nilihakikisha hilo.
Nilimwambia tutaondoka pamoja kwenda Dodoma kwa hiyo nilimnunulia nguo na viatu.’’
Balozi alinieleza maneno haya kwa shida sana na kwa hakika niliona kuwa historia ya Dossa ilikuwa imemuumiza sana.''
''Hapo King's College Budo ndipo Abbas Sykes ailipokuja kusoma na Freddie Mutesa ambae baadae akajakuwa Kabaka wa Buganda na Rais wa Uganda mwaka 1962 Uganda ilipopata uhuru.
Balozi Sykes anakumbuka kumuona mama yake Freddie Mutesa akiwa kavaa yale magauni ya Kiganda akija shule kumtembelea mwanae na jinsi shule nzima ilivyokuwa ikitetemeka kwa ujio wa bi. mkubwa yule kwani Freddie ndiye aliyekuwa akitegemewa kuwa Kabaka wa Uganda.''
''Ananihadithia safari yake ya London akiwa Mwenyekiti wa ATC alipokwenda kuchukua mwili wa ndugu yake, kama alivyomwita mwenyewe, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Abbas Sykes kamjua Nyerere mwaka wa 1952 na Nyerere alipoacha kazi ya ualimu akaja kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes wakati wanamtafutia makazi yake.
Kifo cha Mwalimu na Abbas Sykes yumo ndani ya ndege ya ATC analiangalia jeneza la Nyerere.
Hili lilimrudisha nyuma sana wakati wako katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Fikra zake zilikarudi nyuma sana wako Mnazi Mmoja katika mkutano wa TANU yeye kijana wa kiasi cha miaka 24 hivi ikamjia picha Nyerere kaishiwa maneno anamwambia Bi. Titi, ''Titi hebu zungumza wewe.''
''Abbas Sykes alinihadithia anasema Nyerere alikuwa akija Dar es Salaam kutoka Pugu kuja kuonana na kaka yake alikuwa anapanda basi moja la Muhindi likiitwa ''Majigo.''
Kituo cha basi hili kilikuwa Mtaa wa Msimbazi na Aggrey.
Ukiingia na mzigo ndani ya basi basi yule Muhindi utamsikia akipiga kelele, ''Majigo juu, majigo juu.''
Maana ya maneno haya ilikuwa, ''Mzigo juu.''
Yaani mizigo ipandishwe juu ya basi kwenye ''carrier.''
Hivi ndivyo basi lile lilivyopata umaarufu wake na kuishia kuitwa ''Majigo.''
Hiki kilikuwa kipindi kabla ya Nyerere hajajiuzulu ualimu.
Nyerere alikuwa akishashuka pale kwa Majigo atashika njia kuelekea Kariakoo Market ofisini kwa Market Master Abdul Sykes.''