Michango isiyokuwa na manufaa kwa mchangiaji

Michango isiyokuwa na manufaa kwa mchangiaji

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kuna kipindi nilipitia wakati mgumu, wa kuuguza watu wangu wa karibu wawili kwa wakati mmoja, na ikapelekea hali ya kuyumba kiuchumi. Kwa sababu pia matibabu yao yalikuwa yako juu.

Nilikomba mpaka senti ya mwisho; hakuna rafiki, kikundi, wala ndugu aliyejigusa. Wengi walikaa mbali na mimi, zaidi ya kuniambia pole tu, Mungu atakusaidia.

Ikafikia mpaka hatua za kutaka kuuza rasilimali zangu; kilichonisaidia, ilibidi nikope bank ili kuweka mambo sawa. Bahati nzuri, hicho kipindi kikapita, ingawa nilipoteza mmoja kati ya wale niliokuwa nawapambania.

Baada ya muda nikawa nimerudi kwenye mstari; sasa changamoto inayojitokeza, ni baadhi ya vikundi kuniletea kadi za michango; mara mchango wa jengo la kuabudia, mara jumuia, mara harusi, mara shida mbali mbali n.k

Sasa najiuliza, mimi ndio natakiwa kutoa tu na si kusaidiwa pale na mimi ninapotaka uhitaji?

Kwa kifupi wakuu, mi sitoi mchango, na wala sichangii chochote, ni bora hiyo hela nikapige bia pamoja na mtoto mrembo pale kwa mangi maisha yaendelee.

Waniite mbahili powa tu, lakini chakula cha muumba ni sala na si hela.
 
Toa au changia tu kama sehemu ya fuaraha yako wala usisubiri na wewe waje wakuchangie.

Binadamu utapendwa kutokana na nafasi yako uliyonayo kinyume na hapo huna thamani.
 
Nilipata funzo kubwa sana mkuu; usipojiwekeza wewe mwenyewe, uje utegemee kikundi, marafiki, ndugu n.k utaenda na maji
Ni kweli ndugu. Inabidi tuzijengee familia zetu uwezo wa kujitegemea na kustahimili kwa kiasi fulani hususani wakati wa majanga.
 
Toa au changia tu kama sehemu ya fuaraha yako wala usisubiri na wewe waje wakuchangie.

Binadamu utapendwa kutokana na nafasi yako uliyonayo kinyume na hapo huna thamani.
Kuna swali moja, niliulizwa na mzee wangu; 'ni nani yuko tayari, kuuza nyumba yake au gari lake ili aweze kukuuguza?'
 
Wewe uliwaomba msaada mkuu, ujue kuna kutoa taarifa na kuomba msaada.
Kuna baadhi ya familia huwa wanakataa misaada kabisa wanakomaa wenyewe tu.

Tusilaumu watu ilhali hukuomba msaada bali unatoa taarifa (mtu ajiongeze) kwa ndgu unaweza kutoa tu taarifa ajiongeze mwenyewe lakini kwa watu baki ni tofauti, wao pia wana shida zao so kujua ukubwa wa shida yako bila kuwashirikisha aina ya msaada unaohitaji ukiwalaumu unakosea sana.
 
Pole na hongera kwa yote. Imeandikwa "tusichoke kutenda mema" ikiwa ndani ya uwezo wetu, bila kujalisha binadamu wengine wanaishije nasi.
Ndugu kaza kidogo basi,haya mambo ya sijui 7×70 sijui sote ni ndugu sjui vuta subira ndo yanatufikisha hata kama watanzania.Mbona ukiwa na njaa huvuti subira??
 
Wewe uliwaomba msaada mkuu, ujue kuna kutoa taarifa na kuomba msaada.
Kuna baadhi ya familia huwa wanakataa misaada kabisa wanakomaa wenyewe tu.

Tusilaumu watu ilhali hukuomba msaada bali unatoa taarifa (mtu ajiongeze) kwa ndgu unaweza kutoa tu taarifa ajiongeze mwenyewe lakini kwa watu baki ni tofauti, wao pia wana shida zao so kujua ukubwa wa shida yako bila kuwashirikisha aina ya msaada unaohitaji ukiwalaumu unakosea sana.
Ni sawa na kwenda kumtazama mgonjwa hospitali, huku hujabeba matunda, hata senti tano, au kutoa maamuzi yenye tija; unabaki kusema Mungu atakusaidia; mgonjwa amekuwa tv?
 
Ni sawa na kwenda kumtazama mgonjwa hospitali, huku hujabeba matunda, hata senti tano, au kutoa maamuzi yenye tija; unabaki kusema Mungu atakusaidia; mgonjwa amekuwa tv?
Wewe hukua mgonjwa ila ndgu zako ndio walikua wagonjwa, vipi kama kitaa unaonekana una wadhfa!?

Hujasema utasaidiwaje sasa!? Huoni wale wanaotangazwa kwenye social media husaidiwa haraka coz wameweka wazi shida zao na misaada wanayohitaji, anaesaidia hawezi kumsaidia mtu nyumba wakati hakuomba hilo.

Huenda wewe ungeomba msaada wapo ambao wangejitolea kupeleka chakula hospital kila siku, ila uliamua kukomaa na kuweka sura ya huruma bila kusema, sio wote wanajua kusoma saikolojia za watu ndgu yangu.

Kama uliwaomba na wakakuchinjia baharini basi una haki ya kua na hasira nao mkuu.

Pole kwa yaliyokukuta lakini.
 
Back
Top Bottom