Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
-
- #4,441
Wanachama SHIWATA wapatiwa hati miliki
na Makuburi Ally
WANACHAMA 127 wa Taasisi ya SHIWATA wamepatiwa hati za kimila za kumiliki maeneo yao katika kijiji cha Mwanzega kwa ajili ya makazi.
Akizungumza katika mkutano wa wanachama wa SHIWATA, jana, Mwenyekiti wa Shiwata, Taalib Cassim, alisema pamoja na wanachama hao kupatiwa maeneo yao lakini awali yaliyotokea malalamiko kwamba viwanja walivyopewa ni vidogo, hivyo wamewaongezea ukubwa wa viwanja hivyo.
Cassim alisema baada ya kuongeza ukubwa wa viwanja hivyo hivi sasa, viwanja hivyo ambavyo viligawanywa kwa viwanja 30 kwa block moja ambako kwa sasa vitakuwa viwanja 26 katika block moja.
Aidha Cassim alisema baada ya kuanza kwa makabidhiano hayo, Februari 19, utafanyika uzinduzi wa ugawaji wa viwanja utakaofanyika kijijini Mwanzega.
Awali kabla ya ugawaji wa hati hizo, jana ilifanyika semina kutoka Mawakala wa Utafiti wa Majengo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHRBA) walitoa semina ya ujenzi wa nyumba za wanachama hao.
Meneja Ushauri wa HNRBA, Dk. Simona Kintingu alisema gaharama za ujenzi wa nyumba hizo kwa kiwango cha juu ni sh mil 26 na cha chini ni sh mil. 5.
Kintingu aliongozana na Injinia Dk. G.M Kawiche ambaye ni Mkurugenzi wa NHRBA ambaye naye alitoa somo kwa wanachama hao.
na Makuburi Ally
Akizungumza katika mkutano wa wanachama wa SHIWATA, jana, Mwenyekiti wa Shiwata, Taalib Cassim, alisema pamoja na wanachama hao kupatiwa maeneo yao lakini awali yaliyotokea malalamiko kwamba viwanja walivyopewa ni vidogo, hivyo wamewaongezea ukubwa wa viwanja hivyo.
Cassim alisema baada ya kuongeza ukubwa wa viwanja hivyo hivi sasa, viwanja hivyo ambavyo viligawanywa kwa viwanja 30 kwa block moja ambako kwa sasa vitakuwa viwanja 26 katika block moja.
Aidha Cassim alisema baada ya kuanza kwa makabidhiano hayo, Februari 19, utafanyika uzinduzi wa ugawaji wa viwanja utakaofanyika kijijini Mwanzega.
Awali kabla ya ugawaji wa hati hizo, jana ilifanyika semina kutoka Mawakala wa Utafiti wa Majengo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHRBA) walitoa semina ya ujenzi wa nyumba za wanachama hao.
Meneja Ushauri wa HNRBA, Dk. Simona Kintingu alisema gaharama za ujenzi wa nyumba hizo kwa kiwango cha juu ni sh mil 26 na cha chini ni sh mil. 5.
Kintingu aliongozana na Injinia Dk. G.M Kawiche ambaye ni Mkurugenzi wa NHRBA ambaye naye alitoa somo kwa wanachama hao.