Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Kocha Yanga aisifu mipango ya Simba Afrika Wednesday, 02 February 2011 20:38

Jessca Nangawe
KOCHA wa zamani wa Yanga, Kenny Mwaisabula amesema Simba ina nafasi kubwa ya kuvuka raundi ya pili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kutokana na morali na juhudi walizoonyesha katika mchezo wao wa awali huku akidai Yanga inahitaji kuongeza juhudi na kushikamana zaidi kutokana na kutawaliwa na migogoro ndani ya klabu hiyo.

Simba na Yanga zote zinakabiliwa na michezo ya marudiano baada ya wote kutoka sare katika mechi zao za awali. Simba itakuwa nyumbani ikimenyana na Wacomoro wa Elan wakati Yanga wataifuata Dedebit ya Ethiopia mjini Addis Ababa wiki ijayo.

Mwaisabula alisema timu hizo zinakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha zinaiwakilisha vema Tanzania na kuvuka hatua ya pili hivyo zina kazi kubwa mbele yao katika kufanikisha hilo.

Kwa upande wake, alisema tofauti na Yanga, lakini Simba imeonekana kuwa na morali kubwa na kujituma zaidi hivyo kupewa nafasi ya kufika mbali ikilinganishwa na Yanga ambao walicheza chini ya kiwango na kusumbuliwa na migogoro inayoendelea kuikumba klabu hiyo.

Naye Kanakamfumo alisema kwa kiasi kikubwa, migogoro imesababisa kucheza chini ya kiwango tokea mchezo wa awali na endepo hawatajipanga na kucheza kwa ushindani ni wazi watayaaga mapema mashindano hayo.

Alisema kocha Msaidizi wa timu hiyo anatakiwa kuendelea na mfumo aliouacha Kosta Papic na kinyume na hapo atawachanganya wachezaji na kujikuta wakipoteza mchezo wa marudiano.

"Sisemi hivi ili kuwavunja moyo Yanga bali natoa kama hadhari kwao kuweza kujipanga mapema na kutambua makosa yao.

Yanga wanakabiliwa na migogoro inayoendelea ndani ya klabu hiyo na kwa kiasi kikubwa inaadhiri hata matokeo kuwa mabaya kwa timu hivyo ni vyema wakaangalia na ukubwa wa mashindano haya ili kutambua nini wanapaswa kufanya kwa sasa:alisema Kanakamfumo.
 
Van Persie: United will slip up






Updated Feb 4, 2011 8:49 AM ET
Robin van Persie is "100% confident" Manchester United will drop points as the race for the Premier League title hots up.
The Gunners head into this weekend's fixtures still within striking distance of the leaders after they came from behind to beat Everton 2-1, while United made it 24 league games without defeat as a double from Wayne Rooney helped them defeat Aston Villa.

Sat., Feb. 5
Stoke City vs. Sunderland
Aston Villa vs. Fulham
Everton vs. Blackpool
Man City vs. West Brom
Newcastle vs. Arsenal
Tottenham vs. Bolton
Wigan vs. Blackburn
Wolves vs. Man United
Sun., Feb. 6
West Ham vs. Birmingham
Chelsea vs. Liverpool
BPL Scores | Table | Fixtures


Sir Alex Ferguson takes his men to bottom club Wolves in Saturday afternoon's late kick-off at Molineux - a venue where Chelsea have already come unstuck earlier in the season.
Next up is the small matter of the Manchester derby at Old Trafford, while United head to Stamford Bridge on March 1 and then Anfield five days later with a showdown against the Gunners at Emirates Stadium set for the end of April.
While van Persie believes United, currently five points clear, face a tough ask to collect maximum returns from all those key fixtures, the Dutchman accepts first and foremost Arsenal must deliver consistency themselves.
"It is vital to just keep looking at yourself," van Persie told Arsenal TV Online.
"We all know United's schedule, we know Chelsea's schedule, but the main thing is to just look at our own.
"We have got a tough opponent now at Newcastle away, and so we only need to look at that."
The Dutch striker continued: "I am confident Manchester United will drop points, 100%, because they have big games coming up - they have their own derby, they have games against Chelsea, other big games, so we will see what is going to happen.
"We just have to stick to ourselves and I am confident we can fight until the end."
Van Persie has slowly regained his match sharpness after his return from injury, hitting seven goals since the turn of the year.
The 27-year-old, who was part of the Dutch squad which reached the World Cup final in South Africa, is confident he grows stronger with every appearance.
"I am feeling really happy and healthy in myself at the moment," Van Persie said.
"I was right to take things quite carefully when I first came back - you have to keep in mind that I was basically injured for an entire calendar year, except for the summer.

TRANSFER SPECIAL

Keep up with all the biggest moves around the globe with our 2011 January transfer gallery.

"I'd had two big ankle injuries in the space of 12 months and needed some time to get properly fit.
"That is why the boss, the medical team and I chose to do things more slowly, step by step, and I think it has paid off in the end.
"Since the Chelsea game things have really kicked on - I have become stronger in every game and every training session.
"Sometimes it is good to start cautiously and that was definitely the case for me."
Arsenal captain Cesc Fabregas found himself under the media spotlight this week, his temperament brought into question by allegations from Everton boss David Moyes of improper conduct as the players went down the tunnel at half-time on Tuesday night, when the hosts were trailing to a controversial goal.
Gunners boss Arsene Wenger yesterday launched a staunch defence of his skipper, while hitting out at Moyes for going public with "what he pretends to have heard in the tunnel".
Wenger, though, maintains the club "do not want to develop a paranoia" over the treatment of their captain as they focus on maintaining interest on four fronts.
"We have a good mentality - we are hungry for success and we want to do well," he said.
"We have a good togetherness - one of the advantages of our team is that when you look at our side, they have all been educated here, they started in the Premier League together so there is a natural bond.
"We have the spirit, but it is not there forever if you don't care for it and that is one of the things which is in front of us."
Newcastle beat Arsenal 1-0 at Emirates Stadium in November through a header from Andy Carroll.
Despite selling their star striker to Liverpool on transfer deadline day for a cool £35million, Wenger still feels the Magpies will present a tough challenge.
"We expect Newcastle to be up for it against us and we prepare ourselves to meet a good team," he said.
 
Fernando Torres explains quitting Liverpool for Chelsea


Torres was unveiled at Chelsea's Cobham training ground on Friday


Chelsea new boy Fernando Torres said he left Liverpool because they were a club in transition and a long way from delivering the success he craves.
Torres, signed for a British record £50m on Monday, said: "Things had changed a lot in the last year.
"I think they have great ambition and they are doing the right things to get back but it will take time. I didn't have that time."
Torres said he would not celebrate if he scores against Liverpool on Sunday.
 
Henry: Dalglish the best choice






Updated Feb 4, 2011 4:48 AM ET
John W Henry has hinted Liverpool will hand Kenny Dalglish an extended deal as manager and stay at Anfield by redeveloping the famous venue.
Dalglish was named Reds manager for the remainder of the season following Roy Hodgson's sacking last month, much to the delight of the club's fans.


Despite a slow start to Dalglish's return, the team are now in fine form having won their last three matches without conceding a goal.
The 59-year-old Scot has lifted the doom and gloom surrounding the club and Henry admits the club are reaping the rewards of bringing Dalglish back.
"It's still early, but in retrospect you could not have made, in our case it was very fortunate for us, but we could not have made a better choice," he told Fox Soccer Channel.
"I know he, for a long time now, has wanted to be in this position, so it's a great thing for the club, for Kenny and for us."
As well as retaining Dalglish's services Henry has hinted the club could opt to stay at Anfield and redevelop the venue rather than move to a new home.
A new stadium has been top of Liverpool's agenda for some time but having sampled the unique atmosphere, Henry is against running the risk of losing their identity in a new ground.
"The Kop is unrivalled," he continued. "The atmosphere, I was really surprised because we've heard so much about needing a new stadium.
"We were surprised at how beautiful Anfield was both viewing it as an empty stadium and then with the first game. It would be hard to replicate that feeling anywhere else."
This week saw the exit of star striker Fernando Torres for rivals Chelsea and Henry insists there was little point in retaining a player who wanted to move.
Sparks are sure to fly on Sunday with Torres is line to make an immediate appearance against Liverpool when he makes his Chelsea debut.
"One of things that we talked about from the very beginning was how important it was that everyone was on the same page. No player is bigger than the club," Henry said.
"We expect players to want to be there. If they don't want to be part of Liverpool Football Club then we should do everything we can to facilitate them going elsewhere."
 
Terry: Bridge must applaud Joe






Updated Feb 4, 2011 5:45 AM ET
Chelsea captain John Terry hopes Blues fans give Joe Cole a good reception when he returns to Stamford Bridge for Sunday's game with Liverpool.
The 29-year-old spent seven years with the Blues following his move from West Ham before leaving on a free transfer last summer.

TURNING POINT

Jamie Trecker presents his five keys to victory as Chelsea and Liverpool meet in the 'Game before the Game' this Sunday with coverage starting at 10 a.m. ET on FSC.

The England international was a firm fans' favourite during his time at the club and Sunday's game will be first return to his former home as a Reds player.
Terry insists Cole is a "Chelsea boy" and believes that he deserves to be recognised for his efforts with the Londoners.
"Joe gave everything for this club and hopefully the fans will recognise that and give him the reception he deserves," explained Terry.
"He is a Chelsea boy, even when he was at West Ham he said he was a Chelsea boy as a kid.
"I was sorry to see him go, others were too. That's why I'm 100 per cent sure he'll get a great reception."
Terry remains close friends with Cole and despite the fact he has endured a slow start to life at Anfield, he is backing the midfielder to come good.
"He's a great lad and I'm still in contact with him," Terry continued.
"I watched his debut and him getting sent off - he should never have been sent off. Then he picked up a knock but he is confident in his own ability and me too.
"I'm sure he will have a huge part to play for Liverpool."
 
Wachezaji Yanga wavivu-Timbe

Imeandikwa na Zena Chande; Tarehe: 4th February 2011 @ 23:59

KOCHA mpya wa Yanga Sam Timbe, jana alitambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kuahidi mambo mengi ya kuifanyia timu hiyo mojawapo likiwa ni kuondoa uvivu kwa wachezaji.

“Nimeona wachezaji wengi wana uvivu yaani mtu akipoteza mpira hatafuti utakuta anasimama au akitoa pasi hafuatilii kuona kama imefika au la wakati unatakiwa kufuatilia lakini hilo nitalifanyia kazi mara nitakapoanza kazi, lazima beki ujue kama unatakiwa kufuata mpira ukipoteza pasi,” alisema Timbe alipokuwa akijibu maswali ya waandishi katika utambulisho huo.

Pia alisema kitu kingine alichokigundua kwa wachezaji wa timu yake hiyo mpya ni bidii, hasa alipoiona ikicheza na Dedebit ya Ethiopia katika mechi ya michuano ya Kombe la Shirikisho mwishoni mwa wiki iliyopita.

“Yanga haikucheza kwa bidii katika mechi ile, hawakuwa na presha na wachezaji walipoamua kucheza kwa presha ndio wakapata mabao yale kwa hiyo na hilo pia ni suala la kulifanyia kazi,” alisema.

Alisema pamoja na hayo lakini atakapoanza rasmi kukinoa kikosi hicho atayafanyia kazi upungufu aliouona na aliahidi pia timu yake itashinda dhidi ya Dedebit katika mechi ya marudiano itakayofanyika Ethiopia mwishoni mwa wiki ijayo.

“Kama wao (Dedebit) walitufunga hapa mabao manne, kwa nini sisi tusishinde kwao, tunaweza tu kushinda,”alisema.

Katika mechi ya kwanza, Yanga ililazimishwa sare ya mabao 4-4 na kufanya kuwa na nafasi ngumu ya kusonga mbele katika mechi ya marudiano kwani italazimika kupata ushindi wowote na kama itatoka sare basi iwe ya kuanzia mabao 5-5.

Akizungumzia suala la mgogoro wa viongozi wa klabu hiyo, Timbe alisema ugomvi huo haumhusu yeye wala wachezaji.

“Mimi ninachoomba ni ushirikiano kati ya wachezaji, wanachama na mashabiki, ikiwa hivyo tutafanya vizuri tu kwenye mashindano na hapo viongozi tutawaleta pamoja watapatana,”alisema.

Hata hivyo Ofisa Habari wa Yanga Louis Sendeu ambaye jana ndiye aliyemtambulisha Timbe kwa waandishi alisema kocha huyo ataanza kuifundisha timu akiwa hana mkataba.

“Kwa sasa hatujaingia naye mkataba bado ataanza kuifundisha timu huku mambo mengine yakifanywa taratibu… leo (jana) akishamaliza na nyie hapa ataondoka kwenda kwao Kampala halafu atarudi Jumapili (kesho) ambapo ataungana na wachezaji na kuanza kazi rasmi,” alisema.

Timbe aliwahi kuifundisha timu ya taifa ya vijana ya wanawake ya Kuwait na kwa upande wa Klabu amewahi kuzifundisha timu za Villa SC, Polisi za Uganda na Atraco ya Rwanda ambapo zote alizifundisha kwa mafanikio makubwa baada ya kuziwezesha kutwaa taji la Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame).

Kocha huyo anachukua nafasi ya Mserbia Kostadin Papic aliyebwaga manyanga baada ya kutofautiana na uongozi. Atasaidiwa na mzawa Fredy Minziro.

Wakati huohuo, Yanga leo itashuka Uwanja wa Majimaji Songea kuivaa Majimaji ya huko katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuwa mkali na wa kuvutia.

Michezo mingine leo itakuwa kati ya Kagera Sugar na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, huku AFC Arusha ikiwa mwenyeji wa Ruvu Shooting Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.


 
Tegete, Gumbo watemwa Stars, Mgosi, Banka warudishwa

Imeandikwa na Evance Ng'ingo; Tarehe: 4th February 2011 @ 23:55

KOCHA Mkuu wa Taifa Stars Jan Poulsen ametangaza kikosi chake kipya huku akiwaacha Jerry Tegete wa Yanga, Rashid Gumbo wa Simba na nyota wote wanaocheza soka nje ya Tanzania.

Katika kikosi hicho cha wachezaji 22 amewaita kwa mara ya kwanza beki Chacha Marwa wa Yanga, Julius Mrope wa Mtibwa Sugar, Ramadhan Chombo wa Azam, huku akiwarudisha beki Juma Jabu na Haruna Shamte wote wa Simba.

Wengine ambao amewarudisha tena kwenye kikosi hicho ni Mussa Mgosi na Mohammed Banka wa Simba pamoja na John Bocco wa Azam.

Kiungo Godfrey Bonny wa Yanga ambaye kwa muda mrefu hayupo kwenye kikosi cha Taifa Stars naye amekumbukwa.

Akizungumza jana, Poulsen alisema kikosi hicho ni kwa ajili ya mchezo wa kirafiki na Palestina utakaofanyika Februari 9, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia sababu za kumwacha mchezaji Ali Ahmed ‘Shibori', Paulsen alisema kuwa mchezaji huyo anatakiwa kujiendeleza zaidi hasa kwa kujifunza kasi na kuongeza uwezo wa kucheza.

Wachezaji wanaocheza nje ya nchi wote amewaacha ambao ni Athumani Machupa (Sweden), Said Maulid (Angola), Idriss Rajabu (Kenya), Henry Joseph (Sweden) na Nizar Khalfan (Canada).

Kikosi kamili ni makipa: Shaaban Kado (Mtibwa Sugar) na Juma Kaseja (Simba), mabeki Shadrack Nsajigwa (Yanga), Aggrey Morris (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Juma Nyoso, Haruna Shamte na Juma Jabu (Simba) na Chacha Marwa (Yanga).

Viungo ni Shaaban Nditi (Mtibwa Sugar), Nurdin Bakari (Yanga), Jabir Aziz (Azam), Godfrey Bonny (Yanga) na Ramadhan Chombo (Azam). Washambuliaji ni Mrisho Ngasa (Azam), Julius Mrope (Mtibwa) Mohamed Banka, Mgosi (Simba), Machaku Salum (Mtibwa), John Bocco (Azam) na Mbwana Samata (Simba).

 
Choki aibomoa Twanga Pepeta

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 4th February 2011 @ 23:50

BENDI ya Extra Bongo 'Kujinafasi Next Level' imechukua wanamuziki watano kutoka bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta'.

Akizungumza wakati wa kuwatambulisha wanamuziki hao Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa bendi hiyo, Ally Choki alisema uamuzi wa kuwachukua wanamuziki hao ni katika kujijenga kwa bendi yake.

"Kaulimbiu yetu sasa hivi ni mapinduzi kwenye muziki, nimedhamiria kwa dhati kabisa kufanya mapinduzi kwenye muziki, hivyo nimewachukua hawa vijana kuhakikisha najiimarisha vizuri zaidi," alisema Choki ambaye amepata kuimbia Twanga.

Aliwatambulisha wanamuziki hao ambao pia walikuwepo kwenye mkutano huo ni Hassan Mussa 'Nyamwela' Danger Boy na Otilya Boniphace ambao ni wanenguaji, wakati mwimbaji ni Rogart Hega 'Katapila'.

Kwa upande wa wanamuziki wengine ni mpiga gita la besi Hoseah Mgohachi na mpiga solo Godfrey Kanuti wakati repa ni Saulo John 'Ferguson'.

Choki alisema wanamuziki hao watajiunga na wenzao leo kambini jijini Dar es Salaam tayari kwa maandalizi ya albamu ya bendi hiyo aliyoielezea kuwa itakuwa moto wa kuotea mbali.

Wanamuziki hao kwa nyakati tofauti wakizungumza kwenye mkutano huo walisema kujiunga kwao Extra Bongo ni katika kujiendeleza zaidi kimuziki.

 
 
PHP:
Ruta: asante ripoti kamili juu ya kikosi cha timu ya Taifa:
Niko pembezoni mwa nchini kiasi kwamba magazeti huwa tunayapata baada ya siku moja.
 
Kumbe na Kelvini Yondani naye kaachwa!!!!!

ndiyo hivyo ndugu yangu.......................
 
Tegete, Gumbo nje, Samata, Bonny ndani Stars
Friday, 04 February 2011 21:00
kocha wa Taifa Stars,Jan Poulsen

Sweetbert Lukonge
MSHAMBULIAJI Jerryson Tegete na Rashid Gumbo kwa mara nyingine wameshindwa kupenya kwenye chujio la kocha Jan Poulsen na kuwa kati ya wachezaji walioachwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kinachojiandaa kucheza mechi ya kirafiki na Palestina, mchezo utakaofanyika Februari 16, jijini Dar es Salaam.

Mshambuliji huyo wa Yanga, aliyeachwa na kocha huyo katika michuano ya Chalenji, lakini aliitwa na Sylvestre Marsh kwenda michuano ya Mto Nile, lakini jana Poulsen alipotangaza orodha yake mpya jina la nyota huyo halikuwemo.

Naye Rashid Gumbo, mmoja wa wachezaji chipukizi wanaoonyesha soka ya uhakika, pia hayumo kwenye orodha hiyo ya wachezaji 22. Mchezo huo ni sehemu ya Stars kujiandaa na mechi dhidi ya Afrika ya Kati hapo Machi 9 kuwania kucheza Fainali za Afrika mwaka 2012.

Kocha wa Stars, Poulsen amemrudisha Mussa Hassan Mgosi aliyeachwa kutokana na kuelezwa kushuka kiwango pamoja na kumuita, beki wa Yanga, Chacha Marwa pamoja na kiungo wa timu hiyo, Godfrey Bonny aliyeachwa dakika za mwisho na Marcio Maximo.

Beki wa Simba, Juma Jabu na mshambuliaji chipukizi wa timu hiyo, Mbwana Samata wameitwa kwenye timu hiyo. Kiungo wa zamani wa Simba anayekipiga Azam FC, Ramadhani Chombo 'Redondo' ameitwa pamoja na Julius Mrope wa Mtibwa Sugar.

Akizungumza na Mwananchi Poulsen alisema kuwa ameamua kuwaita wachezaji hao kutokana na uwezo wao mkubwa waliounyesha katika mechi mbalimbali za Ligi Kuu walizocheza wakiwa na klabu zao.

"Zaidi mimi naangalia uwezo wa mchezaji pia mafanikio, najua watu wengi watajiuliza kwanini nimemwita Bonny katika kikosi hiki wakati ana umri mkubwa.

"Nimemwita Bonny pamoja na wachezaji hao wengine kutokana na kuonyesha uwezo wa kucheza soka katika baadhi ya mechi nilizoziona wakiwa na timu zao, umri kwangu siyo tatizo nachoangalia zaidi ni mafanikio," alisema Poulsen.

Wengine walioitwa ni pamoja na Juma Kaseja na Shabani Kado (makipa) wakati mabeki ni
Shadrack Nsajigwa, Aggrey Morris, Nadir Haroub 'Cannavaro', Juma Nyoso, Kelvin Yondani na Haruna Shamte.

Viungo ni Shaaban Nditi, Nurdin Bakari na Jabir Aziz wakati washambuliaji ni Mrisho Ngassa, Mohamed Banka, Salum Machaku na John Bocco.

Hata hivyo Poulsen alisema kuwa alimewaacha Mohamed Shibori, Godfrey Taita, Jerryson Tegete, pamoja na Setephan Mwasika siyo kuwa viwango vyao vimeshuka isipokuwa baadhi yao ni majeruhi na pia ni moja ya kuwapa nafasi wengine ya kuonyesha viwango.

 
Mwanaidi kumtuza Mzee Yusuf ‘Nitakufa kwa Ahadi' Valentine


na Abdallah Menssah


MWIMBAJI wa wakongwe wa mipasho, East African Melody, Mwanaidi Shaaban, anatarajiwa kupamba onyesho maalum la Jahazi Modern Taarab lililopangwa kurindima mkesha wa siku ya Wapendanao ‘Valentine Day'.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Msaidizi wa Jahazi Modern, Hamis Boha, alisema kuwa wamemwalika Mwanaidi katika onyesho hilo kwa ajili ya kuimba kibao chake cha ‘Nitakufa kwa Ahadi'.
"Unajua, tumeona ni muhimu kumwalika Mwanaidi katika onyesho hili, ili kumfariji Mzee Yussuf ‘Mfalme' atakayerejea tena jukwaani siku hiyo baada ya likizo ndefu ya ugonjwa, kwa vile alishazushiwa kifo," alisema Boha.
Aidha, Boha alisema kuwa, mbali ya kibao hicho cha ‘Nitakufa kwa Ahadi', Mwanaidi pia ataimba nyimbo zake nyingine kadha wa kadha zinazovuta hisia za mashabiki pamoja na wapenzi wengi wa mipasho.
Kwa upande wake, Mfalme Yussuf alisema, amepanga kuwapoza mashabiki machungu ya kutomwona kwa muda mrefu, kwa kuwaimbia vibao vyake vyote alivyorekodi tangu alipoanzisha Jahazi Modern.
"Siku hiyo, nitaimba ‘Two In One', ‘Nakula kwa Nakshi Nakshi', ‘Tupendane Wabaya Waulizane', ‘VIP Nafasi Yangu', ‘Daktari wa Mapenzi' pamoja na ‘My Valentine', ili mradi tu niweze kuwasafirisha kila sehemu na nwajisike wamefika," alisema Yussuf.
Kadhalika, alisema kibao chake cha ‘My Valentine' kitakuwa ni maalum siku hiyo, ambako kwa kuwaonyesha mashabiki kuwa, alisikitika kwa kutokuwa nao kwa muda, atakiimba akiwa amekaa chini mbele ya jukwaa.





juu
 
Yanga yasaka heshima Songea
Friday, 04 February 2011 20:55

Sosthenes Nyoni, Songea
BAADA ya kuadhibiwa na Mtibwa kwa bao 1-0, Yanga leo inatakuwa ugenini mjini Songea kuikabili Majimaji katika mpambano utakaofanyika kwenye Uwanja wa Majimaji.

Kikosi cha Yanga ambacho kiliondoka jijini Dar es Salaam juzi mchana kikiwa na wachezaji 20, tayari kimewasili mjini hapa. Awali walishindwa kufika hapa kwa wakati baada ya basi wanalolitumia kusafiria kuharibika maeneo ya Chalinze mkoani Pwani.

Yanga ambayo bado inashikilia usukani wa ligi hiyo kwa pointi moja, 31 huku Simba ikiwa na pointi 30, itabidi ifanye kazi ya ziada kuchukua pointi tatu mbele ya Majimaji yenye pointi 10 ambayo itapigana kutaka kujinasua kutoka mkiani inakoshikilia nafasi ya 11 kati ya timu 12.

Ugumu mwingine wa mpambano wa leo unatokana na sababu za kihistoria ambazo zinatueleza kuwa vijana hao kutoka Mitaa ya Jangwani na Twiga jijini Dar es Salaam mara nyingi wamekuwa wakiambulia matokeo mabaya wanapocheza katika dimba hilo la nyumbani la Majimaji.

Kocha wa Yanga, Fred Felix Minziro alisema juzi kabla ya kuondoka kuwa amewaambia wachezaji wake wajiepusha na kufikia matokeo yaliyopita bali wajipange kuhakikisha wanashinda mechi ya leo na nyingine zinazofuata.

"Kuna makosa madogo tumekuwa tunayafanya ambayo yamekuwa yanatugharimu, nimerekebisha hali hiyo lakini pia nimewaambia wachezaji wangu waache kufikiria matatizo mengine ya klabu bali watimize wajibu wao," alisema Minziro.

Kwa upande wake kocha wa Majimaji, Sebba Nkoma alisema kuwa hakuna namna ambayo Yanga inaweza kupita kuepuka kipigo licha ya kwamba atamkosa winga wake Ulimboka Mwakingwe ambaye ana kadi nyekukundu aliyoipata walipocheza na African Lyon mjini Morogoro.

Hata hivyo Nkoma alisema kazi ya Ulimboka amemkabidhi Mohamed Kijuso waliowaji kucheza pamoja Simba na kiungo Kasim Kilungo.

"Nasikitika kumkosa Ulimboka kwani leo ndio atakuwa anamaliza adhabu yake ya kadi nyekundu lakini si tatizo sana nashukuru nina safu nzuri sasa ya ushambuliaji kuna Kijuso na huyu Kilungo nina uhakika watafanya kazi vizuri," alisema Nkoma.
 
Choki ainyong'onyeza Twanga Pepeta


na Mwandishi wetu


BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo jana ilitangaza kuwachukua wanamuziki wanane kutoka The African Stars ‘Twanga Pepeta'.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ukumbi wa Rufita Sinza jijini Dar es Salaam, jana, Mkurugenzi wa Extra Bongo, Kamarade Ally Choki aliwataja nyota hao walionyakuliwa kutoka Twanga kuwa ni pamoja na Roggert Hegga ‘Caterpillar', Rapa Saulo John ‘Ferguson', wapiga magitaa Hosea Simon na God Kanuti aliyekuwa mkali wa Solo.
Wengine ni wanenguaji Mussa Hassan ‘Nyamwela' na Otilia Boniphace.
 
...Timbe atua Jangwani Friday, 04 February 2011 20:54

Vicky Kimaro
HATIMAYE klabu ya Yanga, imemtambulisha kocha mpya, Sam Timbe kuziba nafasi ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Kosta Papic aliyetimkia kwao baada ya migogoro ya hapa na pale ndani ya klabu hiyo.

Kocha huyo alitambulishwa jana kwa waandishi wa habari ofisini kwa mfadhili mkuu wa timu hiyo, Yusuf Manji jengo la Quality Plaza, Barabara ya Nyerere. Hata hivyo, alisema kuwa hajamalizana na Yanga kuinoa timu hiyo.

"Najua kuna mpasuko Yanga, viongozi hawaelewani, naomba tuwe marafiki tushirikiane, viongozi, wachezaji na mashabiki kwa ajili ya maendeleo ya Yanga, bila hivyo timu haiwezi kufanya vizuri," alisema Timbe.

Sam Timbe aliyeziongoza SC Villa na Polisi na kutwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati michuano iliyofanyika Tanzania mara zote, ataanza kuinoa timu hiyo kwa majaribio kabla ya kupewa mkataba wake.

Timbe alisema bado hawajamaliza na uongozi wa Yanga kuhusu mkataba wake na ameondoka jana kurudi Uganda na anatarajia kurejea nchini Jumapili na kuongoza jahazi la timu hiyo.

Kocha huyo wa Atraco alikuwa na ndoto kubwa za kunoa timu za Tanzania hususani Simba na Yanga na alidai kuwa bado anafanya mazungumzo na anatarajia yataenda vizuri, na iwapo watafanikiwa kusaini mkataba habari za ndani zinadai kuwa atasaini wa mwaka mmoja.

Timbe alikuwa akichuana na makocha Loly Baleto raia wa Uingereza aliyekuwa akifundisha soka nchini Zimbabwe, Ivo Ivan wa Slovakia, na kocha mwingine raia wa Yugoslavia.

Hata hivyo kikao kilichoketi juzi usiku kwenye hoteli ya Kilimanjaro Kenmpiski kati ya viongozi wa Yanga, kocha na mfadhili wao Yusuf Manji kilipitia vigezo na kuridhishwa na Timbe ambaye waliamua kumpitisha.

Kati ya vigezo ambavyo waliviangalia ni suala zima la mshahara, uzoefu na mafanikio katika timu mbalimbali alizofundisha.

Lakini jana akizungumza na Waandishi Timbe alisema "Kama tunafanya kazi tuwe pamoja sio kugawana wale wa huko, wale wa huku hatutapata mafanikio, lakini kama tukiungana mafanikio yatakuja tu,"alisema Timbe aliyewahi kuzinoa pia Vital'O ya Burundi, Atraco ya Rwanda na timu ya taifa ya wanawake ya Kuwait.

"Mimi ni mfanyakazi lakini maneno maneno waache, tuwe wamoja, wachezaji wanahitaji motisha ili wafanye vizuri kama vile mtoto anapoahidiwa zawadi basi itekelezwe, watajitaidi kwa kujua kuwa kuna zawadi wanapigania.

"Wachezaji wa Tanzania hawapendi mazoezi, mfano Bengo alikuja huku akawa hachezi mpira ni kwa vile alikuta mazoezi ya huku sio makali ingawa wao wanadhani wanafanya sana mazoezi, wachezaji wa Tanzania hawawezi kufurukuta kucheza nchi za nje angalau hapo Uganda kwa sababu hii wanatakiwa wapate mazoezi magumu.

Timbe ambaye ataungana na Yanga kesho alisema anaifahamu timu hiyo kwa vile amekuwa akiifuatilia kwa muda mrefu kwani hata kwenye mechi yao dhidi ya Dedebit ya Ethiopia aliiona na kugundua upungufu wake.

 
Mmiliki Palm Night Club matatizoni


na Sitta Tumma, Mwanza


JESHI la Polisi mkoani Mwanza limesema litamfikisha mahakamani muda wowote mmiliki wa baa na ukumbi wa muziki wa Palm, Nyakato Mecco, jijini hapa mara baada ya upelelezi wa jeshi hilo kukamilika.
Kauli hiyo ya Jeshi la Polisi, imekuja siku chache baada ya mmiliki huyo kukamatwa na polisi kituo kidogo cha Nyakato-Mwatex akidaiwa kuongoza kundi la watu wapatao 20 kisha kumvamia nyumbani kwake na kumjeruhi vibaya mfanyabiashara wa jijini Mwanza, Gibral Kamanga.
Kwa mujibu wa jeshi hilo, mmiliki huyo atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka juu ya tuhuma zinazomkabili na kwamba kamwe halitafumbia tabia za watu kama hao wanaovamia na kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.
Kaimu kamanda wa polisi mkoani hapa, Nonosius Komba, aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake kwamba, upelelezi wa tukio hilo bado ungali unaendelea.
"Jalada bado lipo kwa OCD wa kituo cha Nyakato na upelelezi unaendelea...lakini mimi nasema tukikamilisha upelelezi wetu huyu mtu tutamfikisha mahakamani kujibu mashtaka," alisema kamanda Komba huku akilaani uvamizi huo.
Mmiliki huyo anadaiwa kuongoza kundi hilo la watu 20 kisha kumvamia na kumjeruhi vibaya kichwani Kamanga na familia yake, Januari 31 mwaka huu, majira ya saa 11 alfajiri, wakati mfanyabiashara huyo alipokuwa akifanya mazoezi ya mwili nyumbani kwake Nyakato Mecco jijini Mwanza.
Baada ya kuvamiwa, Kamanga alikimbizwa katika hospitali ya mkoa, Sekou Toure, kwa ajili ya kupatiwa matibabu na kwamba mkewe, Mayasa Mbwana, naye alijeruhiwa kwenye mkono wa kushoto, magari mawili yalivunjwa vioo, mageti na vitu vingine kadhaa.
Katika hatua nyingine, wakazi wa eneo la Nyakato Mecco wameiomba serikali kuufunga ukumbi huo wa muziki wa Palm, kwani uko katikati ya makazi ya watu na umekuwa kero kubwa na uvunjifu wa amani na maadili.
Baadhi ya wakazi hao, Majaliwa Ahmed, Musa Ramadhan na Kapeji Donald, walisema ukumbi huo wa muziki umegeuka kero kubwa kutokana na kupigwa kwa muziki wa juu usiku kucha, huku baadhi ya vijana wakionekana kufanya ngono hadharani eneo la baa na ukumbi huo.
"Tunakerwa sana na hii Palm Night Club, kwa sababu usiku hatulali wala watoto wetu hawajisomei usiku sababu kelele ni nyingi. Pili usalama wa eneo hili ni mdogo sana na hii inatokana na baadhi ya vijana ambao ni wateja wake kuendesha vurugu na matusi ya nguoni, tunataka Palm ifungwe," alisema Kapeji.
Katika ombi hilo la wananchi, kamanda Komba alipoulizwa alisema kwa ufupi: "Kimsingi hakuna Night Club inayoruhusiwa kwenye makazi ya watu, kama ni kufungwa na ifungwe."
 
Mabao yamliza Samata
Friday, 04 February 2011 20:52

Jackson Odoyo

DAKIKA 90 zimemtoa machozi ya uhuzuni na furaha mshambuliaji wa timu ya Simba Mbwana Samata baada ya kuifungia timu yake mabao mawili wakati wa mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Afrika Lyon.

Samata ambaye juzi alikuwa kinara na nyota wa machezo huo aliiwezesha Simba kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya timu yake ya zamani ya Afrika Lyon.

Akizungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya mechi hiyo kumalizika, Samata alisema amepatwa na huzuni baada ya kuifunga timu yake iliyomkuza kisoka, lakini hakuwa na jinsi kwa sababu walikuwa wakihitaji ushindi.

"Tangu nilipoanza kucheza soka sijawahi kuwa na wakati mgumu katika maisha yangu kama ilivyonitokea leo (juzi) sikuwahi kufikiria kuwa ipo siku nitaifunga timu iliyonikuza kisoka,"alisema Samata.

Alisema,"Hatua ya kuifunga Afrika Lyon ni sawa na kumvua baba msuli kiunoni kwa sababu ndiyo timu iliyonilea na imenitoa kimasomaso mpaka hivi leo niko hapa, lakini sikuwa na jinsi kwa sababu Simba ilihitaji ushindi wa hali na mali na ndiyo nilichokifanya."

Alisema kabla ya kuingia uwanjani hakujua kuwa kocha atampa kazi ya kuiwezesha Simba kupata ushindi katika mechi hiyo kwa sababu Simba ina wachezaji wengi, lakini kitendo cha kupewa dakika 90 zilikuwa sahihi kwa kocha.

"Dakika 90 nilizopewa katika mechi hiyo zilikuwa sahihi kwa kocha, lakini kwangu ilikuwa ni huzuni na furaha ndiyo maana uliona hata aina ya ushangiliaji wangu ilikuwa ni huzuni zaidi, nilikuwa nikiona aibu kuwatizama mashabiki,viongozi na wachezaji wa Lyon waliokuwa katika benchi la ufundi,"alisema Samata.

"Hali hiyo iliongezeka nilipofunga magoli kwa ujumla kiasi kwamba nikalazimika kwenda kushangilia sehemu nyingine kwa aibu ili beachi la ufundi lisinione,"alisema Samata.

Pamoja na kwamba Simba ilihitaji ushindi ili ijiweke pazuri, lakini mchezaji huyo aliongeza kuwa,"badaa ya mechi nililazimika kwenda kuwaomba msaamaha viongozi na wachezaji wa Afrika Lyon."
 
Mabao yamliza Samata
Friday, 04 February 2011 20:52

Jackson Odoyo

DAKIKA 90 zimemtoa machozi ya uhuzuni na furaha mshambuliaji wa timu ya Simba Mbwana Samata baada ya kuifungia timu yake mabao mawili wakati wa mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Afrika Lyon.

Samata ambaye juzi alikuwa kinara na nyota wa machezo huo aliiwezesha Simba kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya timu yake ya zamani ya Afrika Lyon.

Akizungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya mechi hiyo kumalizika, Samata alisema amepatwa na huzuni baada ya kuifunga timu yake iliyomkuza kisoka, lakini hakuwa na jinsi kwa sababu walikuwa wakihitaji ushindi.

“Tangu nilipoanza kucheza soka sijawahi kuwa na wakati mgumu katika maisha yangu kama ilivyonitokea leo (juzi) sikuwahi kufikiria kuwa ipo siku nitaifunga timu iliyonikuza kisoka,”alisema Samata.

Alisema,"Hatua ya kuifunga Afrika Lyon ni sawa na kumvua baba msuli kiunoni kwa sababu ndiyo timu iliyonilea na imenitoa kimasomaso mpaka hivi leo niko hapa, lakini sikuwa na jinsi kwa sababu Simba ilihitaji ushindi wa hali na mali na ndiyo nilichokifanya.”

Alisema kabla ya kuingia uwanjani hakujua kuwa kocha atampa kazi ya kuiwezesha Simba kupata ushindi katika mechi hiyo kwa sababu Simba ina wachezaji wengi, lakini kitendo cha kupewa dakika 90 zilikuwa sahihi kwa kocha.

“Dakika 90 nilizopewa katika mechi hiyo zilikuwa sahihi kwa kocha, lakini kwangu ilikuwa ni huzuni na furaha ndiyo maana uliona hata aina ya ushangiliaji wangu ilikuwa ni huzuni zaidi, nilikuwa nikiona aibu kuwatizama mashabiki,viongozi na wachezaji wa Lyon waliokuwa katika benchi la ufundi,”alisema Samata.

“Hali hiyo iliongezeka nilipofunga magoli kwa ujumla kiasi kwamba nikalazimika kwenda kushangilia sehemu nyingine kwa aibu ili beachi la ufundi lisinione,”alisema Samata.

Pamoja na kwamba Simba ilihitaji ushindi ili ijiweke pazuri, lakini mchezaji huyo aliongeza kuwa,“badaa ya mechi nililazimika kwenda kuwaomba msaamaha viongozi na wachezaji wa Afrika Lyon.”
 
Liverpool, Torres wakamiana
Friday, 04 February 2011 20:48

LIVERPOOL, England
LIVERPOOL tayari imeshasahau kuondoka kwa Fernando Torres, anasema kocha Kenny Dalglish wakati kikosi chake kikijiandaa kuvaana na nyota huyo wa zamani akiwa na timu yake mpya ya Chelsea.

Nyota huyo wa Hispania anatarajiwa kuanza kuitumikia klabu yake mpya kesho watapocheza dhidi ya timu yake ya zamani kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, huku kocha Dalglish akionyesha kuhuzunika kwa kumwachia mshambuliaji huyo.

"Kila moja amehuzunika kuondoka kwake, lakini kinachooumiza zaidi ni muda alioondoka, lakini maisha lazima yaendelee," Dalglish aliwaambia wanahabari alipoulizwa kuhusu kumwachia Torres kwa pauni 50 milioni.

"Sitajali nacheza na timu gani, kazi yangu itakuwa ni kufanya kazi kwa uadilifu, lengo ni kiona Chelsea inafanikiwa, naamini nitafunga mabao ya kutosha," alisema Torres.

Torres ana rekodi ya mabao saba katika mechi nane ikiwa ni pamoja na yale aliyoyafunga wakati Liverpool ilipoishinda Chelsea mabao 2-0 katika Uwanja wa Anfield, Novemba mwaka jana.

"Awali nilipokuwa nikicheza dhidi ya Chelsea, nilikuwa nikijitahidi sana, huwa ni mechi ngumu. Hiyo ndio sababu iliyonifanya nitamani kujiunga na Chelsea, nataka kuwemo katika timu ngumu."

"Chelsea ipo katika nafasi ya nne nyuma ya vinara Manchester United kwa pointi 10, ni wazi itataka kupanda. Kocha Carlo Ancelotti alisema: "Tutamjaribu katika mechi ya kesho."

Lakini pengo la Torres katika klabu ya Liverpool tayari limezibwa na Luis Suarez, ambaye alifunga bao katika mechi yake ya kwanza wakati Liverpool ilipoifunga Stoke City mabao 2-0 na jambo hilo limemfanya kocha Kenny Daglish afikishe ushindi mara tatu na sare moja tangu alipojiunga na klabu hiyo kuchukua nafasi ya Roy Hodgson.

Kwa upande mwingine, Manchester United itasafiri kwenda kupambana na Wolves leo. Nyota Wayne Rooney alifunga mabao mawili katika mechi dhidi ya Aston Villa katikati ya wiki, hiyo inawafanya watu waamini ameanza kurudi katika hali yake ya awali.

Kama nyota wa Alex Ferguson wataepuka kipigo wataweka rekodi ya klabu kwa kutofungwa katika mechi 30. Na huenda wakafanikiwa kwani wana ari kufuatia ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Aston Villa.

Arsenal, ambayo ipo nyuma ya vinara kwa pointi tano itataka kuongeza presha kwa Manchester United wakati itakapocheza na Newcastle ambayo bado inaomboleza kuondoka kwa Andy Carroll aliyetua Liverpool kuchukua nafasi ya Torres.
Manchester City iliyo katika nafasi ya tatu itategemea kuona nyota mpya Edin Dzeko akishirikiana na Tevez katika kufanya mambo makubwa wakati watakapoikaribisha West Bromwich Albion leo .
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…