Sevilla inakaribia kumsajili winga wa Uholanzi Quincy Promes, mwenye miaka 26, kutoka Spartak Moscow katika mkataba wa thamani ya Euro milioni 20. (AS)
Aliyekuwa mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast Yaya Toure, mwenye miaka 35, anakaribia kukamilisha uhamisho wake kurudi Olympiakos. (Mirror)
Mshambuliaji wa Ubelgiji Divock Origi, 23, anatarajiwa kuondoka Liverpool kabla ya muda wa mwisho wa uhamisho Ulaya huku Besiktas ikiwa miongoni mwa vilabu vinavyomuwania mchezaji huyo. (Liverpool Echo)