The Tomorrow People
JF-Expert Member
- Jul 11, 2013
- 2,675
- 2,807
Ha ha ha KOMBOLELA, kuna Signature ya mdau mmoja inasema "Butua uwakomboe wenzio" so funny. ila sasahivi sidhani kama hii michezo bado ipo.
kuna mchezo ulikuwa unaitwa malede(kwa wanawake) na nilikuwa napenda sana ule mchezo wa baba na mama au mnachanga hela ikifika ijumaa mnafanya harusi,mnamchagua mmoja wa kike kama bi harusi na wakiume bwana harusi,mnapika pilau mnaimba. hadi raha.
duu...bwana baba mi nakumbuka selemko...kwa wale waliokulia mbeya hii jambo inafahamika kufuatana na geographical location yake...baaasi nmechana sana nguo na kikubwa kuvunjika baada ya mgomba nlioupanda kutoka mabako yote na kiniacha katikati ya safari....loooooo ilikua ni kuburuta makalio mpaka mtoniii....!!!
huu uzi nimeugumia leo, dah ndugu zangu mumenikumbusha mbali sana. maana hiyo michezo yote muliyoitaja nimeipitia.
Ila mumesahau kupiga kigoma cha daku mwezi wa ramadhani.
Tulikuwa tukiwaita fukufuku.aah nakumbuka kuna wadudu tulikuwa tunafukua ardhini then tunaweka kwenye manyonyo ili yakue haraka
Habari zenu wana JF,
Katika pitapita zangu nikaliona gari limeandikwa Utoto mtamu, basi nikakumbuka tulivyokua tunacheza kombolela. Je, mwenzangu ni michezo gani uliicheza utotoni?