TPA
Member
- Sep 28, 2016
- 49
- 71
Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng. Deusdedit Kakoko akizungumza na Wafanyakazi wakati wa kufungua michezo ya Bandari ambayo imeanza kutimua vumbi jijini Tanga Disemba 15 katika viwanja vya 'Harbors Club' na Shule ya Sekondari ya Popatlal .
Eng. Kakoko akikagua timu ya mpira wa soka wakati wa uzinduzi wa michezo hiyo.
Eng. Kakoko akibadilishana mawazo na baadhi ya viongozi wa timu na watendaji wa Bandari ya Tanga.
Eng. Kakoko na meza kuu wakiwapungia wachezaji wakati wakiingia uwanjani kuanza michezo ya "Inter-Ports-2016" jijini Tanga.
Timu wenyeji wa michezo ya mwaka huu Bandari ya Tanga ikiingia uwanjani kwa ukakamavu.
Baadhi ya Viongozi wa DOWUTA na Menejimenti ya Tanga wakibadilisha mawazo wakati wa ufunguzi wa michezo.
Timu wawakilishi kutoka Bandari za Maziwa za Mwanza, Kigoma na Kyela.
Timu ya Michezo kutoka Makao Makuu nao hawakubaki nyuma.
Mabingwa waliopita Bandari ya Dar es Salaam nao wamejipanga kuhakikisha wananyakuwa kikombe cha ushindi wa jumla kwa 'Inter-Ports Games 2016'.