Midomo yangu inakauka na kupasuka

Midomo yangu inakauka na kupasuka

PlayBoyMwema

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2014
Posts
1,714
Reaction score
1,829
Habari wadau samahani naomba msaada wenu nina tatizo la kukauka na kupasuka lips zangu za midomo kiasi kwamba napata maumivu.. Je kuna tiba yoyote kwa tatizo hili??

Nawasilisha...!!!
 
paka Asali , hafu baada ya wiki moja njoo pm unipe mrejesho
 
Paka mafuta au lip balm pia kunywa maji mengi angalau lita 2 kwa siku
 
Habari wadau samahani naomba msaada wenu nina tatizo la kukauka na kupasuka lips zangu za midomo kiasi kwamba napata maumivu.. Je kuna tiba yoyote kwa tatizo hili??

Nawasilisha...!!!

DRY MOITH.jpg
MATUNDA.jpg
MAJI.jpg



UFANYE KITU GANI ILI UJITIBU MARADHI YA MDOMO KUWA MKAVU?

UKAVU katika midomo ni tatizo, ambalo huwakabili watu wengi bila kujali jinsia wala umri.
Pamoja na kuonekana ni la kawaida, lakini hukosesha raha na kumfanya mtu ajihisi kupoteza mvuto wake.

Watu wa jinsia zote hasa wafuatiliaji wa masuala ya urembo na utanashati, huangaika mara kwa mara kutafuta njia au dawa inayoweza kuwasaidia kuondokana na tatizo hili, bila kujua nini chanzo.
Tatizo hili husababishwa na mambo kadha wa kadha, kubwa zaidi likiwa ni hali ya hewa, upepo mkali huchangia kwa kiasi kikubwa kukauka kwa midomo, hatimaye kupasuka kabisa kama hakutafanyika lolote kukabiliana na kero hiyo.

Sababu nyingine zinazoweza kuchangia kutokea kwa tatizo hili ni matumizi ya dawa, maambukizi katika midomo, matumizi ya vipodozi vyenye kemikali, kukosekana kwa virutubisho mwilini pamoja na magonjwa ya ngozi.

Namna ya kufanya
Zipo njia mbalimbali za asili, rahisi na ambazo zinaweza kukabilana na tatizo hili kwa kukinga, kupunguza na hata kumaliza kabisa ukavu wa midomo, endapo zitafuatwa na kutumika kwa usahihi.

Zifuatazo ni miongoni mwa njia hizo.
Unywaji wa maji
Pamoja na kukabiliana na tatizo hili maji yana umuhimu mkubwa katika mwili wa binadamu.
Katika hali ya kawaida, upungufu wa maji unaweza kuchangia kwa namna moja au nyingine kutokea kwa tatizo hilo.

Ni vyema binadamu kunywa maji yasiyopungua lita tano kwa siku, hiyo itachangia kulainisha siyo midomo tu, bali ngozi ya mwili mzima kwa ujumla.

Matunda na mboga za majani
Matunda pia hususani yenye maji maji kama karoti, matango, nyanya na matikiti yanaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kukinga au kukabiliana na tatizo hili.
Unaweza kula matunda hayo yakiwa hivyo au kwa kutengeneza juisi. Mboga za majani pia kama mchicha na spinachi unaweza kuchemsha na kunywa maji yake.

Matumizi ya lipbam
Umakini unahitajika katika uchaguzi wa mafuta ya kutumia mdomoni. Ni vyema zaidi yakatumika mafuta yenye ladha ya matunda ya kawaida na kuachana na zile zenye kemikali.

Ukiwa na Swali au tatizo lolote usikose kunitafuta kwa kubonyeza hapa.Kwa mawasiliano;
MziziMkavu
Barua pepe: fewgoodman@hotmail.com
Simu (Whatsapp) +90 534 450 8169
 
Back
Top Bottom