Mifumo ya malipo ya bidhaa kwa njia ya simu na fao la dharura

Mifumo ya malipo ya bidhaa kwa njia ya simu na fao la dharura

Samwel Ngulinzira

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2017
Posts
1,829
Reaction score
1,972
Asalam aleykum!

Bila kupoteza muda naomba tujadili hili suala kama dharura.

Ninaomba TCRA, BoT na mitandao ya simu watengeneze haraka mfumo wa malipo kwa njia ya simu.

Huduma kama lipa kwa M-Pesa, Airtel Money, T-Pesa, Halo Pesa, Tigo Pesa na Ezzy Pesa ili tuepuke matumizi ya pesa taslimu inayoweza kupelekea kusambaa kwa ugonjwa wa corona.

Simu za wafanyabiashara wadogo na wakubwa ziwezeshwe kupokea malipo kwa njia ya simu kama ilivyo kwenye Master Card.

Jambo la pili napendekeza mifuko ya jamii iandae fao la dharura kwa waajiriwa na wanachama wa hiari.

Fao hili liwe maalum kwa wale ambao shughuli zao zitakwamishwa na ugonjwa wa Corona kwa namna moja au nyingine waweze kujikimu kama itatokea tukapewa tangazo la kutokutoka nje.

Kuna maeneo kama utalii, shule, mabenki, kumbi za mikutano, kumbi za sherehe, nyumba za ibada na supermarket zitapata madhara makubwa kwa kua ndiyo maeneo ambayo yanategemea uwepo wa watu ili kutengeneza vipato vya wafanyakazi na wamiliki.

Hivyo kama hali ya kufunga shule na nyumba za ibada itatokea ulipaji wa mishahara pia utakua mgumu hivyo itabidi mifuko ya jamii iwapatie wafanyakazi fao la kujikimu ili waweze kujikimu mpaka hali itakapokua sawa.

Kwa hayo machache naomba kuwasilisha.
 
Point yako nzuri sana. Itakuwa suala la msingi kama huduma hii itaendana na kupunguza kiwango cha makato ya kutoe fedha.

Mathalani mitandao karibu yote unapotoa laki 5 makato ya kutolea ni zaidi ya 7,000 wakati kwenye ATM ni kati ya 700-1000 kwa kila unapotoa fedha.

Sijui ni mamlaka gani inaratibu hizi withdrawal charges tunazokatwa na makampuni kushirikana na mawakala wao.

Kwa mtu anaelipia kwa scanned QR Code withdrawal charges ni 0; hata ingekuwa 500 but less than 1000 sio mbaya.

Kama wazo lako litafanyiwa kazi, wazingatie udhibiti wa withdrawal charges.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Point yako nzuri sana. Itakuwa suala la msingi kama huduma hii itaendana na kupunguza kiwango cha makato ya kutoe fedha.

Mathalani mitandao karibu yote unapotoa laki 5 makato ya kutolea ni zaidi ya 7,000 wakati kwenye ATM ni kati ya 700-1000 kwa kila unapotoa fedha.

Sijui ni mamlaka gani inaratibu hizi withdrawal charges tunazokatwa na makampuni kushirikana na mawakala wao.

Kwa mtu anaelipia kwa scanned QR Code withdrawal charges ni 0; hata ingekuwa 500 but less than 1000 sio mbaya.

Kama wazo lako litafanyiwa kazi, wazingatie udhibiti wa withdrawal charges.

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukrani mkuu...kama nilivyopendekeza hapo juu huduma hii wapatiwe wauza bidhaa na watoa huduma ili tuepuke kutumia pesa.
Noti 1 inaweza kushikwa na mikono 100 ndani ya masaa machache.
Wakati tukitangaza kujihami na ugonjwa huu ni vyema tukaanza kuepuka matumizi ya pesa taslimu.
Inasambaza virusi kwa kasi kuliko kawaida.
Najaribu kujiuliza pesa alizolipwa yule mama mwenye Korona imepita kwenye mikono ya watu wangapi, nkabaki nasikitika.
Nadhani serikali itachukua hatu kabla hali haijawa mbaya zaidi.
 
Back
Top Bottom