Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Mpo salama bila shaka.
Inapotokea migomo ya nyakati hizi kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ni muhimu kuiendea kwa umakini.
Wanasiasa wanaelewa nazungumzia nini.
Watatuzi wa migomo lazima wawe na ujuzi, uwezo na hekima za kuongea mbele za Watu.
Sio unachagua mtu asiye na ujuzi wa mambo hayo anaanza kuropoka ropoka na kutia chumvi kwenye kidonda.
Kizazi cha sasa sio kile kizazi cha wajinga ambao unaweza kutisha tisha Watu kama watoto ilhali Watu wanahitaji haki fulani. Uelewa na elimu ya kizazi hiki imeongezeka maradufu hivyo hata mbinu za kudili na wananchi lazima ziwe za kisomo na uelewano.
Kwenye ulimwengu huu wenye vitisho bila kutumia akili na maarifa hawadumu hata ungekuwa na cheo kikubwa kiasi gani.
Kwanza unatisha wanaume wenzako hiyo kama sio dharau ni nini? Mtu hafanyi uhalifu anahitaji marekebisho kuhusu jambo fulani wewe kwa akili zako za kizamani unakuja kutisha Watu. Unafikiri wewe ni nani hasa? Na hivyo unavyojifikiria unadhani kila mtu anakuona hivyo.
Heshimu Watu ili uheshimiwe.
Kuna Watu wanaushamba fulani wa kizamani. Hata raia wa kawaida unakuta mtazamo wake upo kizamani.
Hawa ndio wakipewa kinafasi na kicheo fulani wanaanza kuumiza Watu.
Elewa, hukohuko serikalini kuna Watu ni Open minded ambao mitazamo yao ipo kisasa na sio kizamani.
Elewa, wale unaodhani wanakulinda wapo mitazamo yao sio yakizamani.
Unapokuwa mtawala au kiongozi usiwe mjinga. Angalia nyakati ulizomo. Hiyo ipo hata katika ngazi ya familia. Baba ukiwa mpumbavu na mbabe mbabe elewa usaliti unaweza kufanywa hata na mtoto wako uliyemzaa. Sasa ikiwa mtoto au mkeo anaweza fanya hayo sembuse Watu back wanaokulinda kwa kisa cheo.
Viongozi wenye hekima hujua namna ya kuchagua maneno ya kuongea mbele za Watu.
Mihemko huiweka mbali. Ishu ya vitisho huweza kuwa indirect au field lakini mbele za Watu hutumia lugha ya hekima
Adui wa mbali ndio hutolewa mikwala na kufanyiwa ubabe. Lakini kuwapa mikwala wananchi na kuwafanyia ubabe Watu wako. Kimedani Umefeli.
Elewa, mtu mzima kumfanyia ubabe ni kumdhalilisha. Tena ubabe kwa haki yake. Alafu uchukulie itaisha au atasamehe utakuwa haufikirii vizuri.
Wanaokemewa ni wahalifu. Wanaokemewa ni waovu.
Hivyo ndivyo ilivyo.
Vijana wenye ndoto za kuwa viongozi ni hayo tuu.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Inapotokea migomo ya nyakati hizi kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ni muhimu kuiendea kwa umakini.
Wanasiasa wanaelewa nazungumzia nini.
Watatuzi wa migomo lazima wawe na ujuzi, uwezo na hekima za kuongea mbele za Watu.
Sio unachagua mtu asiye na ujuzi wa mambo hayo anaanza kuropoka ropoka na kutia chumvi kwenye kidonda.
Kizazi cha sasa sio kile kizazi cha wajinga ambao unaweza kutisha tisha Watu kama watoto ilhali Watu wanahitaji haki fulani. Uelewa na elimu ya kizazi hiki imeongezeka maradufu hivyo hata mbinu za kudili na wananchi lazima ziwe za kisomo na uelewano.
Kwenye ulimwengu huu wenye vitisho bila kutumia akili na maarifa hawadumu hata ungekuwa na cheo kikubwa kiasi gani.
Kwanza unatisha wanaume wenzako hiyo kama sio dharau ni nini? Mtu hafanyi uhalifu anahitaji marekebisho kuhusu jambo fulani wewe kwa akili zako za kizamani unakuja kutisha Watu. Unafikiri wewe ni nani hasa? Na hivyo unavyojifikiria unadhani kila mtu anakuona hivyo.
Heshimu Watu ili uheshimiwe.
Kuna Watu wanaushamba fulani wa kizamani. Hata raia wa kawaida unakuta mtazamo wake upo kizamani.
Hawa ndio wakipewa kinafasi na kicheo fulani wanaanza kuumiza Watu.
Elewa, hukohuko serikalini kuna Watu ni Open minded ambao mitazamo yao ipo kisasa na sio kizamani.
Elewa, wale unaodhani wanakulinda wapo mitazamo yao sio yakizamani.
Unapokuwa mtawala au kiongozi usiwe mjinga. Angalia nyakati ulizomo. Hiyo ipo hata katika ngazi ya familia. Baba ukiwa mpumbavu na mbabe mbabe elewa usaliti unaweza kufanywa hata na mtoto wako uliyemzaa. Sasa ikiwa mtoto au mkeo anaweza fanya hayo sembuse Watu back wanaokulinda kwa kisa cheo.
Viongozi wenye hekima hujua namna ya kuchagua maneno ya kuongea mbele za Watu.
Mihemko huiweka mbali. Ishu ya vitisho huweza kuwa indirect au field lakini mbele za Watu hutumia lugha ya hekima
Adui wa mbali ndio hutolewa mikwala na kufanyiwa ubabe. Lakini kuwapa mikwala wananchi na kuwafanyia ubabe Watu wako. Kimedani Umefeli.
Elewa, mtu mzima kumfanyia ubabe ni kumdhalilisha. Tena ubabe kwa haki yake. Alafu uchukulie itaisha au atasamehe utakuwa haufikirii vizuri.
Wanaokemewa ni wahalifu. Wanaokemewa ni waovu.
Hivyo ndivyo ilivyo.
Vijana wenye ndoto za kuwa viongozi ni hayo tuu.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam