LGE2024 Mikoa 5 yavunja rekodi kujiandikisha uchaguzi wa TAMISEMI 2024 asema waziri Mohamed Mchengerwa

LGE2024 Mikoa 5 yavunja rekodi kujiandikisha uchaguzi wa TAMISEMI 2024 asema waziri Mohamed Mchengerwa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
20 October 2024

Mikoa yavunja rekodi kujiandikisha uchaguzi wa TAMISEMI 2024
Mikoa mitano ya Tanganyika iliyoongoza nchini Tanzania ni kama ifuatavyo :
  1. Tanga asilimia 101.13 ya lengo ,
  2. Pwani 98.74% ya lengo ,
  3. Mwanza 94.09%, ya lengo
  4. Dar es Salaam 86.66% ya lengo
  5. na Dodoma 80.63% ya lengo
Mikoa hiyo hapo juu ndiyo yaongoza asema ndugu Mohamed Mchengerwa ambaye ni waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hakutakuwa na siku ya nyongeza ikifika saa 12 jioni itakuwa mwisho wa uandikishwaji, na hakuna siku za nyongeza kuandikisha wapiga kura katika daftari ya wapiga kura wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji .

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa ametoa tathimini ya uandikishaji katika daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali Mitaa huku akitaja mikoa mitano vinara wa kuandikisha.

Mchengerwa ametoa tathimini hiyo leo Oktoba 20, 2024 akiwa katika Tarafa ya Ikwiriri, Rufiji mkoani Pwani.













Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mohammed Mchengerwa amefunga zoezi la kujiandikisha kupiga kura na kutoa taarifa ya siku Tisa ya waliojitokeza kujiandikisha nchini ambapo Watanzania zaidi ya milioni 26 wamejiandikisha sawa na asilimia 81.15 ya Watanzania wamejiandikisha.




Mheshimiwa Mchengerwa amejiandikisha katika kituo cha uandikishaji cha Umwe Mchikichini kilichopo Jimboni kwake Ikwiriri Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani ambapo alitumia nafasi hiyo kuzungumza na wananchi na waandishi wa habari jimboni kwake mara baada ya kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura na kumesema kuwa zoezi hilo litafungwa ifikapo saa12 jioni leo.



Mhe.Mchengerwa amesema kuwa taarifa ya jumla itatolewa ifikapo saa sita usiku leo muda hautaongezwa.



"Amewapongeza wananchi kwa kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la mpigakura kote nchini ambapo waliojiandikisha kwa mujibu wa taarifa ya awali ni asilimia hizo 81. 15


"Mtakumbuka kuwa kwa muda wa siku 9 sasa toka tarehe 11 Oktoba, 2024 Wasimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wamekuwa katika zoezi la kuandikisha Watanzania watakaoshiriki zoezi la upigaji kura kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa itakapofika tarehe 27 Novemba, 2024. Uandikishaji huu unafanyika kwa muda wa siku 10 hadi tarehe 20 Oktoba, 2024" alisema Mchengerwa.



Alisema uandikishaji na maandalizi ya orodha ya wapiga kura wa Uchaguzi wa Mamlaka za Serikali za Mita ni takwa mojawapo la Kanuni za Uchaguzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa za mwaka 2024.



"Kanuni hizo zinaelekeza kuwa kutakuwa na orodha ya wapiga kura ambayo itatumika katika uchaguzi wa kuwachagua mwenyekiti wa Kijiji, mwenyekiti wa mtaa, mwenyekiti wa kitongoji na wajumbe wa serikali za vijiji na kamati za mitaa" alisema.



"Nimeona nikutane nanyi ili kuwafahamisha Watanzania kuhusu mwenendo wa uandikishaji huo hadi kufikia siku ya 9 tarehe 19 Oktoba, 2024 na kutoa wito kwa Watanzania ambao hawajajitokeza kujiandikisha watumie siku ya leo ambayo pia ni siku ya mapumziko" alisema.



"Jumla ya wapiga kura 26,769,995 wamejiandikisha kupiga kura sawa na asilimia 81.15 ya lengo la kuandikisha watu 32,987,579 kwa siku zote 10 ambapo wanaume ni 13,033,988 sawa na asilimia 48.69 ya watu wote waliojiandikisha kwa tarehe 11-19 Oktoba, 2024 na wanawake ni 13,736,007 sawa na asilimia 51.31 ya watu wote waliojiandikisha"



"Kwa ujumla, mwenendo huu ni mzuri sana, na kama utaendelea hivi kwa siku ya leo, uwezekano wa kufikia malengo ya uandikishaji ni mkubwa. Hii ni kwa kuwa kuanzia siku ya 5 hadi ya 9 kumekuwa na kuongezeka kwa idadi ya Watanzania waliojitokeza kujiandikisha

Siku ya 5 tarehe 16 Oktoba, 2024 waliandikishwa jumla ya wapiga kura 2,460,664 sawa na asilimia 7.46 ya lengo la siku" alisema.



"Siku ya 6 tarehe 16 Oktoba, 2024 waliandikishwa jumla ya wapiga kura 2,472,605 sawa na asilimia 7.50 ya lengo la siku; siku ya 7 tarehe 17 Oktoba, 2024 waliandikishwa jumla ya wapiga kura 2,971,219 sawa na asilimia 9.01 ya lengo la siku; Siku ya 8 tarehe 18 Oktoba, 2024 waliandikishwa jumla ya wapiga kura 3,409,211 sawa na asilimia 10.33 ya lengo la siku; siku ya 9 tarehe 19 Oktoba 2024 waliandikishwa jumla ya wapiga kura 3,813,999 sawa na asilimia 115.6 ya lengo la siku



Soma Pia:
Taarifa ya nchi nzima kuhusu mikoa yote iliyotekeleza zoezi la uandikishwaji katika daftari la mpiga kura maalum kwa ajili ya Uchaguzi wa November 2024 itatolewa leo saa Sita Usiku wa manane tarehe 20 October 2024
 
mtaji wa ccm ni wasukuma pwani,tanga,dodoma
Hawa siyo kweli huwa wanatoa wapinzani sn, Tanga, Dodoma na Pwani hazijawahi kutoa wapinzani ndiyo mikoa ya watu wajinga na masikini, fanya research ndogo, maza muda mwingi anatumia Mwanza sababu anajua hana ushawishi na wasukuma hawaitaki CCM hasa kuongozwa na mwanamke ndiyo kabisa, kumteua Doto ni mkakati wa kuwaridhisha wasukuma + miradi mingi anapeleka Mwanza makusudi
 
20 October 2024

Mikoa yavunja rekodi kujiandikisha uchaguzi wa TAMISEMI 2024

View: https://m.youtube.com/watch?v=HeTN8FebJdw
Mikoa mitano ya iliyoongoza nchini Tanzanoa ni kama ifuatavyo :
  1. Tanga asilimia 101.13 ya lengo ,
  2. Pwani 98.74% ya lengo ,
  3. Mwanza 94.09%, ya lengo
  4. Dar es Salaam 86.66% ya lengo
  5. na Dodoma 80.63% ya lengo
Mikoa hiyo hapo juu ndiyo yaongoza asema ndugu Mohamed Mchengerwa ambaye ni waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hakutakuwa na siku ya nyongeza ikifika saa 12 jioni itakuwa mwisho wa uandikishwaji, na hakuna siku za nyongeza kuandikisha wapiga kura katika daftari ya wapiga kura wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji .

Taarifa ya nchi nzima kuhusu mikoa yote iliyotekeleza zoezi la uandikishwaji katika daftari la mpiga kura maalum kwa ajili ya Uchaguzi wa November 2024 itatolewa leo saa Sita Usiku wa manane tarehe 20 October 2024

Asilimia 101? Kwamba Kuna wapiga kura wengi kuliko waliotarajiwa? How? Waooh!
 
Asilimia 101? Kwamba Kuna wapiga kura wengi kuliko waliotarajiwa? How? Waooh!

Wamejitokeza kwa kishindo kisichotarajiwa kitakwimu

TOKA MAKTABA:

IJUMAA 14 JUNE 2024
Tanga, Tanzania

MATUMIZI YA SENSA YA TAIFA NA CHAMA DOLA KONGWE CCM

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimewataka viongozi na watendaji wa chama hicho kuongeza umakini katika zoezi la usajili wa wanachama kieltroniki na utoaji wa kadi kwa lengo la kuzuia usajili holela wa watu ambao wanasajiliwa kwa ajili ya kura za maoni tu. .

Tahadhari hiyo imetolewa na Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Selemani Sankwa alipokuwa akifunga mafunzo ya siku moja ya Sensa ya Watu na Makazi kwa ajili ya wajumbe wa Baraza la Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT), Mkoa wa Tanga. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Usagara, jijini Tanga.

Sankwa alisema kuwa hivi sasa kuna watu wanawania kugombea nafasi mbali mbali za uongozi katika chaguzi mbalimbali, hivyo wasipokuwa makini kuna watu watapata kadi kiholela na huku Katibu wa Tawi au wa Wilaya akiwa hajui,

“Watu hao ni wale ambao baada ya kura za maoni wanarudisha kadi kwa wapinzani wakidai wamejitoa CCM,” alisema na kuahidi kuwa wanafuatilia zoezi hilo kwa karibu na kuhakiki kadi hizo ili kusiwe na utoaji wa kadi kiholela.

Akizungumzia kwa ujumla juu ya zoezi la usajili wa wananchama kieletroniki alisema kuwa bado zoezi hilo halijakuwa la kuridhisha.

“Tunalenga kusajili wanachama 100,000 ifikapo mwisho wa mwaka huu na tumesajili wanachama 27,000 hadi mwezi Machi,” alieleza.

Aliwataka viongozi wote kupanga mikakati ya kuongeza simu za usajili ili kuongeza kasi ya usajili. Akaeleza kuwa wanafuatilia kwa ukaribu zoezi hilona kila siku matokeo ya usajili yanawekwa katika Group la Whatsap ya Halmashauri Kuu ya Mkoa.

Alisema kuwa wilaya za Handeni, Muheza na Lushoto zimekuwa zikifanya vizuri, lakini kwa mwezi Mei, Tanga wamefanya vizuri kwa kusajili wanachama 1,000.

Pia aitoa wito mahususi kwa viongozi na watendaji wa UWT kupanga mikakati ya kuongeza simu kwa ajili ya kuongeza kasi ya usajili wa wanachama.

Sankwa pia aliwataka viongozi wote waliopata mafunzo kuhakikisha waliyojifunza yanafika ngazi ya chini. Alisema kuwa kuanzia wiki inayokuja Kamati ya Utengaji ya mkoa itaanza ziara kwa jili kuhakiki zoezi hilo.

Aliwahimiza kuwahamasisha watu wajitokeze kwa wingi katika zoezi la kuboresha na kujiandika kaika daftaril a wapiga kura wsikose haki ya kuchagua viongozi katika ngazi mbalimbali .Katibu wa UWT wa Mkoa wa Tanga, Aziza Hussein Kiduda alisema kuwa wamepanga kusajili wanachama 300,000 hadi kufikia mwisho wa mwaka huu.

Alisema hadi hivi sasa wamekwishasajil wanachama 3,528 na wanategemea kuongeza kasi ya usajili ili wafikie lengo walilojiwekea.

Hate hivyo katibu huyo aliwapomgeza wa bunge wa viti maalum mkoa wa Tanga kwa kugawa simu kwaajili ya usajili wa wanachama.





 
Wamejitokeza kwa kishindo kisichotarajiwa kitakwimu

TOKA MAKTABA:

IJUMAA 14 JUNE 2024
Tanga, Tanzania


MATUMIZI YA SENSA YA TAIFA NA CHAMA DOLA KONGWE CCM

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimewataka viongozi na watendaji wa chama hicho kuongeza umakini katika zoezi la usajili wa wanachama kieltroniki na utoaji wa kadi kwa lengo la kuzuia usajili holela wa watu ambao wanasajiliwa kwa ajili ya kura za maoni tu. .

Tahadhari hiyo imetolewa na Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Selemani Sankwa alipokuwa akifunga mafunzo ya siku moja ya Sensa ya Watu na Makazi kwa ajili ya wajumbe wa Baraza la Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT), Mkoa wa Tanga. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Usagara, jijini Tanga.

Sankwa alisema kuwa hivi sasa kuna watu wanawania kugombea nafasi mbali mbali za uongozi katika chaguzi mbalimbali, hivyo wasipokuwa makini kuna watu watapata kadi kiholela na huku Katibu wa Tawi au wa Wilaya akiwa hajui,

“Watu hao ni wale ambao baada ya kura za maoni wanarudisha kadi kwa wapinzani wakidai wamejitoa CCM,” alisema na kuahidi kuwa wanafuatilia zoezi hilo kwa karibu na kuhakiki kadi hizo ili kusiwe na utoaji wa kadi kiholela.

Akizungumzia kwa ujumla juu ya zoezi la usajili wa wananchama kieletroniki alisema kuwa bado zoezi hilo halijakuwa la kuridhisha.

“Tunalenga kusajili wanachama 100,000 ifikapo mwisho wa mwaka huu na tumesajili wanachama 27,000 hadi mwezi Machi,” alieleza.

Aliwataka viongozi wote kupanga mikakati ya kuongeza simu za usajili ili kuongeza kasi ya usajili. Akaeleza kuwa wanafuatilia kwa ukaribu zoezi hilona kila siku matokeo ya usajili yanawekwa katika Group la Whatsap ya Halmashauri Kuu ya Mkoa.

Alisema kuwa wilaya za Handeni, Muheza na Lushoto zimekuwa zikifanya vizuri, lakini kwa mwezi Mei, Tanga wamefanya vizuri kwa kusajili wanachama 1,000.

Pia aitoa wito mahususi kwa viongozi na watendaji wa UWT kupanga mikakati ya kuongeza simu kwa ajili ya kuongeza kasi ya usajili wa wanachama.

Sankwa pia aliwataka viongozi wote waliopata mafunzo kuhakikisha waliyojifunza yanafika ngazi ya chini. Alisema kuwa kuanzia wiki inayokuja Kamati ya Utengaji ya mkoa itaanza ziara kwa jili kuhakiki zoezi hilo.

Aliwahimiza kuwahamasisha watu wajitokeze kwa wingi katika zoezi la kuboresha na kujiandika kaika daftaril a wapiga kura wsikose haki ya kuchagua viongozi katika ngazi mbalimbali .Katibu wa UWT wa Mkoa wa Tanga, Aziza Hussein Kiduda alisema kuwa wamepanga kusajili wanachama 300,000 hadi kufikia mwisho wa mwaka huu.

Alisema hadi hivi sasa wamekwishasajil wanachama 3,528 na wanategemea kuongeza kasi ya usajili ili wafikie lengo walilojiwekea.

Hate hivyo katibu huyo aliwapomgeza wa bunge wa viti maalum mkoa wa Tanga kwa kugawa simu kwaajili ya usajili wa wanachama.





Makadirio yanafanywa kutokana na sensa, rate ya kuzaliana, rate ya uhamiaji. So unataka kusema walikadiri vibaya? Watoe takwimu za walitaka watu wangapi, waepata wangapi na mkoa una watu wangapi?
 
Gerrymandering ni kutengeneza mipaka ya majimbo bunge mengi, mitaa, vitongoji kwa kuweka mipaka / au wingi lengo ili kuhakikishia kupata wabunge, madiwani, wenyeviti wa mitaa, vitongoji na vijiji wengi na kushinda uchaguzi.

MICHEZO MICHAFU YA KUHONGA NA KUGAWA MIPAKA YA MAJIMBO

Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Tundu Antipas Lissu kwa mifano hai ya michezo ngazi ya jimbo akiangalia mgawanyo wa majimbo yenye watu wengi zaidi anagundua kuwa haiwakilishi na idadi inayostahili ya wabunge. Wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam Mwanzo

Mfano mkoa wa Dar es Salaam ulitakiwa kuwa na wabunge wasiopungua 25. Lakini una wabunge wachache sana wakati ina idadi kubwa ya wapiga kura .

Mkoa wa Lindi yenye wabunge 9 huku idadi ya wapiga kura ni ndogo sana. Mkoa wa Tabora ina idadi ndogo ya wapiga kura lakini ina wabunge wa kuchaguliwa 12 huku mkoa wa Tanga wenye idadi ndogo pia ya watu ina wabunge 12. Mikoa hii iliyotajwa kama mfano wa uwiano usiolingana baina ya idadi ya wapiga kura na wingi wa wabunge pia ni maeneo yaliyo ngome ya CCM.

Na kwa hiyo mgawanyo wa majimbo umeiba uchaguzi kwa kutumia mifumo ya kikatiba na kitaasisi kwa maana Tume ya Uchaguzi ni ya rais na mwenye mamlaka ya kutengeneza mikoa ni rais na mteuzi wa viongozi wa Tume ya Uchaguzi ni rais pia. Orodha ya Jumla ya majimbo ya uchaguzi kwa kufuata na tovuti ya bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni majimbo 273 : source : Parliament of Tanzania

Huko nchini Kenya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Majimbo ya Uchaguzi yaani IEBC ndiyo yenye mamlaka ya kutengeneza mipaka ya majimbo ktk Kenya yote inayotumia formula ya idadi ya watu ktk sehemu ndiyo itatoa mwangaza kutakuwepo wabunge wangapi. Sababu ni kuwa nchini Kenya demokrasia inaangazia kuwa wabunge wanawakilisha watu kwa kura na siyo eneo.

Tofauti na Tanzania ambapo ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC haina nguvu kikatiba kutengeneza majimbo kwa kufuatana na idadi ya wapiga kura.

Mfumo huo wa kuangalia eneo hata kama lina wapiga kura wachache na kuwapatia idadi kubwa ya wabunge huku mikoa kama Dar es Salaam, Mwanza yenye idadi kubwa ya wapiga kura inapewa wabunge wachache sana.

Sababu ni kuwa imeonekana maeneo yenye watu wengi ambao ni wapiga kura huwa wana tabia au mazoea ya kuchagua wapinzani hivyo kwa Tanzania wengi hao wanapewa wabunge wachache ili kudhibiti idadi ya wabunge wa upinzani wanaoweza kuchaguliwa . Parliament of Tanzania

Wawakilishi wa waangalizi wa chaguzi toka ndani na nje wameona mapungufu haya ya kuwa kuna maeneo yana wapiga kura wachache sana lakini ina wabunge wengi, huku kuna maeneo yenye wapiga kura wengi inawakilishwa na wabunge wachache sana na hii Indonesia kukosekana uwiano kati ya idadi ya wabunge na wapiga kura wao.

Source : Forbs Media
Tume ya Uhusiano na Uratibu Rasimu ya Warioba ililenga kuhakikisha ... Warioba alisema idadi ya wabunge isizidi 75, Bunge Maalum likasema..... soma zaidi : source : Hotuba ya Jaji Josefu Warioba kuhusu Rasimu ya Katiba ya Tanzania
Gerrymandering is to manipulate district boundaries, for political advantage.
 
Fikiria Zanzibar ina watu milioni 2 na ina wabunge 80 wakati Dar ina watu milioni 6 ina wabunge 13! ni aibu kubwa
Na kati ya hao 2 million kuna wajumbe wa baraza la wawakilishi, mawaziri kwenye baraza la mapinduzi na utitiri wa vyeo vingine vya kizanzibari. Literally huko visiwani kila familia ina kiongozi na analipwa kwa kodi zenu, mleliwa yaani.
 
uchumi wa dar na pwani umeletwa na watu from bara
kidogo kwa mbali mwanza kua na uchumi mkubwa ni juhud zao

dar na pwani maskini wengi ni wazawa
Kwa hiyo nyie matajiri wa Mzee Mbow ndio akili zenu hizi 🙆‍♂️🙆‍♂️
 
Back
Top Bottom