Mikopo umiza, kausha damu ni matunda ya mifumo ya kibenki iliyojaa urasimu

Mikopo umiza, kausha damu ni matunda ya mifumo ya kibenki iliyojaa urasimu

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kwenye vyombo vya habari madhila wayapatayo wakopaji wa taasisi za mikopo midogomidogo hususani akina Mama inaonekana sauti ya vilio ni kama imepanda zaidi.

Kwanza kabisa taasisi hizo pamoja na kupewa jina baya kana kwamba zinakosea sana ni zao la mifumo mibovu iliyojaa urasimu mwingi ya kibenki. Watanzania walifurahia sana kipindi cha uanzishwaji wa benki ya "National Microfinance Bank" iliyobeba jina la makabwela ila kiuhalisia makabwela hawaaminiki hata kidogo.

Maadili mabovu yaliyotukuza yametuaondolea Watanzania wengi uaminifu na kuaminika siyo tu na taasisi za kifedha ila hata vyombo vya Serikali vinapotaka kuisaidia jamii kiuchumi hujikuta katika pata potea.

Elimu ya fedha "financial education" ni janga la Taifa linalosubiri kutangazwa tu. Ni suala la muda tu uhalisia hauvumilii kufichwa. Elimu tunayofundishwa inatuandaa kujiajiri au kuajiriwa na imeacha ombwe kubwa la Usimamizi wa fedha inayotokana na ujira ndiyo maana leo mfanyakazi anapewa elimu ya matumizi ya pesa anapofikia umri wa kustaafu Ili asichanganyikiwe zaidi.
 
Ukiwalaumu bank unakosea, hio imetokana na sisi wenyewe kutokuwa waaminifu kabisa kwenye kulipa marejesho, ingekuwa jamii inayoheshimu kulipa madeni, am sure tungepata unafuu sana bank zetu, ila ndio hivyo, mbongo ukimkopesha bila kuchukua kitu chake ni umeliwa hio.
 
Ukiwalaumu bank unakosea, hio imetokana na sisi wenyewe kutokuwa waaminifu kabisa kwenye kulipa marejesho, ingekuwa jamii inayoheshimu kulipa madeni, am sure tungepata unafuu sana bank zetu, ila ndio hivyo, mbongo ukimkopesha bila kuchukua kitu chake ni umeliwa hio
Mifumo hiyo ni zao letu
 
Vigezo lazma vizingatiwe japo hizi benki zinaweza kuangalia ni aina gani ya mkopo na dhamana wanayoweza kuitumia ili iendane na watu waliopo katika sekta zisizo rasmi.

Ukiondoa vigezo utawapata wadau wa kausha damu maana wengine marejesho yanawashinda kwa sababu mikopo waliitumia kwenye kutunzana kwenye sherehe zao.
 
Vigezo lazma vizingatiwe japo hizi benki zinaweza kuangalia ni aina gani ya mkopo na dhamana wanayoweza kuitumia ili iendane na watu waliopo katika sekta zisizo rasmi..

Ukiondoa vigezo utawapata wadau wa kausha damu maana wengine marejesho yanawashinda kwa sababu mikopo waliitumia kwenye kutunzana kwenye sherehe zao..
Hapa ndipo tunapojipiga
 
Majuzi hapa nilienda bank moja ina tawi mwenge barabara ya kwenda coca, aiseee yule afisa mikopo kwanza anajifanya anamambo mengi kweli kweli mara link ya kikaoo mara chukua namba utanitafuta na brah brah kibaoo
kungekuwa kuna sehem ya kutoa rate kwa mfanya kazi mmoja mmoja huyu jama ningempa negative ya 10/10 ovyoo kabisaa na nilimtafuta zaid ya mara 3 Hakuna respond ya maana.
Nimeamuwa kwenda branch nyingne na ninatarajia kupokea mkopo wangu.
Hivyo basi wakati mwingne siyo kosa la mabenk wao wana taratibu zao za kukopesha ambazo kiuhalisia watu weng tulioko sekta ambazo sio rasimi tunapata shida kwasababu weng wetu vigezo havitoshelezi vya kupewa mkopo.

bank wao wanaangalia uwezekano wa pesa yao kurudi sasa wakiona uwezekano wa kurud pesa ni mdogo una hatari ya kukosa mkopo na ndo unaanguoia kwa kina ASA,BRAC na wengneo
 
Majuzi hapa nilienda bank moja ina tawi mwenge barabara ya kwenda coca, aiseee yule afisa mikopo kwanza anajifanya anamambo mengi kweli kweli mara link ya kikaoo mara chukua namba utanitafuta na brah brah kibaoo
kungekuwa kuna sehem ya kutoa rate kwa mfanya kazi mmoja mmoja huyu jama ningempa negative ya 10/10 ovyoo kabisaa na nilimtafuta zaid ya mara 3 Hakuna respond ya maana.
Nimeamuwa kwenda branch nyingne na ninatarajia kupokea mkopo wangu.
Hivyo basi wakati mwingne siyo kosa la mabenk wao wana taratibu zao za kukopesha ambazo kiuhalisia watu weng tulioko sekta ambazo sio rasimi tunapata shida kwasababu weng wetu vigezo havitoshelezi vya kupewa mkopo.

bank wao wanaangalia uwezekano wa pesa yao kurudi sasa wakiona uwezekano wa kurud pesa ni mdogo una hatari ya kukosa mkopo na ndo unaanguoia kwa kina ASA,BRAC na wengneo
Mkuu hatuaminiki hata kidogo, hatuna elimu ya fedha wengi wetu. Jamii yetu inatakiwa ibadilike kama tunataka kusaidika na uchumi wa kidunia. Kama sisi wenyewe kwa wenyewe tu hatuaminiani kabisa....dah!
 
Mkuu hatuaminiki hata kidogo, hatuna elimu ya fedha wengi wetu. Jamii yetu inatakiwa ibadilike kama tunataka kusaidika na uchumi wa kidunia. Kama sisi wenyewe kwa wenyewe tu hatuaminiani kabisa....dah!
Siyo kuaminika mkuu ni suala la vigezo kama una vigezo ambavyo bank wameweka wanakukopesha
Sasa wengi vigezo hatuna kwasababu biashara zetu haziko kwenye mfumo rasim wa ulipa kodi ndo maana wanataka watu walioko kwenye vikundi ndo wanawakopesha kiasi kwamba siyo rahisi watu 15 wote kukimbia kwa wakati mmoja
 
Asante kwa mada nzuri inayoleta changamoto kwenye mitazamo na machukulia yetu kwenye elimu ya fedha.
Uhalisia tumekuzwa katika utafutaji na utumiaji kwa leo tu, hatuna chochote tunachofanya wala kuwaza kwaajili ya kesho!
Hii ni kwa sababu ya ukubwa wa umaskini uliopo tunachokipata hakitoshi hata leo ndio maana kesho inakuwa inatudai kila kunapopambazuka.
 
Asante kwa mada nzuri inayoleta changamoto kwenye mitazamo na machukulia yetu kwenye elimu ya fedha.
Uhalisia tumekuzwa katika utafutaji na utumiaji kwa leo tu, hatuna chochote tunachofanya wala kuwaza kwaajili ya kesho!
Hii ni kwa sababu ya ukubwa wa umaskini uliopo tunachokipata hakitoshi hata leo ndio maana kesho inakuwa inatudai kila kunapopambazuka.
Mwalimu wangu wa Economics of education Prof. Justinian Galabawa anaita higher propensity to consume
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kwenye vyombo vya habari madhila wayapatayo wakopaji wa taasisi za mikopo midogomidogo hususani akina Mama inaonekana sauti ya vilio ni kama imepanda zaidi.

Kwanza kabisa taasisi hizo pamoja na kupewa jina baya kana kwamba zinakosea sana ni zao la mifumo mibovu iliyojaa urasimu mwingi ya kibenki. Watanzania walifurahia sana kipindi cha uanzishwaji wa benki ya "National Microfinance Bank" iliyobeba jina la makabwela ila kiuhalisia makabwela hawaaminiki hata kidogo.

Maadili mabovu yaliyotukuza yametuaondolea Watanzania wengi uaminifu na kuaminika siyo tu na taasisi za kifedha ila hata vyombo vya Serikali vinapotaka kuisaidia jamii kiuchumi hujikuta katika pata potea.

Elimu ya fedha "financial education" ni janga la Taifa linalosubiri kutangazwa tu. Ni suala la muda tu uhalisia hauvumilii kufichwa. Elimu tunayofundishwa inatuandaa kujiajiri au kuajiriwa na imeacha ombwe kubwa la Usimamizi wa fedha inayotokana na ujira ndiyo maana leo mfanyakazi anapewa elimu ya matumizi ya pesa anapofikia umri wa kustaafu Ili asichanganyikiwe zaidi.
I dont think you are right. Tatizo linaanzia kwenye uongozi wa nchi. Nchi yoyote isipokuwa na uongozi mzuri kila kitu kinakwenda kombo. Nasema hivi kwa sababu benki zipo kufanya biashara na siyo kufanya hisani. Ukiona benki hazitaki kutoa mikopo basi uelewe tatizo ni kukosa wateja wenye sifa za kuweza kukopesheka. Kuhusu hizi taasisi uchwara za kukopesha, nalo ni tatizo la serikali kwenye usimamizi.
 
I dont think you are right. Tatizo linaanzia kwenye uongozi wa nchi. Nchi yoyote isipokuwa na uongozi mzuri kila kitu kinakwenda kombo. Nasema hivi kwa sababu benki zipo kufanya biashara na siyo kufanya hisani. Ukiona benki hazitaki kutoa mikopo basi uelewe tatizo ni kukosa wateja wenye sifa za kuweza kukopesheka. Kuhusu hizi taasisi uchwara za kukopesha, nalo ni tatizo la serikali kwenye usimamizi.
In a free economy government act as a buffet zone to enhance fair play between buyers and consumers....kazi sana
 
Back
Top Bottom