Mikutano ya Vyama vya Siasa imezuiliwa kwa Sheria ipi ya Katiba yetu?

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2021
Posts
3,085
Reaction score
4,890
Wadau nchi yetu inaongozwa kwa Mujibu wa KATIBA iliyopo japo kuna Ukiukwaji Mkubwa wa KATIBA Unafanyika na Wenye KINGA Zao.

VYAMA vya SIASA vipo kwa Mujibu wa KATIBA na Shughuli zao zimeainishwa kwa Mujibu wa KATIBA

Toka AWAMU ya 5 imeingia Madarakani IMEVIZUIA VYAMA vya UPINZANI TU kufanya MIKUTANO ya HADHARA na ya NDANI Zuio ambalo Halikuwepo katika AWAMU zilizopita

Najiuliza ni Kwa Sheria ipi ndani ya KATIBA iliyovizuia VYAMA vya UPINZANI TU Kufanya MIKUTANO lakini IKARUHUSU CCM ifanye MIKUTANO?
 
Vimezuliwa kwa Amri halali ya Raisi wa Jamhuri ya Muungano ambaye pia Mwenyekiti wa Chama Tawala.
 
Magaidi hawatumii sheria. Jiongeze
 
ni uhuni tu wa CCM, hamna sheria yoyote waliyotumia kuzuia shughuli za kisiasa, mikutano ya hadhara na maandamano - wana hofu sababu hawakubaliki tena na wananchi hasa wa hali ya chini, hivyo kuzuia ni moja tu ya mbinu wanayotumia kubakia madarakani... zipo nyingi tu.
 
Nenda kituo chochote cha polisi kilicho karibu yako ukahoji,asante!!
 
Wakati ule pascal alipomuuliza Mwendazake ni sheria ipi anayotumia kuzuia mikutano hiyo alichojibiwa ni kuwa ana njaa
 
Wakati huo huo Pinda na Shaka wanapita kuimarisha chama, wakina Mama wa chadema wakifanya mazoezi ni nongwa.
 
Wakati ule pascal alipomuuliza Mwendazake ni sheria ipi anayotumia kuzuia mikutano hiyo alichojibiwa ni kuwa ana njaa
Hakujibu kabisa hilo swali. Na hakuna mwingine yeyote aliyewahi kumuuliza hilo swali. Pongezi kwake Pascal Mayala.
Mi' nikategemea, wanaonyimwa haki hiyo, wangeenda Mahakamani ili ifafanue uhalali wa amri hiyo iliyotolewa na Rais. Kukaa kimya, na kulalamika tu, ni kama kuikubali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…