Mila na desturi zinachangia katika umri wetu wa kuishi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Umri wa kuishi huchangiwa na maisha yako ya kila siku. Kuanzia vyakula, pombe, mazingira unayoishi kama ni sehemu yenye hewa safi utaepukana na magonjwa yanayoathiri mfumo wa upumuaji.

Kuna muandishi mmoja alisema maisha unayoishi yanatabiri maisha yako miaka kumi mbele. Maana yake kama wewe ni mtu wa kutembea hata masaa mawili kila siku iwe kwa kupenda au kwa kukosa nauli ya basi una uhakika miaka kumi ijayo utaweza kumudu matumizi ya miguu yako vyema tu. Kama ni mnywa konyagi chupa kila siku usishangae kupata matatizo ya ini miaka kumi ijayo.

Wale watu ambao culture zao haziruhusu kunywa pombe mara nyingi huwa wana umri mrefu zaidi ya walevi. Licha ya hayo wataalamu wanasema kunywa kwa moderation yaani glass moja tu ya 125 mils jioni kabla ya kulala inaweza kukusaidia kurefusha maisha.

Kuna wanaoomba kufa mapema kutokana na matatizo yaliyowazunguka na kuna wanaokufa mapema na kuacha ukwasi Iwan mali nyingi wala wasingemaliza kuzitumoa hata wangeishi miaka 200 duniani.
 
Mila na Desturi za Yellow people's zinawafanya waishi Musa mrefu. Kuna Jamii ni matajiri wa mila na desturi. Hadi unaona wivu.

NI kwa Nini sisi hatuna mila na desturi na kama zipo Tunaona hazina maana. Tumeng'ang'ania Mila na Desturi za wazungu.
Kuanzia
Dini
Mavazi
Chakula
N.k
Natamani siku Moja na sisi tujivunie Mila na Desturi zetu, siyo kuziona hazina Maana
 
Sisi tuna vitu vingi vizuri lakini hatujui jinsi ya kuishi vizuri. Labda ni umasikini na kukosa elimu vinatusumbua.

Ukiishi sehemu yenye uoto na mimea ya kijani hiyo ni nafasi yako nzuri ya kuongeza miaka. Nyumba iwe safi na imepangwa vizuri itakuepusha na vumbi pia nyumba iliyopangwa vizuri upa ubongo mapumziko.

Kutengeneza hivi si gharama kubwa. Wazungu wakija Tanzania wanakumbilia Iringa au Lushoto sisi tung’ang’ania kubanana Kwamtogole.
 
Wewe lengo lako ni kutaka tuache POMBE tu hayo mengine ni mbwembwe tu hahahahhaha mjanja sana wewe dada ila nimekuelewa kwenye kunywa moderately.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…