thanx LAT ngoja nku pm unipe detailz.thanx alot
Mheshimiwa LAT na mimi pia nahitaji sana hizo details nipe e-mail yako au number yako ya simu tuwasiliane
wawe wanaweka bnki kila J 3...yeah uku mbuzi katoliki ni wengi kilo ni 3500 tu.i think ata hii ni biashara nzur ila inahitaji space ya kutosha.
Kwa bodaboda hesabu yao ni 7000 kwa cku ila inabd kupata mtu mwaminifu sn,weng wao huwa hawalet hela cku zote,sbb kibao kila cku
mama derick... je songea juices za concentrates kama zinazokua packed kwenye cups kama za METL zinapatikana.... kuna machine ndogo (semi automatic sealing machine) yaku seal juice kwenye cups kama hizo za METL ....zinapatikana china kwa bei ndogo sana...halafu utanunua juice concentrates with different flavour from anywhere pamoja na cups and seal film zitatoka china... ukapack na ku seal na kuuza katika mji mzima wa songea... ukaipa brand name ya derick juices.... budget yako ni nzuri kwa mradi huu... ni PM nikutumie more details pamoja na photos na machine particulars uamue kusuka au kunyoa bure kabisa
View attachment 21901
something like this
Mkuu LAT; mimi natafuta machine ya kupack maziwa ya ng'ombe, je naweza kupata container za 1 litre or 1.5 litre kwa mashine hizi. Naomba mawazo yako kama unafahamu aina nyingine ya mashine ambayo inaweza kunifaa. Hata hivyo naomba nami unitumie details za hii mashine
mkuu mgombezi.... nafurahia juhudi zako nyngi katika kufanikisha ujasiriamali..... ngoja niangalie kwenye database yangu ya sourcing nitakujibu nadhani ipo ambayo it will best fit for you..... pia nitamuuliza huyu supplier wa hizi PEP cups kama wana bottles..au atupe supplier wa hizi bottles nitaku pm
KAMA SI CCM BASI WE CUF au PONA!We zinywe pombe tu, make hizo huwezi kufanya chochote. ukilazimisha kufanya biashara yoyote haziwezi kutoka make ni kidogo sana
We zinywe pombe tu, make hizo huwezi kufanya chochote. ukilazimisha kufanya biashara yoyote haziwezi kutoka make ni kidogo sana
Teh teh teh! drphone umefikiria mbali sana, kinda funny lakini kuna point....maesabu mazuri sana tena sana kasoro ujaweka hesabu ya miguu na mikono ya bandia kwa madereva watakao tumia mwaka mmoja na nusu bado mda atakao kaa muhimbili na siku hizi hawakai sana mana wanakata miguu na mikono kupunguza garama za kuuguza
Nyange we vipi? Mama Derick baadhi ya watu watakukatisha tamaa lakini usitishike kwani inawezekana, muhimu ni kuweka nia , kisha ni kuangalia kuna opportunity gani kama alivyokushauri Prime Dynamics, msingi wako kweli ni mdogo kwa hivo ni muhimu katika chochote kile utakachofanya inabidi uwajibike wewe mwenyewe (Front line)
Kama walivokueleza waliotangulia kuna watu walianzia biashara na hela ndogo zaidi ya hapo, mfano biashara ya mama ntilie haihitaji msingi mkubwa, kwa uzoefu wangu kwa kiasi kama cha kwako ni bora ujishughulishe na biashara inayohusiana na chakula, (ufugaji kuku, ngombe wa maziwa, bekari, mama ntilie, mazao etc.) biashara ya chakula always ina high demands, muhimu ni kuangalia competition na uboreshe huduma iwe juu zaidi ya wengine.
Nikupe mifano miwili.
1. Nimeona mara nyingi naenda bar mida ya usiku unaagiza mbuzi unaambiwa imekwisha, kuku imekwisha muhudumu anakwambia labda tumebaki na ndizi tu! Kwa hio hapo kuna marketing opportunity, kama utanunua deep freezer unaenda kwa wafugaji vijiji vya karibu ( kufuata unafuu) unanunua kuku, kitimoto ama mbuzi mfano kwa kuanzia kuku 100 kilo 50 mbuzi na 50 kitimoto kwa wiki, unachinja unawahifadhi kwenye Freezer yako, weka contact zako kwenye mabaa wakihitaji emergency unawaletea fasta fasta nadhani kwa siku unaweza kuuza kuku kama 10 kirahisi kabisa, hapo vifaa vinavohitajika ni Freezer, bodaboda 1 na kama hela inaruhusu jenereta yenye nguvu ya kuendesha hio freezer, kwa vile umeme wetu wa mgao ili biashara yako isioze kwa kukikosekana umeme, na hapa kwa hii jenereta ndio utapiga bao sana, na hii bodaboda nyakati za mchana unaweza kuipigia kazi ya abiria vilevile.
Nafasi na biashara za kufanya hata kwa kima ulichonacho ni nyingi, wewe kwa kuanza angalia mazingira yaliyokuzunguka, jee kuna usumbufu gani unaweza kuupatia suluhisho kwa kiwango cha fedha uliyonayo? Ama huduma gani ya kijamii ambayo unaona imezorota na unaweza kuiboresha?
2. Nimeona wafanyakazi wakisumbuka kufuata lunch umbali wa maili nzima na wakifika mkahawani waanze kupanga ques by the time wamepata oda yao na lunch break imeisha! ( jee wazo la kuchukua tenda ya kuhudumia lunch boxes maofisini?) kama utaweza kuanza kuwa-convince hata wafanyakazi 10 na kuingia dili na mwenye mkahawa unaleta lunch boxes on time ofisini na kutoza hela ndogo si ajabu baada ya mwezi unaweza kujikuta una wateja kama 100.
The opportunities is endless, just kaa kitako, fikiria kero, angalia uwezo wako, unaweza kuboresha ama kuondoa hio kero? unaweza fanyia kazi hio issue na kama huwezi fikiria tena kitu kingine mpaka utakapopata kile kilicho kwenye uwezo wako.
Mfano:Mimi binafsi sipendi kunununua bidhaa nikafungiwa na gazeti, kama ningalikuwa naishi hapa ningeanza na kuangalia uwezekano kwa kutengeneza cheap environmental friendly paper caring bags.
Theorists of success in business and life wana discourage dabbling...u shud mean biznezz..and not kujaribu jaribu.
Usahuri wangu:
>>Find out your brilliance zone.....u can't be good at everything but u can be very good at one thing..most people enjoy something they are very good at..in this sense utafanya wholeheartedly...and u will stand firm for it constantly and persistently no matter what problems u may face.It will help you to deliver unique and good service/customer care.
>>Ukishagundua your brilliance zone,start learning how to make a good approach/start from various sources available.Learn from anyone u think can get something from....remember the more u think u know the more dumber you are
>>Set up your goals,,dream big
>>jot down your plan in priorities
>>Make sure everyday u do for something written in your plan and towards your goals.....no matter what,,,get up,dress up and show up according to your plan.
>>80% of your world(outer world) comes from your thoughts(inner world)....so enrich and purify your thoughts.
>>Commitment ....get committed..spend more time and energy towards your goals..the reason why successful people make only 10% of the population is that they do things which the rest cant do.
As for what to do...inategemea your brilliance zone and opportunities.....but all in all napendekeza zaidi investment by low scale production and/or processing....kutokana na kwamba bado mfanyakazi na mtaji mdogo.
Kwa hiyo figure out..it can be seasonal food production kama vile nyanya ..hapa utatumia water pump machines na water tanks to facilitate irrigation,...au..bakery..kuna low scale machines for baking...maana huko sidhani kama Azam mkate wafika...au hiyo juice processing etc.
Unaweza pia kununua clinical diagnostic machine kama ultrasound,ya kupimia mkojo,kupimia damu etc ukaingia ubia na zahanati ukawa unakula bingo taratiiiiiiibu.
Kama ni kufuga kuku...nakushauri ununue incubator yako pamoja na machine ya kuangalizia mayai viza au mazima....they are cheap out there....kusanya mayai ya kienyeji...weka kwenye incubator..aisee utakuwa unafyatua kuku kama matofali...na soko la kuku siku hizi ni kubwa.
Machine ya kuranda na kutengeneza mbao pia nayo si mbaya au hata machine ya kusaga na kukoboa....check opportunities na vigezo hapo juu.
Kumbuka all of the things we have and do are once were formless thoughts from just a single person like me and you my dear Mama Derek
nashkuru sana voice of reason.ata cjui niwashukuru vp jmn kwa ushirikiano mlionao,ila thanx 4 everything,may GOD bless u more.ntayafanyia kazi mawazo yakoWakuu Salaam; Pamoja na Mawazo yote mazuri naomba mama Derick asisahau yafuatayo katika biashara atakayofanya:-
Mtaji (Capital)
Amesema anazo Milioni 3; Je hizo Boda Boda mtaji utafaa, pili kabla ya kununua mashine ya packing awe very careful mtaji wake usiishe kwenye packing machine inabidi aconcentrate kwanza kwenye product yenyewe kabla ya kuingia kwenye extras, Is the product good enough sababu ukipaki mchanga kwenye chupa nzuri sio kwamba watu watanunua
Product
Kabla haujaanza kupack hiyo product yenyewe kwanza angalia kama ni nzuri na inapendwa, (sababu I as know hizo concentrates mimi nilikuwa kuna kipindi nanunua nilivyokuwa shule because of price, zilikuwa cheap na sio kwamba ni nzuri zilikuwa zinaacha uchungu fulani kwenye koo) Kwahiyo kabla haujainvest kwenye packing labda anza kuuza hiyo juice kwenye powder form ili watu wenyewe watest uone kama kweli inapedwa au wewe unaipenda, Pili hata ukipata mashine kutoka China angalia kama kuna uwezekano wa kupata chupa kutoka Tanzania hii itapunguza shipping cost na ushuru.
Competition
Je Juice yako itakuwa nzuri kama au zaidi ya Azam, Je itakuwa cheaper, kwanini watu wanunue yako na sio ya Azam?
Branding
Sometimes Brand inaweza ikawa negative au positive, mfano mtu anaponunua Azam au Del Monte kichwani anapata wazo la Juice safi inayotengenezwa kwa vizuri bila madhara, Je atakapoona Mama Derick atawaza nini?, kwahiyo ni bora kwanza tengeneza Juice nzuri kwanza ipate soko na watu waijue na waipende Then hapo ndio unaweza ukacapitalize kwenye Branding lakini It does not mean usiweke contact zako kwenye hizo Chupa what I mean start slow na dont spend unnecessarily.
Who are Your Customers?
Je utamuuzia nani, machinga mitaani au wholesale kwenye supermarket na kwenye maduka ?, Machinga they dont really care about packaging ila bei iwe ni ndogo , lakini kama ni supermarket na maduka package na appearance ni muhimu.
Je Juice kama Azam n.k. zina wateja kiasi gani, watu wanapenda natural drinks au artificial ?
Legal Issues ?
Ukienda all guns blazing sababu hiki ni kinywaji na watu wanakunywa itabidi kichekiwe ubora wake, na upewe vibali n.k. which might take time and money
JE MTAJI WAKO WA 3 Million Bado unatosha
USHAURI WANGU
Anza polepole usisubiri mpaka upate pesa nyingi, hata kama hauna pesa ya mashine unaweza bado ukatengeneza Juice ukaweka hata kwenye mifuko ya plastic (decrease cost) hii itakusaidia hata wewe kuweza kuuza vitu kwa bei rahisi
Ni vizuri kuanza polepole sababu kuna learning curve ?, na watu wakuzoee Concentrate first on the product before packaging. Ukishapata soko na product yako ni nzuri then move kwenye extras.., pili am sure hata dar kuna viwanda vya chupa tupu kama ukinunua nyingi sana unit price huenda ikawa chini ya 50 tshs.
nashkuru sana voice of reason.ata cjui niwashukuru vp jmn kwa ushirikiano mlionao,ila thanx 4 everything,may GOD bless u more.ntayafanyia kazi mawazo yako
nashkuru sana Qadhi kwa mawazo yako mazuri kbs.am hap kuingia ktk jf mana wana jf are so cooperative.thanx 4 everything.
Sasa Qadhi unaweza ukawa na idea wapi zinauzwa izo incubator ndogo pamoja na kifaa cha kuangalia mayai na pia zinauzwa kwa bei gani?
Karibu Mama Derick,
Niliziona pale Guangzhou(China) last year,incubator zenye capacity ya mayai 500 ilikuwa ni us$ 200~us$ 300.Ukiagiza kutoka China unatakiwa uongeze umakini,utafute suppliers wa uhakika,ukinunua vibandani tu utalamba feki.
Mashine ya kuchekia mayai sikuwahi kuulizia bei.
Kila la kheir Mama Derick
Kama haupendi biashara ya mboga mboga na boda boda, basi nunua mshine ya juice pale university of Dar es salaam, inauzwa milioni moja na nusu. Nenda sido lipa laki mbili na nusu soma wiki 2 jinsi ya kutengeneza juice. Mashine inatengeneza lita mia moja kwa saa. Uwiano kama ukitengeneza maembe ya shilingi elfu mbili na mia tano, utauza na utapata shilingi elfu kumi na tano kwa kuuza kila glass au robo lita shs mia tano. Kama una mtoto wa kiume au wa kike ambaye si mlevi, mtume akanunue alizeti magunia mia moja. Kila gunia moja litakupatia faida ya shilingi elfu ishirini. 20,000 x 100 = 2,000,000/= Magunia mia utayapata kwa shilingi milioni mbili. Nimekwisha kufanyia hesabu nyingine kama vile usafiri, kukamua mafuta kwa mashine ya mtu. Kusafirisha mafuta sokoni na mwisho wa siku kwa siku 60 utakuwa na faida shilingi milioni 2, akiba yako ingelikuwa laki 4 na mtaji wako utakuwa umebaki pale pale milioni 3. Utakuwa umekwishajilipa mshahara pia hata kama umeajiriwa. Kwa mawazo zaidi, 0718 19 4606. Mwalimu wa ujasiriamali. Nitakuchaji shilingi elfu kumi ushauri kwani wewe ni mwana JF. Usisahau kukata bima kama utaamua kufanya biashara ya boda boda. Ukinitumia mimi nitakuuzia pikipiki na utakata bima shs 72,000 majambazi wakikunyanganya au ikipata ajali tunakupa pikipiki nyingine. Jamaa alioandika biashara ya mboga mboga na pikipiki nao pia ushauri ni mzuri sana. Uchukue wowote