Mimba changa

mrsfulani

Senior Member
Joined
Oct 19, 2015
Posts
113
Reaction score
69
Habari zenu jaman nahitaji msaada jinsi ya kulea au kutunza mimba ikiwa changa ndo mimba ya kwanza sijui chochote naomba mnasidie vitu gani vya kuwa navyo makin au kuacha kbs ktk kipindi iki
 
Habari zenu jaman nahitaji msaada jinsi ya kulea au kutunza mimba ikiwa changa ndo mimba ya kwanza sijui chochote naomba mnasidie vitu gani vya kuwa navyo makin au kuacha kbs ktk kipindi iki
Tafuta mama mwenye hekima na busara na umuulize utapata msaada zaidi kama litashindikana nenda kliniki ya mama na mtoto huko kuna wataalam wa mambo hayo... Siyo kila jambo linapaswa kuwekwa barazana mengine jisetirie faragha.
 
Naomba usichukue ushauri online hasa JamiiForums maana huyo ni kiumbe any mistake might lead to damage. JF kuna tabia ya watu ambao kichwani hawako vizuri, kitu hata kama hawakijui watakupa story wanazosikia mtaani ili mradi tu kuendesha discussion au kujaribu kuonekana kua ni smart kumbe ni very stupid. Mwisho wa siku utafata ushauri wao utaumia.
 
kidogo ninavyojua ukiumwa usinunue dawa phamacy ukajinywea bila ushauri dktar asa dawa za kienyeji pia kingne usipende kunywa vinywaji vya kikemikari asa vile wanaita energy drink
mf redbul azamenergdrink nk
mke wa rafiki angu mimba ilitoka baada kunywa peps mbiri kwa mkupuo ilikuwa ya wiki 3
na ikiwezekana pia usinywe chai ya majani ya chai
enzi hzo wkt sec kimimba cha wiki 1 au 2 dawa yake ilikuwa chai kikombe kimoja pakt 10 za sh 20/=(bei ya miaka ya 2002 hiyo sasa )
 

Kuna Dada alishawahi kuaribu mimba kwa kufuata Ushauri wa JF,tena huo Ushauri umetoka kwa jamaa maarufu sana humu lakini alivyoleta feedback kwamba kichanga kimearibiki mtaalamu wa JF akaruka futi 100,ni kweli JF Kuna vilaza wengi wanaojifanya smart.
 

Nakuunga mkono kwa 100%
 
Cha kwanza nenda kajiandikishe clinic,kuna vitu muhimu unatakiwa kupewa kwa mfano,unatakiwa kupewa madini ya folic acid mimba ikiwa changa kuzuia kuzaa mtoto mwenye kichwa kikubwa, hii ni sabb kazi ya kwanza ya uumbaji wa mtoto ni ubongo...
 
Cha kwanza kaanze clinic wakupe prenatals na folic.....

Jitahidi kula balanced diet..... na kunywa maji ya kutosha hata kama ua kichefuchefu

Epuka kutumia madawa au yoyote bila ushauri wa daktari(hata herbals usitumie)

Epuka kunyanyua vitu viziiiito kwa sasa

Relax na muombe mwanao mara kwa mara

Ukiona hali yoyote ya ajabu wahi hospitali
 

Hiyo prenantal ni nini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…