Mimba iliyotungwa kwenye ovary

Mimba iliyotungwa kwenye ovary

Poluyakhtov

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2017
Posts
358
Reaction score
300
Habarini za usiku ndugu zangu,

Mimi ni kijana wa miaka 27, nimeoa miezi mitatu iliyopita. Sasa, juzi ghalfa mke wangu akaanza kujisikia maumivu upande wa chini wa kulia. Baada ya kumpeleka hospitali nikaambiwa ana UTI na Fangasi,alipewa dawa za kutibu hayo maradhi lakini hakupata nafuu.

Ikabidi nimpeleke tena Clinic moja akapate kipimo cha Ultra Sound.

Matokeo yameonesha kuwa ana Ectopic Pregnancy kwenye Ovary ya kulia.Sasa nimeshauriwa kumpeleka hospitali ya rufaa kwa msaada zaidi. Changamoto iliyopo ni kwamba kwa sasa kipato hakija kaa sawa(mimi ni mtu wa mshahara)na sijalipwa pato langu la disemba.

Ninahitaji kukopa fedha ili niweze kumsaidia mke wangu,lakini sijajua ni kiasi gani inagharimu kufanya hiyo operation kwa hospitali za serikali.Naomba kwa anayejua gharama zake anijulishe ili nijue nakopa kiasi gani na niweze kumsaidia.Asanteni.
 
Ushauri wangu ungeenda hospital kwanza watakupa majibu nini cha kufanya. Ila ukisubiri unaendelea kumuweka katika hali hatarishi mke wako. .
 
Habarini za usiku ndugu zangu,

Mimi ni kijana wa miaka 27, nimeoa miezi mitatu iliyopita. Sasa, juzi ghalfa mke wangu akaanza kujisikia maumivu upande wa chini wa kulia. Baada ya kumpeleka hospitali nikaambiwa ana UTI na Fangasi,alipewa dawa za kutibu hayo maradhi lakini hakupata nafuu.

Ikabidi nimpeleke tena Clinic moja akapate kipimo cha Ultra Sound.

Matokeo yameonesha kuwa ana Ectopic Pregnancy kwenye Ovary ya kulia.Sasa nimeshauriwa kumpeleka hospitali ya rufaa kwa msaada zaidi. Changamoto iliyopo ni kwamba kwa sasa kipato hakija kaa sawa(mimi ni mtu wa mshahara)na sijalipwa pato langu la disemba.

Ninahitaji kukopa fedha ili niweze kumsaidia mke wangu,lakini sijajua ni kiasi gani inagharimu kufanya hiyo operation kwa hospitali za serikali.Naomba kwa anayejua gharama zake anijulishe ili nijue nakopa kiasi gani na niweze kumsaidia.Asanteni.
Mkuu,

Ectopic pregnancy ni suala la dharura, tafadhari mpeleke hospitalini pasipo kusubiri hadi upate pesa.

Utaratibu wa hospitali za Serikali unaruhusu watu wenye changamoto kama yako watibiwe kwanza kupitia ustawi wa jamii ikiwa tu utatoa hakikisho kuwa kabla mgonjwa hajaondolewa utalipia gharama husika.

Kuhusu gharama, kwa sasa sina uhakika zinafikia kiasi gani kwa kuwa zinabadilika mara kwa mara, pia kutakuwa na vipimo vingine (pengine hapo atapimwa tena), pia gharama za dawa.

Generally, gharama siyo kubwa sana kwa kuwa huu ni upasuaji mdogo.
 
Wahi hospitali mkuu,hiyo ni dharura atatibiwa tu,hayo mambo ya malipo na vitu vingine itajulikana huko huko...
 
Asee Muwahishe shem haraka sana hosi, hiyoni dharura na ni hatari kwake, angalia asije pata madhara zaidi kwani lazima afanyiwe upasuaji na kufunga mrija uliodhurika.
 
Back
Top Bottom