Mimi Masudi Kipanya na safari yetu ya miaka 100

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KUTOKA DHUHR HADI ALASIRI NA MASUDI ''MTU SPECIAL'' KIPANYA

Leo ilikuwa siku makhsusi yaani special sana kwangu kwa kuwa katika chumba kimoja na Masudi Kipanya na vijana wake ''sharp'' wa Clouds Plus.

Hiki kwa hakika si chumba kwa maana ya chumba kama tulivyozoea bali ni Maktaba ya Elite Bookstore Mbezi Samaki.

Masudi Kipanya alinikaribisha ndani ya Maktaba hii nadhifu sana si kwa kuangalia na kusoma vitabu bali kwa ajili ya kufanya kipindi cha televisheni.

Mvua kubwa iliyonyesha kipindi cha adhuhuri kwa kiasi cha saa moja hivi ilitosha kunionya kuwa ile ilikuwa tahadhari kwangu kwa mfano wa ''thunder and lightning,'' (radi na kimulimuli) katika mchezo wa Mcbeth kuwa mchana wangu hautakuwa wa kawaida.

Kwa muda wa saa mbili Masudi Kipanya akitembea katika mengi niliyopata kuandika katika historia ya Tanganyika alinirudisha nyuma miaka 100 hapa hapa Dar es Salaam ya 1920s akitaka kujua maisha ya wazee wangu waliosukuma gurudumu la historia ambayo si wengi wanaifahamu.

Masudi Kipanya kama ni mchezo wa masumbwi nitamwita, ''South Paw,'' kwa jinsi alivyonitaabisha na maswali ya kushtukiza na wakati mwingine kunibana nisema nisiyopenda kusema na wakati mwingine kunitoa kwa haraka katika niliyodhani yangefaa kusemwa.

Muda ulikwenda kwa haraka sana jua likazama nikiwa sina habari na hatujamaliza safari yetu ya miaka 100.

 
Masudi akili nyingi sana huyo jamaa, namkumbuka vizuri mwaka 2010 nilionana nae pale Makumbusho ilipokuwa Steers ,Kuna jambo nilihitaji muongozo kwake, Duuuu badala yake alikuwa akinipa maswali magumu sana mpaka nikajuta
 
Kwahiyo hii ni taarifa kabla ya habari au taarifa baada ya habari?

U met Masudi Kipanya in the library, so what? What have u two talked?

Isije kuwa ni ule uzushi wako na uongo uliozoea kuumwaga redio Nur, Iman na zingine za dini yako.

Kwa hapa hutaweza kutusokota nakuambia babu,

Sawa sawa???
 
Kwikwikwi
 
Kwikwikwi
Oto...
Sina kawaida ya kumkejeli mtu wala kujaribu kumfanya ajihisi si lolote si chochote.
Hapakuwa na haja ya hiyo ''kwikwikwi.''

Hakuna radio mashuhuri duniani ambayo haijanitafuta kufanya mahojiano na mimi.


Hapa niko BBC Glasgow, Scotland 1991



Hii ni V o A Washington 2011


Radio Iran, Tehran 2007


Hawa ni TBC 7 April 2021


AZAM TV 2015
 
Baaria kitambo
 
Hiyo hapo chini Library of Congress Washington 2011.

 
Masudi Kipanya mbona kwenye picha hapo amefanana sana na Marehemu Rais Magufuli? isije kua tumeachiwa urithi wa tabia mbaya hapa kwa vijana wetu na mwendazake.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 

Mkuu nini lengo hasa la huu uzi wako? Sijaona hata highlights za hiyo safari ya miaka 100.
 
Hiyo hapo chini Library of Congress Washington 2011.

View attachment 1755368
Nakukubali sana mzee wangu vijana tuwahitaji sana watu wa Kariba yako ili kuijenga vema nchi yetu.
Karibu na kwetu kaskazini maana huku wazee wetu wamejitahidi sana kuihifadhi historia yetu na kutupa mwongozo wa kuitengeneza kesho iliyonjema
 
Mzee shikamoo!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…