Mimi ni mtazania mweye wasiwasi na Samwel Sitta!

Mimi ni mtazania mweye wasiwasi na Samwel Sitta!

Kaguta

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2013
Posts
414
Reaction score
504
pongezi.jpg


Sitta amekuwa mtu wa kutilia shaka kwa mtu yoyote. Katika picha hiyo anaonekana akimkumbatia mtu anayeweza kutafisiriwa kama adui yake namba moja hasa kama ulifuatilia suala ugonjwa wa Mwakyembe. Yeye mwenyewe aliutangazia umma wa watanzania kwamba Mwakyembe alipewa sumu na kundi la mafisadi, leo hii anawakumbatia tena hadharani. Kwenye sakata hilo Sitta aliongea kuliko Mwakyembe mwenyewe.

Mwaka jana aliumbuliwa na Dr Slaa kwamba mwaka 2010 alikuwa mgombea wa Chadema kabla ya kula kona na kukubali kupewa uwaziri wa A. Mashariki. Kabla ya hapo alikuwa amejaribu kuanzisha chama chake huku akiwa bado mwanachama wa Ccm, lakini itakumbukwa jinsi alivyozima suala la Richmond lililoasisiwa na kundi lake. Hii ilikuwa baada ya kutishiwa kunyang'anywa kadi ya Ccm.

Binafsi simuelewi, labda katika uzi huu kuna watu wanamjua zaidi wanaweza kutuletea ushuhuda. Unajua jinsi ambavyo amekuwa akiikosoa serikali ambayo yeye ni sehemu yake? Je anafaa kupewa nafasi kubwa zaidi ya hizi alizonazo wakati haeleweki kama ni moto au baridi? Kuna wanaotafisiri kauli zake kama msimamo wake, je tuchukue msimamo gani?
 
Mwl. Nyerere mwaka 1995 aliwahi kutamka kwamba anatamani CCM igawanyike, kwa kuwa aliamini wapo watu ndani ya ccm wasio ipenda ila wako tu kule kwa sababu ya mkate wa kila siku
 
Mimi namfahamu kama mtu ambaye yuko kimaslahi zaidi..na ana kaubinafsi zaidi kuliko uzalendo..angebadilika hiki tu angekuwa kiongozi mzuri kuliko wote katika CCM ya sasa
 
mimi mwenyewe si muamini mheshiwa Sita ni kinyonga si dhani kama atamkuta Kificho
 
Namuomba afanye kweli safari hii, ajuwe katiba ni kitu kingine kabisa asikifananishe na Richmond
 
Hata mie namwona ni anayependa kuzarau watu, kulewa madaraka na kikubwa ni mnafiki na asiyekuwa na maamuzi sahihi kwa wakati unaofaa.
 
Sitta ninaweza kumueleza kwa kifupi tu: mnafiki na msaka vyeo tu
 
Huyo ni mnafiki na wala haeleweki.

Sitta kwa kweli nimuonavyo mimi ni mtu mpenda madaraka sana. Kama alivyowahi kusema Dr. Silaa, ni mtu ambaye yupo tayari kufanya lolote hata kama lina athari kubwa kwa mwenzake au jamii ili mradi atimize malengo yake ya kisiasa. Pia namuona kuwa ni mtu mwenye kupenda sifa asizostahili na mwenye kupenda kujigamba. Si mdemokrasia hata kidogo. Huko bungeni atakandamiza wapinzani wake vibaya sana. Ana lengo la kugobea Uraisi 2015, atatumia fursa hi kujinadi ili kuridhisha CCM kwa kukandamiza wabaya wake na wapinzani wa chama chake. Mungu Ibaki TZ na Mungu ibariki Afrika. Hapo alipopata nadhani pamemtosha lakini Urais NO.
 
Ukitaka kumjua vizuri kaangalie nyumba anayoishi mama yake na ulinganishe na ofisi yake Urambo na nyumba yake binafsi ,maisha yake na uwezo wake linganisha na maisha ya mama yake,wema anaounyesha kwa watu vs wema kwa nduguze wa damu,ukiisha angalia yote na kuyatafakari utakuwa umemjua vizuri mzee wa CCJ/
 
Kwa ile hotuba yake ya shukrani jana bungeni niliona ya kitoto sana iliyojaa majivuno na sifa, ana sifa kuu zote tatu za unafiki.
 
Wasiwasi wako na njaa zako zinatuhusu nini watanzania? Jitilia wasiwasi mwenyewe kwanza.
 
Wote mkafie mbali pamoja na mleta maada wenu. Sitta ni jembe.
 
inabidi tusubirie kwanza tusianze kuhukumu mapema.
 
mimi mwenyewe si muamini mheshiwa Sita ni kinyonga si dhani kama atamkuta Kificho

Ni kweli mkuu...amewekwa na chama kwa maslahi ya chama ambacho anategemea kitampitisha kuwa mgombea urais miezi kadhaa ijayo.
Nikiwaza rumors kuwa alihusika na kuanzishwa CCJ mwisho wakamhadaa Mpendazoe kisha wakam-ditch...sina hamu na huyu mzee.
 
Back
Top Bottom