Mimi ni mwanafunzi niliemalza kidato cha sita na kufanikiwa kuingia chuo kikuu ila nsina uwezo

Kiswahili hakina silabi x na Q sasa hizo x umezitoa wapi?
 
sawa kaka zangu nimwewaelewa wakubwa kwa wadogo siku zote tunajifunza kutokana na yale tulioenda vibaya sawa nimesikia ni makosa tu kidogo ambayo yanaweza kurekebishwa nimewaelewa
 
edit hiyo thread yako hapo juu kwanza ..sio unaomba msamaha huku ndani hakuna atakaye toa pesa yake. Hakuna mtu anayependa kusaidia kilaza. Onyesha hekima zako
 

mtu kama wewe ukikosa mkopo ni sawa tu maana taifa lingeingia hasara..
 
Fanya hivi nenda kwenye media yeyote,
Blogs, Tv, Radio elezea tatizo lako vile vile unaweza waona baadhi ya watu ambao wanaweza kukusaidia katika hilo muone Irene kiwia ana group lake wanachangiza pesa kwa ajili ya kujenga hostel I think kwa wasichana wanaotaka kujiendeleza kielimu kama sijakosea inshu yako itakuwa inashabihiana na project yao wasipokusaidia moja kwamoja naamini watakuonesha A hivyo utajua wapi kwa kupata B pili tafuta mtu akuandikie maombi since umeonesha kushindwa kuandika tafuta mtu akuandikie u submit kwa media mbali mbali kama blogs. U-turn ni blog ya kipumbavu ila mange na mashankupe wake wanaweza kukusaidia
Omba ufanye vipindi kwa Radio, Tv halafu onyesha sympath sio unaomba msaada kama unachat na viji boyfriend vyenu kumbuka unaongea na watu wazima huku..
 
edit hiyo thread yako hapo juu kwanza ..sio unaomba msamaha huku ndani hakuna atakaye toa pesa yake. Hakuna mtu anayependa kusaidia kilaza. Onyesha hekima zako

mkuu umeanza vizuri ila mwishoni umetumia lugha ya kuudhi(hakuna mtu anaependa kusaidia kilaza),sio lugha nzuri kabisa hasa kwa mtu aliye na shida anayehitaji moral and material support,humu jamvini tupo tofauti sana hivyo ata they way tunavyopresent topic zetu lazima tutatofautia,tujifunze kuheshimu mawazo ya wengine,otherwise mkuu naheshimu sana mawazo yako.
 

Asante mkuu kwa kuliona hili. Mimi pia naona kama hayuko serious!
 
vijana hawasomi vitabu , vinasaidia kukupa ujuzi wa ziada katika maswala mbalimbali hasa jinsi ya kukabiliana na matatizo mbali mbali..
DADA kwa sasa ahirisha mwaka kaa na mama chini sababu nae kwa sasa bado ana msongo wa mawazo..Anza tafuta shughuli ktk makampuni ya simu huduma kwa wateja unapata kazi ya kujiwekea akiba au kwengine.Mama najua ni mtu mzima hatakosa chakufanya kujipatia kipato. mpaka mwakani mwezi wa tatu akili itakua imejipanga na matatizo umesahau utasoma vema,kwa sasa utakumbana mengi
 
Mimi mwenyewe kuna maneno sijayaelewa anamaanisha nini kwakweli, 10x ni nini maana yake? Hata hivyo nakutakia kila la heri naamini utafanikiwa

Ila kweli dada umewekaweka maneno ya ajabu ajabu kama upo facebook ila ujumbe umefika
 
Hakuna mahali napaheshimu kama Jamii Forum, ndio social network ya heshima kuliko yoyote hapa Tanzania, na niionavyo Jf hawapendi kusikia au kuona watoto wa facebook wanakuja huku sababu ule utamaduni asilia wa kufikiri kwa makini,undani bila hisia utapotea..dada ungeshapata msaada muda mrefu sana hata wa kulipiwa ada ila lugha za Sintah na Mange Kimambi wanazidharau na kuzichukia sana, ahsante
 
nakushauri ukate rufaa bodi ya mikopo ila lazma uwe na viambatanishi vyote vinavohucka kukutetea Kwa mfano cheti cha kifo cha baba yako,nina uhakika utapata mkopo trust me
karata unaijua bodi vizuri....mwaka huu madogo kibao wenye vigezo vyote wamekosa....hizo rufaa zao ni geresha tu..mara chache sana hubadilisha labda uzunguke mbuyu..
 
nakushauri uende WAMA...Taasisi ya Mama Salma Kikwete huwa inapeleka wasichana wengi tu vyuo kila mwaka...fuatilia ofisi zao zilipo wanaweza kukusaidia
 
edit hiyo thread yako hapo juu kwanza ..sio unaomba msamaha huku ndani hakuna atakaye toa esa yake. Hakuna mtu anayependa kusaidia kilaza. Onyesha hekima zako

nimeipenda hiyo
yani nilivyoona heading roho iliniuma na nikajua sababu anaa tatizo heading hajaandika vizuri kuja kuisoma akanikera na kiswahili hakieleweki hata sielewi inakuwaje hajui matumizi ya ' l' na 'r' hilo nikamsamehe nikajua ni mura yeye
nyingine tena xo aaaa hapo ndo kabisa
sasa dada neema sisi ofisi yetu wanasaidiana watu wenye matatizo kama yako na ninazifahamu sehemu kama tatu
utakazosaidiwa ila unahitaji uandike barua ujielezee(tatizo naogopa kubeba lawama maana sijui kama utaandika barua vizuri)
sawa mdogo wangu basi onyesha umakini hayo ni maisha yako unatakiwa uyasimamie mwenyewe
naomba rekebisha thread andika kiusomi,onyesha unauhitaji si kihunihuni
pia nataka kujua hiko chuo umesharipoti au?maana wanafunzi wamesharipoti? Na kama umesharipoti itakuwa vizuri utafute barua ya head of your department akuidhinishe au barua ya dean of students
sawa utafanikiwa tu usijali
nakuombea sana ufanikishe hilo
 
Asante sana mkuu kwa muitikio chanya juu ya kumsaidia mdogo wetu. Mungu akuzidishie baraka tele.

 

Sawa sawa nadhani ujumbe umefika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…