Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar. Comrade Hashil Seif Hashil anazungumza

Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar. Comrade Hashil Seif Hashil anazungumza

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1550546614002.png


Hiki kitabu ninakisoma hivi sasa.

Bado sijakimaliza lakini nimejifunza mengi katika historia ya Makomredi wa Zanzibar na ushawishi wa Abdulrahman Babu katika fikra za siasa za mrengo wa kushoto zilizokuwa Zanzibar miaka ya 1950 hadi kufikia mapinduzi mwaka wa 1964.

Hashil Seif anaeleza toka mwanzo nia ya Makomredi kupindua serikali ya Zanzibar na kuweka utawala utakaofuata siasa za ki-Marxist.

Kwa ajili hii anaeleza namna Ali Sultan aliyekuwa kiongozi katika ZNP alivyofanya mpango wa mafunzo ya kijeshi kwa makomredi kwenda Cuba kujitayarisha kwa jukumu hili.

Kitabu kinaeleza msuguano uliokuwa ndani ya ZNP hadi kupelekea Babu kufungwa kwa kile Comarade Hashil anaeleza ni njama baina ya wahafidhina ndani ya ZNP na Waingereza.

Juu ya haya yote Hashil ameeleza kwa utulivu mkubwa haiba za wanasiasa wa Zanzibar kama Ali Muhsin ambae kamtaja kwa sifa yake ya "Zaim," yaani Kiongozi, Muhammad Shamte, Ahmed Mohammed Nassor Lemki, Khamis Abdalla Ameir, Badawi Qulatein kwa kutaja wachache ...naendekea kukisoma kweli hiki si kitabu cha mtu kukikosa...

In Shaa Allah nitarejea nikikimaliza.

1550547124594.png


Kulia ni Hashil Seif, Amour Dughesh na aliyekaa ni Mussa Maisara
 
View attachment 1026088

Hiki kitabu ninakisoma hivi sasa.

Bado sijakimaliza lakini nimejifunza mengi katika historia ya Makomredi wa Zanzibar na ushawishi wa Abdulrahman Babu katika fikra za siasa za mrengo wa kushoto zilizokuwa Zanzibar miaka ya 1950 hadi kufikia mapinduzi mwaka wa 1964.

Hashil Seif anaeleza toka mwanzo nia ya Makomredi kupindua serikali ya Zanzibar na kuweka utawala utakaofuata siasa za ki-Marxist.

Kwa ajili hii anaeleza namna Ali Sultan aliyekuwa kiongozi katika ZNP alivyofanya mpango wa mafunzo ya kijeshi kwa makomredi kwenda Cuba kujitayarisha kwa jukumu hili.

Kitabu kinaeleza msuguano uliokuwa ndani ya ZNP hadi kupelekea Babu kufungwa kwa kile Comarade Hashil anaeleza ni njama baina ya wahafidhina ndani ya ZNP na Waingereza.

Juu ya haya yote Hashil ameeleza kwa utulivu mkubwa haiba za wanasiasa wa Zanzibar kama Ali Muhsin ambae kamtaja kwa sifa yake ya "Zaim," yaani Kiongozi, Muhammad Shamte, Ahmed Mohammed Nassor Lemki, Khamis Abdalla Ameir, Badawi Qulatein kwa kutaja wachache ...naendekea kukisoma kweli hiki si kitabu cha mtu kukikosa...

In Shaa Allah nitarejea nikikimaliza.

View attachment 1026089

Kulia ni Hashil Seif, Amour Dughesh na aliyekaa ni Mussa Maisara
inshallah.
tutajie kinakopatikana na bei
 
Kitabu kitasaidia kukuzaa balanced perspective of severely distorted history of Zanzibar. Nadhani role ya comrades mapinduzi ya Zanzibar haijaangazwa kwa undani zaidi or downplayed . Matarajio kitabu kitatujuza zaidi.
 
Umma part ndio walistahili kutawala Zanzibar kwani walijianda kisomu na kijeshi lakini Karume aliwazidi kidogo ila akawa na ndoto ya kuwamaliza kwa kuwaua kina Hanga, Babu na wengineo walikuwa na akili ambazo zingeipeleka mbali nchi hii.
 
Back
Top Bottom