Mind your existence: Binadamu si kwa ajili ya dini bali dini kwa ajili ya binadamu!

Mind your existence: Binadamu si kwa ajili ya dini bali dini kwa ajili ya binadamu!

Wa Busiya

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
326
Reaction score
67
Ningekuwa na uwezo wa kuwakusanya waumini wa dini za Kiislam na Kikristo ningewalaumu kwa kugeuka kuwa watumwa wa dini kiasi cha dini kuwapelekesha kinyume na kusudi la Mungu kuhusu uumbaji wa mwanadamu. Kama dini hizi ni za kweli na Mungu Muumba mbingu na nchi anazithamini dini hizi basi tuzitumie kumwomba mahitaji ili atujalie. Yeye anaweza kushusha moto, kuleta amani, kunyamaza ili watu wake wajifunze jambo fulani, kuruhusu jaribu hata kama ni vifo; kwa kifupi Mungu anajua yote anaweza yote. Je, sisi na dini zetu hizi mbili zilizogeuka janga la dunia tunaweza kumsaidia Mungu kwa kuuana ili baadaye tumwone Mungu?

Ninawasihi watanzania waumini wa dini hizi tuishi kwa kuzingatia uhalisia ulivyo; dini hizi tumezitengeneza na kuzistawisha sisi. Tusije tukasaidia kuchipusha mbegu ya chuki ambayo adui anaipanda kwa ujanja mkubwa kupitia dini. Tukumbuke kuwa Mungu alituumba ili tumwabudu yeyesiyo dini zetu. Tujiulize dini hizi zilianza lini? Je, waliotutangulia ambao tunawaita baba/Babu zetu wa imani: Adam, Eva, Nuhu, Ibrahim, Lutu, Daudi na wengineo walikuwa waumini wa dini gani? Je, Ukristo au Uislam ulikuwepo? Tukataeni propaganda za watu wanaotaka kukaa madarakani milele. Tatizo la nchi yetu siyo dinifulani au chama fulani cha upinzani.

Kama kweli tunaipenda nchi hii tuitendeeni haki kwa kukipa kura chama cha upinzani ili tuweze kufanya tathmini ya mfumo huu wa vyama vingi kama unafaa au haufai. Tukiendelea kukilea CCM tutakuja kujuta baadaye kwa sababu hata CCM hawaelewi kwa nini hali ya Watanzania ni taabani kwa sababu wao hawafikirii watakula nini bali wanawaza kuwekeza kwa ajili ya vitukuu wakati watanzania tulio wengi tunawaza tutakula nini leo. Tusichonganishwe kwa dini wala kabila; tuwwalaani watu wanaohubiri chuki kwenye majukwaa ya siasa na nyumba za ibada. Mbarikiwe watanzania wenzangu na Mungu awape kufahamu kinachotakiwa kufanyika 2015
 
Serikali ndo tatizo ya hii issue ya udin Tanzania, Uchochezi wa kidini hivi sasa unafanywa hadharani kabisa bila wahusika kuchukuliwa hatua imefikia mahali ndugu zetu waislam wanaweka video nje ya misikiti inayoonyesha jinsi gani muislam akiua mkristo mmoja wao wanaita (kafiri), atapata thawabu.
Na hii inafanyika waziwazi bila hata kificho.
Na baadhi ya waumini wa misikiti hiyo ni viongozi wakubwa tu wa serikal, mwisho na wao wanasema Takbir sijui ndo nini?
 
kabla hujaanza kuleta mtizamo wako ungeelewa kwanza nini maana ya neno 'DINI' na unaposema mungu alituumba ili tumuabudu wala tusiabudu dini unakosea sana. toka awali kuanzia nabii ADAM, mungu aliweka utaratibu wa watu wa namna ya kuishi na kumuabudu, huu utaratibu wa kuishi na kumuabudu ndio unaitwa 'DINI' kwahiyo ni lazima ufuate dini flani ambayo mungu ameiteremsha ili uweze kumfikia, kwahiyo dini na mungu vinaenda sambamba. mfano. Musa alipewa Taurati, ndani ya taurati kulikuwa na maelekezo ni namna gani watu wa israel waishi ili kupata baraka za MUNGU, vilevile YESU alipewa Injili, na Muhamadi Quran, vitabu vyote vinamuongozo ni namna gani mtu aishi ili aweze fika mbinguni. hivyo 'DINI' ni mfumo mzima wa maisha ya mwanadamu. swali, dini ipi ndio bora mbele ya MUNGU? hapo kila mtu na imani na yake na hapo ndio chanzo cha migogoro, na ukitaka kuishi bila kufuata 'DINI' hakika utapotea mfano. BABA YAKE IBRAHIMU alikataa kufuata yale mwanawe Ibrahimu aliyomweleza kwamba ndio mfumo ambao MUNGU anahitaji ufuatwe, yeye akasema anafuata mila zao, hivyo akawa amekiuka muongozo wa MUNGU wa Ibrahimu na MUNGU ndiye anajua adhabu gani ya kutoa juu yake...hivyo UKRISTO, UISLAM haya ni majina tu yanayobeba neno DINI, umeyotoa wapi haya majina, soma kitabu chako cha imani ili kujiridhisha kama kweli neno UKRISTO au UISLAM limetajwa ndani ya kitabu chako kama neno ambalo unatakiwa ulitumie kuwakilisha DINI yako.
 
Kwa Heshima na Taadhima kwa wanaJF & Walimwengu;
Natoa Taazia kwa wa Tanzania, Msiba huu umetufundisha mengi. Mheshimwa ulilosema ni la maana kwa jamii yote pamoja na serikali yetu kutafakari. tuungane mikono kwa pamoja Tufungue nyoyo (inner heart ) zetu kwa pamoja
Na TUOMBE kwa MWENYEZZI MUNGU MMOJA atusaidie na atuondolee janga hili. Amin/Amen kweli hatuwezi kupata suluhisho au muarobaini wa kutatua masaibu (mushkeli) huu kwa kuchambua au kuchakachua ya fulani au ya shetani.
Siye wote niwatendaji wa imani zetu, zilizo jaa. kifupi wandugu serikali lazima ifahamu hili. " Desperation " hufanya watu kutenda mambo yasiyo kubalika kijamii " Ni jumkumu la Raia wote kuwa na ushirikiano na kukubaliana kwa busara na hekima kama Taifa lilivyo jengwa.
 
kabla hujaanza kuleta mtizamo wako ungeelewa kwanza nini maana ya neno 'DINI' na unaposema mungu alituumba ili tumuabudu wala tusiabudu dini unakosea sana. toka awali kuanzia nabii ADAM, mungu aliweka utaratibu wa watu wa namna ya kuishi na kumuabudu, huu utaratibu wa kuishi na kumuabudu ndio unaitwa 'DINI' kwahiyo ni lazima ufuate dini flani ambayo mungu ameiteremsha ili uweze kumfikia, kwahiyo dini na mungu vinaenda sambamba. mfano. Musa alipewa Taurati, ndani ya taurati kulikuwa na maelekezo ni namna gani watu wa israel waishi ili kupata baraka za MUNGU, vilevile YESU alipewa Injili, na Muhamadi Quran, vitabu vyote vinamuongozo ni namna gani mtu aishi ili aweze fika mbinguni. hivyo 'DINI' ni mfumo mzima wa maisha ya mwanadamu. swali, dini ipi ndio bora mbele ya MUNGU? hapo kila mtu na imani na yake na hapo ndio chanzo cha migogoro, na ukitaka kuishi bila kufuata 'DINI' hakika utapotea mfano. BABA YAKE IBRAHIMU alikataa kufuata yale mwanawe Ibrahimu aliyomweleza kwamba ndio mfumo ambao MUNGU anahitaji ufuatwe, yeye akasema anafuata mila zao, hivyo akawa amekiuka muongozo wa MUNGU wa Ibrahimu na MUNGU ndiye anajua adhabu gani ya kutoa juu yake...hivyo UKRISTO, UISLAM haya ni majina tu yanayobeba neno DINI, umeyotoa wapi haya majina, soma kitabu chako cha imani ili kujiridhisha kama kweli neno UKRISTO au UISLAM limetajwa ndani ya kitabu chako kama neno ambalo unatakiwa ulitumie kuwakilisha DINI yako.

Unaposema yesu alipewa injiri unamaanisha nn??
 
Ndugu sijakuelewa,
Unataka kusema kitu gani hapa?
'
Uwesema watu wamekua watumwa wa dini kinyume na kusudi la Mungu,ni kusudi gani hilo?Na watu wamekua watumwa wa dini gani?
'
Nani amekuambia dini zote zina mtazamo mmoja?Ni wapi umesoma kuwa Ukristo ni dini?
'
Ni watu wa dini gani wanaouana kwaajili ya Mungu?Je ni Mungu yupi huyo?
'
Usiwajumlishe wote wanaoenda kusali kuwa ni wafanya fujo
'
Dini gani imetengenezwa na binadamu?Kwa ushahidi gani?
'
Umedai kuna chuki iliyopandwa na adui,ni chuki gani?Na huyo adui ni nani?
 
Ningekuwa na uwezo wa kuwakusanya waumini wa dini za Kiislam na Kikristo ningewalaumu kwa kugeuka kuwa watumwa wa dini kiasi cha dini kuwapelekesha kinyume na kusudi la Mungu kuhusu uumbaji wa mwanadamu. Kama dini hizi ni za kweli na Mungu Muumba mbingu na nchi anazithamini dini hizi basi tuzitumie kumwomba mahitaji ili atujalie. Yeye anaweza kushusha moto, kuleta amani, kunyamaza ili watu wake wajifunze jambo fulani, kuruhusu jaribu hata kama ni vifo; kwa kifupi Mungu anajua yote anaweza yote. Je, sisi na dini zetu hizi mbili zilizogeuka janga la dunia tunaweza kumsaidia Mungu kwa kuuana ili baadaye tumwone Mungu?

Kwanza kabisa:

1. Kama ungefahamu maana ya Ukristo, usinge sema Ukristo ni DINI.

2. Tueleze kwa ushaidi, kwanini Mungu aliumba Binadamu?

3. Ukisha tupa maeleza ya sababu za uumbaji wa binandamu, kama zipo au la, tueleze tena, kwanini unamlaumu Mungu?
 
Toa neno dini weka WOKOVU. Wokovu kwa Mwanadamu na Si Mwanadam kwa Wokovu nikiwa na maana ya kwamba Mungu alitupenda sisi na Si sisi tukampenda yeye, na upendo huu umejidhihirisha kwa kumtoa mwanae wa pekee ambae wanadam wengi wamemkataa ila MUNGU alieumba Mbingu na Nchi amemkubal, na wote waliompokea YESU wamefanyika kuwa Wana wa Mungu. Yohane 3:16-17, Warumi 10:9-10.
 
Back
Top Bottom