Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,048
- 22,790
Duniani kuna mipaka ya ajabu sana ambayo wengine wetu huwanda hatuielewi. Mipaka hii ina historia zake, leo hii nitaweka ramani za baadhi ya mipaka hiyo ya ajabu, halafu siku nyingine nitajadili historia za mipaka hiyo. kama unaifahamu mipaka mingine ya ajabu, tufahamishe hapa.
Kuna mipaka miwili ya ajabu pale eneo la Jibrota (Gibraltar) kati ya Uhispania na Morocco. Kama umewahi kutembelea uhispania au Morocco unaweza kuwa umekutana na mipaka hiyo.
Wa kwanza uko ndani ya Uhispania ambapo kuna peninsular ndogo iliyomegwa kutoka jiji la La Línea de la Concepción na kupewa jina Gibraltar ambayo siyo mali ya Spain bali ni sehemu ya Uingereza. Ukiwa upande La Línea de la Concepción na ukataka kuingia Gibraltar lazima uonyeshe passport yako.
Mpaka wa pili uko ndani ya Morocco ambapo jiji la Ceuta kwenye kona ya Morocco limemegwa na kuwa mali ya uhispania. Ukitoka ndani ya Morocco kuingia jiji hilo lazima uonyeshe passport yako, na uwe na viza.
Sehemu nyingine yenye mpaka wa ajabu ni kati ya India na Bangladesh. Sehemu kubwa ya Bangladesh imezungukwa na india, na mpaka baina ya nchi hizo mbili umepindapinda sana. Kuna sehemu nyingine unapinda ili kumega sehemu ndani ya india na wakati mwingine unapinda ili kumega sehemu ndani ya Bangladesh.
Mpaka unaostaabisha sana ni ule unaozunguka eneo la Dahagram ambalo ni la Bangladesh lakini lote liko ndani ya India. Yaani mtu kutoka Dahagram kwenda makao makuu ya nchi huko Dhaka lazima avuke mipaka miwili, kutoka Dahagram kuingia India halafu tena avuke mpaka mwingine tena kutoka India kuingia Bangladesh.
Kwa bahati nzuri wameelewana kiasi kuwa India inawaruhusu watu wa Dahagram kuvuka mpaka kupitia Tin Bigha Corridor kuingia kwao Bangladesh bila kuhitaji passport wala viza.
Mipaka mingi ya Marekani ni mistali iliyonyooka tu. Mpaka kati ya Marekani na Canada kutokea bahari ya Pacific hadi maeneo ya maziwa makuu ni mstali uliyooka. Ukishafika kwenye maneo ya maziwa kati ya Jimbo la Minnesota kwa Marekani na Jimbo la Ontario kwa Kanada ndipo unaaza kupindapinda.
Njia yote kuanzia pale hadi kuingia bahari ya Atlantiki imepindapinda na sehemu nyingie zimepinda kiajabu ajabu ila ninataka kuleta sehemu kati ya Jimbo la Minnesota na lile la Ontario ambapo kuna peninsula mbili za Elm Point na NorthWest Angle zimemegwa kutoka Canada na kuwa sehemu za Marekani.
Mpaka sasa ile peninsula ya Elm point haikaliwi na watu bali ni msitu tu, ila kule NorthWest Angle kuna miji yenye wakazi kadhaa wanokaribia elfu kumi ambao wakitaka kwenda makao makuu ya jimbo lao huko St Paul-Minneapolis kwa gari, ni lazima wavike mpaka waingie Kanada kwanza ndipo wavuke mpaka tena kutoka Kanada kuingia Marekani tena.
Zamani kulikuwa hakuna haja ya kuwa na passport ila baada ya 9/11 ni lazima wawe na passport ingawa hawahitaji kuwa viza.
Mipaka ya nchi za Ulaya imetokana na himaya za kizamani sana zilizojengwa kwa kupigapigana vita, kwa hiyo mipaka yao imepinda pinda sana kutoka na jiographia ya eno la Ulaya.
Bara la ulaya ndilo linaloongoza duniani kwa kuwa na mipaka ya ajabu ajabu. Mmojawapo wa ajabu zaidi ni ule kati ya Uswisi na majirani zake. Ndani ya Uswisi kuna eno linaloitwa Büsingen am Hochrhein ambalo limemegwa kutoka Uswis na kuwa mali ya Ujerumani, eneo hili ni sehemu ya jimbo la Baden-Württemberg ndani ya Ujerumani.
Mkazi wa Büsingen am Hochrhein akitaka kwenda makao makuu ya jimbo lake kule Munich ni lazima avuke mpaka aingie Uswisi kwanza halafu avuke mpaka wa uswis tena ndipo afike Ujerumani
Mpaka mwingine ndani ya uswis wenye utata ni kati yake na Italia ambapo mji wa Campione d'Italia umemegwa ndania ya Uswisi na kuwa sehemu ya Jimbo la Como la Italia. Mkazi wa Campione d'Italia akitaka kwenye makao makuu ya jimbo lake Como, ni lazima avuke mipaka mwili kama ilivyo kwa yule wa Büsingen am Hochrhein.
Bara la Ulaya lina mipaka mingi sana ya ajabu likifuatiwa na Bara la Asia. Kama unfahamu mipaka mingine ya ajabu iweka hapa kwa ajili ya kuongezeana maarifa.
Kuna mipaka miwili ya ajabu pale eneo la Jibrota (Gibraltar) kati ya Uhispania na Morocco. Kama umewahi kutembelea uhispania au Morocco unaweza kuwa umekutana na mipaka hiyo.
Wa kwanza uko ndani ya Uhispania ambapo kuna peninsular ndogo iliyomegwa kutoka jiji la La Línea de la Concepción na kupewa jina Gibraltar ambayo siyo mali ya Spain bali ni sehemu ya Uingereza. Ukiwa upande La Línea de la Concepción na ukataka kuingia Gibraltar lazima uonyeshe passport yako.
Mpaka wa pili uko ndani ya Morocco ambapo jiji la Ceuta kwenye kona ya Morocco limemegwa na kuwa mali ya uhispania. Ukitoka ndani ya Morocco kuingia jiji hilo lazima uonyeshe passport yako, na uwe na viza.
Sehemu nyingine yenye mpaka wa ajabu ni kati ya India na Bangladesh. Sehemu kubwa ya Bangladesh imezungukwa na india, na mpaka baina ya nchi hizo mbili umepindapinda sana. Kuna sehemu nyingine unapinda ili kumega sehemu ndani ya india na wakati mwingine unapinda ili kumega sehemu ndani ya Bangladesh.
Mpaka unaostaabisha sana ni ule unaozunguka eneo la Dahagram ambalo ni la Bangladesh lakini lote liko ndani ya India. Yaani mtu kutoka Dahagram kwenda makao makuu ya nchi huko Dhaka lazima avuke mipaka miwili, kutoka Dahagram kuingia India halafu tena avuke mpaka mwingine tena kutoka India kuingia Bangladesh.
Kwa bahati nzuri wameelewana kiasi kuwa India inawaruhusu watu wa Dahagram kuvuka mpaka kupitia Tin Bigha Corridor kuingia kwao Bangladesh bila kuhitaji passport wala viza.
Mipaka mingi ya Marekani ni mistali iliyonyooka tu. Mpaka kati ya Marekani na Canada kutokea bahari ya Pacific hadi maeneo ya maziwa makuu ni mstali uliyooka. Ukishafika kwenye maneo ya maziwa kati ya Jimbo la Minnesota kwa Marekani na Jimbo la Ontario kwa Kanada ndipo unaaza kupindapinda.
Njia yote kuanzia pale hadi kuingia bahari ya Atlantiki imepindapinda na sehemu nyingie zimepinda kiajabu ajabu ila ninataka kuleta sehemu kati ya Jimbo la Minnesota na lile la Ontario ambapo kuna peninsula mbili za Elm Point na NorthWest Angle zimemegwa kutoka Canada na kuwa sehemu za Marekani.
Mpaka sasa ile peninsula ya Elm point haikaliwi na watu bali ni msitu tu, ila kule NorthWest Angle kuna miji yenye wakazi kadhaa wanokaribia elfu kumi ambao wakitaka kwenda makao makuu ya jimbo lao huko St Paul-Minneapolis kwa gari, ni lazima wavike mpaka waingie Kanada kwanza ndipo wavuke mpaka tena kutoka Kanada kuingia Marekani tena.
Zamani kulikuwa hakuna haja ya kuwa na passport ila baada ya 9/11 ni lazima wawe na passport ingawa hawahitaji kuwa viza.
Mipaka ya nchi za Ulaya imetokana na himaya za kizamani sana zilizojengwa kwa kupigapigana vita, kwa hiyo mipaka yao imepinda pinda sana kutoka na jiographia ya eno la Ulaya.
Bara la ulaya ndilo linaloongoza duniani kwa kuwa na mipaka ya ajabu ajabu. Mmojawapo wa ajabu zaidi ni ule kati ya Uswisi na majirani zake. Ndani ya Uswisi kuna eno linaloitwa Büsingen am Hochrhein ambalo limemegwa kutoka Uswis na kuwa mali ya Ujerumani, eneo hili ni sehemu ya jimbo la Baden-Württemberg ndani ya Ujerumani.
Mkazi wa Büsingen am Hochrhein akitaka kwenda makao makuu ya jimbo lake kule Munich ni lazima avuke mpaka aingie Uswisi kwanza halafu avuke mpaka wa uswis tena ndipo afike Ujerumani
Mpaka mwingine ndani ya uswis wenye utata ni kati yake na Italia ambapo mji wa Campione d'Italia umemegwa ndania ya Uswisi na kuwa sehemu ya Jimbo la Como la Italia. Mkazi wa Campione d'Italia akitaka kwenye makao makuu ya jimbo lake Como, ni lazima avuke mipaka mwili kama ilivyo kwa yule wa Büsingen am Hochrhein.
Bara la Ulaya lina mipaka mingi sana ya ajabu likifuatiwa na Bara la Asia. Kama unfahamu mipaka mingine ya ajabu iweka hapa kwa ajili ya kuongezeana maarifa.