Mipango miji Ilala wamewezaje kuruhusu mgahawa wa kienyeji kujengwa mbele ya Hotel ya Johari Rotana?

Mipango miji Ilala wamewezaje kuruhusu mgahawa wa kienyeji kujengwa mbele ya Hotel ya Johari Rotana?

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Leo nimepita mjini kati Posta, Dar es Salaam, muda kidogo sijatembelea mjini kati, nikashangaa kuona mgahawa wa kienyeji (Mama Ntilie) umejengwa mbele ya jengo la mwalimu Nyerere Foundation ambapo kuna hoteli ya Johari Rotana, kwenye geti la kuingilia kwenye Hotel.

Johari Rotana ni 5 stars Hotel, wamekezaji wameweka pesa nyingi sana kuwekeza pale halafu, cha ajabu halmashauri ya jiji la Ilala imeruhusu mtu aweke genge la chakula mlangoni kwa hotel kubwa namna ile, hii inaingia akilini kweli?

Ukiachilia kuharibu mandhari ya mji kwa ujenzi wa hovyo hovyo, mgahawa ulioko mlangoni kwa Hotel kubwa namna ile ni kutowatendea haki wawekezaji wa ile hotel lakini pia kutokuitendea haki foundation ya mwalimu Nyerere.

Mamlaka ya mipango miji waliwezaje kutoa kibali cha ujenzi wa ule mgahawa mbele ya mlango wa hotel ya Johari Rotana?
 
Mama Ntilie hana friji kwa hiyo chakula chake ni fresh. Siyo kama cha hotel
 
Pichaaa pichaaaa pichaaaaaaaaa!!!!!!!!! Sio wote humu tunaijua hiyo johari rotanaa
 
Posta
Leo nimepita mjini kati Posta, Dar es Salaam, muda kidogo sijatembelea mjini kati, nikashangaa kuona mgahawa wa kienyeji (Mama Ntilie) umejengwa mbele ya jengo la mwalimu Nyerere Foundation ambapo kuna hoteli ya Johari Rotana, kwenye geti la kuingilia kwenye Hotel.

Johari Rotana ni 5 stars Hotel, wamekezaji wameweka pesa nyingi sana kuwekeza pale halafu, cha ajabu halmashauri ya jiji la Ilala imeruhusu mtu aweke genge la chakula mlangoni kwa hotel kubwa namna ile, hii inaingia akilini kweli?

Ukiachilia kuharibu mandhari ya mji kwa ujenzi wa hovyo hovyo, mgahawa ulioko mlangoni kwa Hotel kubwa namna ile ni kutowatendea haki wawekezaji wa ile hotel lakini pia kutokuitendea haki foundation ya mwalimu Nyerere.

Mamlaka ya mipango miji waliwezaje kutoa kibali cha ujenzi wa ule mgahawa mbele ya mlango wa hotel ya Johari Rotana?
Posta ilipoteza hadhi yake kipindi cha magufuli aliruhusu mambo mengi hasa machinga mama ntilie kufanya kazi kule

Japo nampenda magufuli ila aliharibu kwenye swala la kila mtu kufanya biashara anavyotaka yeye yaani popote

Sass hapo johari rotana wapo wengi tu wanalisha watu wa vipato vya chini kama amejenga amekosea ila ninavyojua mimi kila mchana mama ntilie wa city center huwa wanakuja wamebeba masufuria ya wali kwenye kirikou gari kisha wanakuja kuuza na kusepa hawapikii kule city center..... sasa kama wameanza kupika basi kazi ipo
 
Screenshot_20240914-085050_Google Go.jpg
 
Back
Top Bottom